CEO SIKIMBII TENA NITAVUMILIA SEHEMU YA 4 Tunaendelea na tulipoishia ………. "Kwanini hupokei simu zangu?" aliuliza yule mdada huku anazidi kumsogelea Naseer
kwasababu wazazi walisema tuwe pamoja? huoneshi kunijali, kunithamini wewe mkaka mimi ni mzuri sikosi mwanaume ila nimebaki na wewe kwa sababu ya wazazi wetu basi", mimi na huu umbea wangu nikasema "ooh kumbe ni wachumba haina shida: Naseer akamjibu "kwahyo unahisi ni mwanamke wangu huyo?" alijibu uku anarudi nyuma na kuweka sawa suti yake akaendelea kusema "hivi Ramla niongee mpaka lini kwamba kuna muda wa kuongea mimi na wewe na kuna wakuwa nipo busy na kazi kwan una shida unataka kupajua kwangu kwani wewe si nimekujengea? nyumba nikiwa na shida na wewe ntakuja kwako, mbona unanifuata mpaka kazini mhh ?mbona unakua sio msikivu etty" aliuliza kwa kupanic Ramla akasema "kwani mimi si mpenzi wako?, naruhusiwa kwenda na wewe popote ninapotaka…
kukufata popote ulipo ni haki yangu: akajibu Nasser "kwanini kama umepiga sijapokea kwanini hujatuma sms?", wakaendelea kuzozana kweli mpaka nikawa nahisi kichwa kinaniuma sana hatimae Ramla aliondoka hadi nikahisi nimepumua nikawa najiuliza anawezaje kuishi na mwanamke wahivi jamani🤔🤔 mhh hapana ……
Muda ulienda ukafika muda wa kuondoka, nikatoka na Naseer , ila tulivyofika nje akamwambia dereva anipeleke mpaka nyumbani yeye kuna sehem anaenda sikuhoji hata nikimuhoji mimi ni nani kwake, nikawa nimefika nyumbani nikaingia ndani ndy kuwasha simu nakutana na sms ya Kareem ndefu kinoma yan inasema…..
(Sms; kwahiyo kisa huyo mwanaume uliompata ana hela ndio maana simu zangu unakata na mwisho wa siku unanizimia kabisa simu si ndy , yaani umeninyima since tupo chuo mpaka leo, leo unaenda kumpa huyo boya wako ambae umekutana nae kwa bahati mbaya tena kwenye ajali, fanya hivi kila mtu afany yake, lakini hili utalilipia Nasma)…
Ile sms ilinitisha sana kwakweli yaani sikutaka kuamini kwamba mwanaume ninaempenda kiasi hiki ananiiacha🥺🥺 kirahisi rahisi tu jaman nilimchukia Naseer ghafla kama asingenikataza kupokea simu wakati ule labda Kareem asingeniacha, nikasahau kabisa kujiuliza kajuaje kama nilimsaidia mtu na bado nipo nae mpaka hiv sasa tena ninaishi kwake, nikamchukia mkaka wa watu wakati ni mpenzi wangu ndy angetakiwa kusubiri maelezo kutoka kwangu, nampigia Kareem anatumika means ameni block asee nililia🥺😭😭 jaman mhhh nililia sana ……
Lakini mpaka muda huo Naseer hajarud na sijui kaenda wapi ila mimi sikujali wala nini nikawa busy na mambo yangu nikaamua kwenda kula kwa sababu mlango unafunguliwa kwa password na Naseer anaijua hivyo sikua na wasi wasi hata kidogo….
Usiku ulipita na asubhi ikaingia nikaamka nikajiandaa natoka sebleni namkuta Naseer kalala kwenye kiti nikamuamsha "sir mbona umelala hapa?" , Naseer akashtuka kutoka usigizini akanamby "leo hakuna kwenda officine pumzika tuu", sikuitika wala sikufanya chochote nikageuza moja kwa moja chumbani ninapolala , nikafika nikatoa simu na hiv pale ni free wifi ni mwendo wa kuperuzi tu mguu juu😁😁…
Ulipita muda sasa ni mchana nikainuka nikapike, kabla sijafika jikoni naskia Kama kuna mtu jikoni ndy kuchungulia namkuta ni Naseer ypo anapika na hivi nina hasira🤨 nae nahis yeye ndy sabab za mimi kuachana na mpenzi wangu kwa sababu ya sheria zake za hovyo pale officine nkaganda tu namtizaama kwa hasira kweli sijui hata nimfanye nini ili aumie kam ninavyoumia saa hizi, yan nakumsaidia kote haya ndy malipo kweli? nilizidi kukasirika kwakweli yaani ambae angefungua moyo wangu kuutizam angejua jinsi hasira yanguu ilivyoo juu ya yule mwanaume yaani namchukia sana najua asilimia mia yeye ndy sababu ya mahusiano yangu kuvunjika , akageuka akanitizama akanambia "karibu tupike" sikuwa na hiyana nikasogea mpaka jikoni Naseer alinitizama kwa makini na kuniuliza "upo sawa?" nikajibu nipo sawa asijali, tukawa tumepika tumemaliza tukasonga mezani, kwenye meza Naseer akaniuliza "kwani Nasma upo sawa kweli?" nikamjibu "ndio kwani kuna nini?" , akanitizama sana usoni huku mimi natizama chini akanambia "haupo sawa, nambie kinachokutatiza kuwa huru" nikajikuta naropoka "nataka kuacha kazi", nilisema kwa msisitizo mkubwa, alinitizama akauliza yani siku ya kwanza kuanza kazi ndy unataka kuacha kazi nilimjibu kwa ujasiri kweli "ndio" , akanitizama akaniambia "nipe sababu kwanini unatak kuacha kazi wakati ndio siku ya kwanza kazini? nipe sababu" nikaanza ongea kwa uchungu🥺 na kwa kujiamini kweli yaani "ndio kwasababu kazi yako imenifanya mahusiano yangu yamevunjika , kisa ulikataa nisipokee simu, mpaka nimeachwa umefurahi si ndy? wee upo na mahusiano yako lakini mimi nateseka hapa umefurahi sasa?" niliongea kwa hasira mpaka machozi yanatoka😭😭 , Naseer akanitazama kwa makini akanisogelea akanikumbatia🫂 kwa nguvu haponatamani nimtoe ila kwa upande mwingine nahitaji hilo akanambia hivi "kosa ni la kwangu au la mpenzi wako?, angekua anakupenda kweli angekusikiliz ila anaonekana alikwa anakutaftia sababu tu ya kukuacha" , wee nilihisi kama ananichawia nikazidi kulia 😭😭🥺muda huo bado nimemkumbatia🫂 Naseer, mara simu yangu ikaita namba ngeni nikapokea , taarifa nilizopata nilihisi kuishiwa pawa kilio kikazidi mara kumi yake😭😭😭😭😭…
ITAENDELEA……..
Full 1000
Whatsp 0784468229
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
