GENERAL SILI SILALI JUU YAKO SEHEMU YA 03 Walipo fika Catrine alikuwa chini na mimi nilikuwa juu nampiga Catrine
"Niache nimuonyeshe, atanizoea mimu huyu"
Mkuu wakikosi alinishika kwa nguvu, huku akinizuia nisiende, na kuniambia:
"Acha usiwe hivyo Laura , tulia nimesema tulia"
Ndipo ikasikika sauti moja tuu sio kali ila alisema
"Muachie tumuone"
Nilishtuka, na kugeuka haraka kwani nisauti niliyokuwa naijua kabisa, kutizama vizuri alikuwa General, asikuambie mtu nilinywea kama kitunguu majii kwenye mafuta, General alisongea hadi nilipokuwa na kisha akasema:
"Wewe tena"
Nilibaki kimya siku mjibu kitu, nilisimama kwa nidhamu, nikiwa naogopa sijui nini tena kitanikuta awamu hii, General aliniambia:
"Nifuate"
Nakisha aliondoka, namimi nilianza kumfuata kama alivyo sema, na wenzangu waliingia kitandani kulala kimya kimya, nilikuwa najiuliza sijui awamu hii atanipa zoezi gani, na tayari usimu umesha ingia, tulipofika nje aliniambia:
"Laura, sura yako na matendo yako haviendani kabisa, unaumli gani wewe?
"Nina miaka ishirini na tatu mkuu"
Nilijibu kwa sauti yaupole kabisa, kisha General alitabasam na kuniambia:
"Mimi kipindi ninaumli wako nilikuwa najitahidi sana kuwa na nidham, ili nifanikishe kilakitu, lakini ona wewe kila mala unakumbana na adhabu tuu, haya sasa utasimama hapo, mikono inyooshe juu kama unaita mvua, na usiishushe mpaka nitakapo kuruhusu, kisha aliwaruhusu viongozi wa vikosi hapo waende kupumzika, kiongozi wangu kikosi namba saba akamuambia:
"Muheshimiwa General, unaonaje ukaniachia mimi huyo, wewe nenda upumzike maana utakuwa umechoka sana, tangu umefika huku pumzika hata mala moja"
Nilifurahi kusikia hivyo, kwani nilijua mkuu wa kikosi hatonitesa kama huyu General, lakini General alinitizama na kisha akasema:
"Huyu hapana natakiwa nimnyooshe mimi mwenyewe, kidogo awe na nidhamu, maana anaonekana hana nidhamu kabisa"
Niliposikia hivyo, nilizidi kuchukia nikamuambia:
"Lakini mbona mnaniadhibu mimi pekeangu eeh! nawakati alienianza mmemuacha"
General aligeuka, na kumuambia mkuu wa kikosi changu:
"Wewe nenda kapumzike, huyu niachie mimi"
Mkuu wangu wakikosi aliondika, na kuniacha hapo General, kisha akaniambia:
"Endelea na zoezi nililokupa"
Kisha alichukua kiti na kukaa pembeni, huku akiwa na chupa yake ya whisky, na akiwa bize na simu yake, nili endelea kufanya kama nilivyoambiwa, kiukweli nilikuwa ninaumia sana, hadi nilijiku natokwa namachozi, lakini General alikuwa anajifanya yupo bize hanitizami, mwisho nilimuambia:
"Ninajisikia kiu, nahitaji maji yakunywa"
Alinitizama nakisha aliinuka na kuniletea maji yakunywa, akaninywesha maji kwa mkono wake yeye mwenyewe, kwani hakutaka nishushe mikono chini, lakini sikuhishia hapo nilimuambia tena:
"Nahitaji kujisaidia haja ndogo"
"Jisaidie tuu, hakuna anaekuona hapa, kwanza kunagiza"
Kisha aliendelea kunywa kinywaji chake, nilianza kulia kwa kwa kwikwi, yaani mikono ilikuwa inauma sana, na sitakiwi kuishusha chini hata mala moja, nililia sana, kwakweli General ni mkatili sana hana huruma hata kidogo, kisha akaniambia:
"Shusha mikono chini, na kisha chuchumaa chini"
Nilifanya kama alivyoniambia, kisha akaniambia:
"Anza kuruka kichura chura, hapo mpaka kuleee mbele, na kisha urudi hapa fanya hivyo bila kupumzika, naomba uanze mara moja, acha kulialia hapa sio nyumbani kwenu"
Nilianza kuruka huku nalia, jasho likinitoka hatari, nilijikuta namchukia sana General, hadi nilijisemea kimoyoni moyoni:
"Nakuchukia sana"
Tangu kaingia ni ananipa adhabu tuu mimi, niliruka kichula kwa muda mrefu sana, hadi mapaja yalikuwa yakitetemeka, ila General hakujali hadi alipo maliza kunywa mvinyo wake, alisimama na kuniambia:
"Haya inuka"
Niliendelea kuruka kwa hasira, kama sikumsikia, kiukweli nilikuwa nahasira sana muda huo, alinitizama kisha akaniambia kwa sauti ya ukali:
"Inuka na uje hapa"
Nikainuka kwa tabu sana, miguu haikuwa sawa kabisa, ilikuwa inatetemeka nusu nianguke, nikaanza kutembea kumfuata huku ikitetemeka miguu yangu, nilijikuta nikaangukia miguuni kwa General, nnikaanza kujizoa niinuke tena, akaona ainame anisaidiae kusimama, kiukweli nilimpushi mkono kwa hasira, na kufosi kwa nguvu hadi nilifika juu, huku machozi yakinitoka kwa hasira, akaniambia:
"Nenda ukalale, ila alfajiri nataka nikukute kwenye tizi uwanjani"
Nikaanza kuondoka huku akinitizama, nilitembea hatua chache tu nikaanguka chini, mapaja hayana nguvu kabisa yanatetemeka, alinifuata anisaidie nilipomuona nilimuambia:
"Usiniguse tafadhari"
Alitabasam kwa jeuli, nakisha akaondoka kuniacha nilitambaa hapo hadi nilipokaribia bwenini, kiongozi wa kikosi changu alikuwa hajalala, alikuwa akitoka nje anachungulia kisha analudi ndani hivyo hivyo, ndio alipokuwa anachungulia akaniona nipo chini natambaa, alikuja na kunisaidia kuinuka, akanipeleka kitandani kwangu, akaniambia:
"Nilijua tuu, kwa General hutotoka salama, haya inuka upumzike sasa"
Nilimuomba kitu kimoja:
"Naomba nisaidie maji yamoto mkuu, nataka nijikande kidogo mapaja, lasivyo sitoweza kuinuka alfajiri, nakuomba"
"Sawa, ngoja nikakuchukulie jikoni"
Alienda jikoni na kunichemshia maji, kisha alikujanayo, nilimuomba bila aibu anisaidie kunikanda, nilichukua upande wa kanga nikajifunga kujificha sehemu za siri tuu, kuanzia kwenye hips kote nilimruhusu anikande, alikubali na kuchukua kanga akairoweka kwenye maji ya moto, na kisha alinikanda ilikuwa inauma sana, lakini aliniambia:
"Jikaze Laura, hili ndio jeshi"
Nilikuwa nalia kwa uchungu kiukweli, nilikuwa ninamaumivu makali mno, kisha mkuu alienda kuniletea dawa za maumivu, nikameza kisha, mkuu aliniambia:
"Haya lala"
Nikalala akanifunika vizuli shuka ndio kuondoka, alikuwa anatujali sana mkuu wa kikosi chetu, ndio maana alikuwa ananisubili ahakikishe nimeingia kulala kabisa, ndio akaondoka.
Endelea kufuatilia.........
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi