GENERAL SILI SILALI JUU YAKO SEHEMU YA 09 Kisha niliinuka taratibu na kuondoka zangu
"Laura tafadhari utafanya kilamtu ajue kuwa unampenda General, hembu fanya uzifiche hisia zako japo kidogo tuu"
Nilikaa kimya sikumjibu kitu, ila Nancy aliendelea kusema:
Naomba shuka chini twende ukale, haraka twende acha kuwa mjinga"
Nikainuka na kumwambia Nancy huku machozi yakinitoka:
"Unajua Nancy ninavyo mpenda General Ethane"
"Najua kipenzi changu lakini usiwe hivyo, jikaze uitengeneze na kesho yako kwanza, pamoja na kumpenda huyo General, na je vipi kama ameoa inamaana maisha yako wewe ndio basi tena eeh!?
Nilikuwa kimya tuu namtizama kisha nilimjibu:
"Lakini aliniambia hajaoa bado"
"Unawezaje kumuamini mtu umekutana nae muda mfupi tuu Laura jamani"
"Lakini Nancy mapenzi sikuzote watu huseama niupofu nami nahisi kupofuka kwakweli, ila nakuahidi nitajitahidi kujituliza, lakini tulifanyie kazi swala la kumpata General bado moyowangu unateseka hata nikisikia mtu kamtaja jinalake tuu, na kuhusu Catrine huwa hanitishi mimi hata kidogo, na alivyo mpuuzi hawezi kuwa na General hata kwa sekunde moja, General niwangu mimi pekeangu"
Niliamka tukaenda kumalizia kula chakula nakisha tuliagana na kwenda kulala, siku zilisonga nilibadilika kwa kujikaza, lakini ndani ya moyo wangu udhaifu wangu ni General, lakini Nancy alipambana kuhakikisha nafanikisha, hadi siku tunafanyiwa sherehe ya kuhitim mafunzo yetu ilifika, kulikuwa nawageni wengi sana pamoja na ndugu jamaa na marafiki, tukiwa hapo nilikuwa nawaza sana kwani ndio tunatoka na General tangu ameondoka, nitafanyaje sijaweza hata kuwasiliana nae tangu ameondoka, niliona nimfuate mkuu wa kikosi changu kuongea nae, nilimkuta akiwa yupo na viongozi wengine, lakini nilimuomba kuzungumza nae kidogo pembeni, alikubali na kutoka nikamuambia:
"Mkuu samahani kwanza kwa kukutoa pembeni"
"Hakuna shida Laura, ulikuwa unasemaje"
"Mkuu nilikuwa nashida na namba ya General, tafadhari kama unayo nisaidie"
"General mbona yupo njiani anakuja hapa, sio muda atafika utamuomba mwenyewe akija"
Yaani huwezi amini nilivyosikia hiyo taarifa, moyowangu ulipata amani hakika ilikuwa ni taarifa nzuri sana kwangu haijawahi kutokea, nilimshukuru kwa taarifa hata yeye alielewa tuu, kwani nilifurahia sana kisha nilimfuata Nancy na kumuambia:
"Nancy huwezi amini General yupo njiani anakuja"
"Wow! Achabasiii nani kakuambia"
"Hivii unajua nilijitosa kumfuata mkuu wa kikosi namba saba, na kumuomba namba ya General Ethane, akaniambia mbona yupo njiani anakuja na kuhusu namba nitamuomba mwenyewe, huwezi amini furaha niliyokuwa nayo baada ya kupewa hiyo taarifa kipenzi, ninafuraha sana yaani sana namsubili kwa hamu, leo nitamuambia nitamuambia kilakitu"
"Natumai utafurahi zaidi"
"Kabisa kipenzi asante sana kwa kuwa namimi siku zote, mungu akulinde"
"Usijali kipenzi"
Nikiwa naongea kwa furaha hapo na rafiki yangu Nancy, mjomba wangu alikuja karibu yetu na kuniambia:
"Naona unafuraha sana uncle, leo tunarudi nyumbani wote sindio"
"Kabisa uncle"
"Ok basi endeleeni kufurahia nipo palee nimekaa sawa?
"Sawa uncle"
Mimi ninakaa na mjomba wangu pamoja na shangazi yangu , mamaangu alimkabizi mjomba kwani hakuwa na uwezo wa kunilea na kunisomesha, na ndio maana mjomba ndio kaja kwenye sherehe za mimi kuhitimu mafunzo ya kijeshi, mjomba wangu ananilea vizuri sana na kunipa kila nitakacho, bahati mbaya yeye hana uwezo wa kupata mtoto, ndio maana hunichukulia mimi kama mtoto wake mwenyewe, ananidekeza hatari niombe nini mimi napewa kilakitu, nilitaka mimi kuja jeshini japo kuwa yeye hakutaka alijua nitateseka sana, lakini alikubali tuu kishingo upande, basi bwana wakati sherehe zinaendelea kwa mbali niliona gari ya General Ethane inapaki, nakisha alishuka na kwenda kwenye siti aliyopangiwa, nilikuwa natamani hata nikamkumbatie, lakini sio rahisi mbele za watu hapo hivyo nilijizuia, hadi tunamaliza sherehe na kuruhusiwa tuondoke na wazazi wetu, General aliinuka na kwenda ofisini nilimtoroka mjomba na kumfuata General, kabla sijaingia walikuja viongozi wengine walikuwa na vikao vyao, wakati huo mjomba alikuwa ananitafuta nimeenda wapi watu walianza kuonfoka, mjomba alinikuta nipo pembeni ya ofisi akaniuliza:
"Unafanya nini sasa Laura tuondoke"
"Mjomba nilikuwa namsubili General kunajambo nataka kuongea nae"
"Nilitaka tupitie kwa bibiako muda unaenda kipenzi"
Nilifikilia kisha nikaona ngoja nimruhusu aende nitamg'ang'ania General atanirudisha tuu, nikamuambia"
"Mjomba unaonaje utangulie kisha nikisha ongea nae General tutaondoka wote kwani nae anaenda dar"
Mjomba wangu ananiamini sana hakufikilia kabisa kama kutakuwa na mahusiano, ananijua mimi siamini katoka mahusiano, akakubali nakuamua kuondoka, mwisho wa siku watu wote walikuwa wameondoka, na viongozi ndio wakatoka mida ya saa kumi na mbili kwenye kikao, nilikaa kwenye kigiza hivi hakuna alieniona mimi ndio nilikuwa nawaona, General alitoka na alikuwa anaelekea moja kwa moja kwenye gari yake ili aondoke, nilimfuata nyuma kwa nyuma alipo fika kwenye gari yake akiwa anafungua mlango wa gari, nilimkubatia kwa nyuma.
Je General atafanyaje akijua Laura kwani alishaamua kusonga mbele baada ya kukataliwa endeleeni kufuatilia............
WhatsApp 0742133100
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi