GENERAL SILI SILALI JUU YAKO SEHEMU YA 17 na 18 0742133100
GENERAL alinituliza hapo na kunitoa kwenye hali niliyokuwa nayo, kisha tulianza kupiga story mbali mbali kutuhusu sisi wenyewe, kisha nilikumbuka na kumuambia:
"Hayasasa nipe zawadi yangu uliyoniambia umeniandalia"
"Ooh! nikweli ngoja nikupe mpenzi wangu, unajua ulinivuruga ulivyokuja, ulikuwa unahali mbaya sana, sipendi kuona ukilia mpenzi sipendi mtu yeyote akuumize sawa?
"Asante mpenzi wangu "
Kisha alienda kwenye gari na kuja na kimfuko kidogo kizuri, ndani kuna box nzuri ya zawadi, kisha alinipa hako kamfuko na kuniambia:
"Haya fungua mpenzi"
Nilifungua kile kifuko na kutoa box iliyokuwepo ndani yake, kisha nikatoa na kuifungua ndani ya box, nilikuta mkufu mzuri wa gold ambao unakidani chenye herufi yamwanzo ya jinalangu, nilifurahi sana kwani kwangu ilikuwa ni zawadi nzuri mno, na yathamani sana, kisha nilimkumbatia na kumshukuru nikamuambia:
"Ninzuri sana nimeipenda asante"
"Asante wewe kwa kuipenda, kwani ningumu sana kujua kitu kipi kitakuwa kizuri, hasa kwa mwanamke umpendae, nafurahi kama nimefanikiwa kuufurahisha moyo wamtu ninaempenda, Laura nakupenda sana kutoka ndani ya moyo wangu, wewe ni wathamani mno amini hivyo"
"Asante mpenzi wangu"
"Haya tuagize nini utapenda ili tule"
"Chochote mpenzi wangu, wewe agiza mimi nitakula"
Kisha General aliagiza mchemsho wa mbuzi na ndizi tulikula ilikuwa tamu sana pamoja na juice ya nanasi nilifurahia nikasahau matatizo yaliyonikuta asubuhi tulipo maliza kula tukaingia kwenyegani na kuanza safari alitaka kunirudisha nyumbani lakini nilimuambia:
"Hapana kwasasa sitaki niwakute wapo macho nataka nifike niwakute wapo chumbani kwao"
"Utwapa wasi wasi lakini kipenzi"
"Hapana hawakuwahi kujali kuhusu mimi baada ya kumjua mama mzazi nitakuwa najisikiaje?
"Basi kipenzi naona bado haupo sawa"
Niliona nibadili mada kwa kumuuliza kuhusu mambo ya kikazi:
"Ethane vipi nikipangiwa kazi mkoa utanifuata au ndio utanitelekeza?
"Nawezaje kuuterekeza moyo wangu kipenzi siwezi hata kidogo hivyo nitatafuta namna yakuwa karibu nawewe tuu"
"Wow! Asante mpenzi"
"Unaonaje twende fukweni tukale ice-cream utafurahia huko"
"Kweli eeh! Basi twende"
Tulienda hadi siku inaisha ilikuwa nisiku ngumu mno, alinirudisha nyumbani mida ya saa tatu hivi usiku, nilipofika nilinyata na kuingia chumbani kwangu, kumbe shangazi aliniona nikiingia, na kisha nilienda kuoga na baada ya hapo nilipanda kitandani kulala, baadae shangazi alikuja na kunitizama na kisha aliondoka, baada ya siku chache tuliyaongea yakaisha, ila kiukweli sikuwa nataka kumuona mama mzazi kabisa niliamua hivyo, maisha yalisonga mbele ilifika muda tulipangiwa vituo vyakazi, ambapo nilipangiwa hapa hapa dar, nilifurahi sana nikaanza kwenda kazini nikiwa ndani ya sare za jeshi, niliweza kuwa karibu na General Ethane pamoja na rafiki yangu Nancy, tulifurahi mno, siku moja ilikuwa ni siku ya weekend, nilisema nikashinde na General Ethane, kwani huwa nammis sana kutokana na ubize wa kazi, nikiwa nyumbani kwake niliandaa chakula na kisha tulikula pamoja, na sikuhiyo nilimis sana shoo, hivyo Ethane hakuninyima alinipa tena yamaana niliifurahia sana, tulipo maliza tulioga pamoja nakisha tukiwa tunavaa nguo huku tunacheza, mara simu ya Ethane iliita, kuitizama ilikuwa inayoka kwa mamaake dodoma, aliipokea na kuongea nae mamaake, katka mazungumzo yao kunajambo naona halikumpendeza Ethane, hivyo alimuambia mamaake:
"Nitakupigia tutaongea badae sio sasa"
Ila mama nahisi aliendelea kusisitiza kuongea muda huhu, Ethane aliikata simu na kuizima kabisa, nikamuuliza:
"Mbona hivyo kwani mama Ethane anataka nini?
"Aah! Wewe achana nae"
"Baby usichukie ndio mzazi unapaswa kumuelewa, na msikilize kisha umfanyie kile anataka ili iwe baraka kwako mpenzi wangu"
"Sawa kipenzi"
Niliona ameitikia tu basi ila hakuwa sawa kabisa, nilitafuta namna yakumfanya afurahi nilikuwa namchekesha chekesha, ilituu asiwe katika hali aliyikuwa nayo, tukaenda sehemu za bich na tukaanza kukimbizana, ilituu nimfanye awe sawa nilimchangamsha kiukweli, kisha muda ulikuwa tayari umeenda, Ethane alinichukua na kunirudisha nyumbani kwetu, naye akarudi nyumbani kwake, ndipo alipopata nafasi ya kuongea na mamaake vizuri, alimpigia simu na kuanza kuongea:
"Mama hapana mimi tayari ninae mtu ninampenda nae ananipenda, tafadhari sitaki tena matatizo"
"Nakuambia huyu anaadabu nimtoto wa rafiki yake babaako, utafurahi ukimuona kweli nakuambia, nimrembo sana mwanangu '
"No mama, achana na hayo mambo"
Inaonyesha mama tayari anataka Ethane aende kuoa huko dodoma naye hayupo tayari kuniacha namimi
Je nini kitajiri hapo endelea kufuatilia ..............
GENERAL SILI SILALI JUU YAKO
SEHEMU YA 18
0742133100
Siku moja Ethane alinichukua na kunipeleka moja kwa moja hadi dodoma yumbani kwao, nilimkuta mamaake alinikaribisha vizuri, na kisha Ethane alinitambulisha;
"Laura huyu hapa nimamaangu mzazi, mama huyu ni Laura ndio mwanamke ninae kwenda kumchumbia nampenda sana"
Nilinyoosha mkono kumpa mamaake na kumuambia:
"Nimefurahi kukufahamu mama"
Aliitikia yakutafuna tafuna, hata sauti haikutoka vizuri nilishindwa kumuelewa kabisa, nilielewa huenda ndio sauti yake ilivyo, tukiwa bado tupo hapo dodoma siku kama yatatu hivii, Ethane alikuwa katoka kaenda mjini, walikuja wageni hapo nyumbani alikuwa mmama mmoja na mdada mmoja, aliwaribisha vizuri na kisha aliniita mimi:
"Laura hembu wasikilize wageni hata kinywaji"
Nilifanya kama alivyosema, japokuwa kuna wahudumu hapo nyumbani, niliwauliza wote nakisha nilienda kuwaletea, baada ya hapo mama Ethane aliendelea kuongea na wageni wake, mimi nilienda chumbani kwetu kujipumzidha, haikuchukua muda Ethane nae aliingia, alipofika sebreni alimsalimia yule mgeni mmama na binti yake, kisha alikuja chumbani nilipokuwa mimi aliniletea zawadi nikazipokea kwa furaha, akaniuliza:
"Uko poa lakini?
"Ndio baby niko poa"
Kisha tukiwa tunaongea ongea alikuja muhudumu yaani mfanyakazi na kuniambia:
"Boss Ethane mama anakuita yupo sebreni "
"Nakuja mpenzi"
Aliniaga na kwenda kumsikiliza mamaake alichomuitia, alipofika hapo mamaake alimuambia :
"Hembu kaa hapo nikutambulishe"
"Huyu ni mke wa mzee kilie yule aliekuwa rafiki wa babayako, unamkumbuka?
"Ndio namkumbuka, karibu sana mama nyumbani"
Ethane alimpamkono na kumkaribisha huyo mama nyumbani, kwa heshima na upendo, kisha yule mama aliitikia:
"Asante sana mwanangu, umekuwa sana baba jamani, nimuda mrefu haupo ndio maana sikuoni"
"Aah! Nikweli majukumu yakazi ndio yanatubana mama"
Kisha mama Ethane aliendelea kutoa utambulisho:
"Na huyo hapo ni binti yake anaitwa Veronica, nimrembo anaheshima sana mwanangu, ndio nimependekeza tukamchumbie kwaajili yako"
Wakati anaongea hilo neno nilikuwa nipo karibunao kabisa, kwani niliona Ethane anachelewa kurudi, nikaona nimfuate hapo hapo uenda wanapiga story tuu namimi nikajumuike nao, lakini nilichokisikia kiukweli kilinifanya nijihisi vibaya sana, nilijiona kama nimefosi kuja kwenye hiyo nyumba ambayo hawanitaki, niligeuka na kuanza kurudi taratibu kwa bahati mbaya nikajikwaa, kwani nilikuwa natetemeka kwa hasira, ndio nikawashtua Ethane alikuwa wa kwanza kuinuka kutizama, akaniona naishia kurudi chumbani, hivyo aliona mambo tayari yameharibika hapa akaanza kunifuata, nilipofika nilichukua begi langu na kupakia kilicho changu, kisha nilitokea mlango wa nyuma haraka haraka, hata Ethane alipofika hakunikuta alianza kukimbia kunifuatilia, nilidandia piki piki mbio kuelekea stend ya mabasi, kwa bahati nzuri nilibahatika kukuta gari ndio ilikuwa inatoka tuu, nikaingia hivyo hivyo hata siti sikupata nilikaa pale mbele karibu na dereva, tukaondoka Ethane alipofika stendi akaambiwa nimeingia kwenye gari iliyotoka robo saa iliyopita, Ethane alijisikia vibaya sana aliumia mno, na kisha alitoa simu na kuanza kunipigia sikupokea ile simu, iliita na kuita sikutaka kabisa kupokea, kisha Ethane alirudi nyumbani na kumkuta mamaake pamoja na yule binti Veronica, ila mamaake Veronica alikuwa kaondoka, aliingia kimya kimya hadi chumbani kwake, alipofika alijilaza kitandani chali akiwa anamawazo sana, yule binti Veronica akaingia huko chumbani na kujikalisha karibu na Ethane, Ethane alikuwa na hasira sana akamuambia kwa sauti ya chini chini:
"Toka chumbani kwangu"
Yule binti alimtizama na kuzani mzaha akajifanya anamsogelea ili amfanyie masag alipomgusa tu Ethane aliinuka na kumshika mkono kwa nguvu akamuambia:
"Wewe bado mdogo sana, hivyo tafuta mchumba utakae mpenda nae atakupenda, acha kusikiliza wale wazee wanakupotosha, haya inuka nenda kwenu"
"Lakini mimi tayari nimekupenda mbona usihofu kuhusu hilo"
"Wewe nimesema nenda kwenu tafadhari"
Yule binti aliinuka na kuondoka zake alipofika sebreni, mama Ethane akamuuliza:
"Mbona unaondoka imekuwaje?
"Kanifukuza hataki hata kuniona"
"Usijari twende huko huko, mimi ndio nimeamua asijifanye anajua sana"
Kisha walienda hadi chumbani kwa Ethane na kumuita:
"Ethane.! Huyu binti nikwaajili yako nimekuambia, nausimfukuze atalala nawewe hapa huyu nimkwe wangu mimi"
"Mama mimi ndio mwenye chumba simtaki mtu chambani kwangu, kwanza istoshe umefanya hadi Laura kaondoka, sitaki nasema huyu mtu wako"
Mama Ethane alifosi kumuingiza binti Veronica kwa Ethane, mwisho Ethane alichukua begi lake na kutoka, aliwasha gari yake na kuondoka zake"
Je nini kitajiri kwa Ethane na Laura endelea kuifuatilia.............
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi