GENERAL SILI SILALI JUU YAKO SEHEMU YA 15
"Laura, nikuambie kitu?
"Ndio niambie mpenzi"
"Laura, wewe ni wathamani kubwa sana maishani mwangu, unajua kuwa siku ya kwanza tuu kukuona pale kambini, moyowangu uliniambia huyu ndio yule uliekuwa unamtafuta, na nilipo kusogelea hata mapigo yangu yamoyo yaliniambia kwa inshara kwani yalibadilika gafla, Laura nilijaribu kupingana na hiyo hali kwakujaribu kukuweka mbali nami, lakini hatma pia zilikuwa zinatukutanisha, kwani ile siku nilipokuambia ukae tule wote, nilifurahi sana huo muda niliuweka katika kumbu kumbu zangu, nakupenda Laura wangu"
"Naje mbona ulikuwa ukinitesa sana kambin
"Yote hayo niliyafanya ili nikuweke mbali namimi kujaribu kupingana na hatima yangu lakini nilikuwa nakutana tena nawewe hata nilipokutamkia kuwa nakupenda ilitoka ndani ya uvungu wa moyo wangu kabisa Laura"
"Kweli General Ethane?
"Ukweli baby"
"Hata mimi nilijihisi hivyo hivyo kama wewe mpenzi, nafurahi kama hadi leo hii tumekuwa wapenzi, nakuahidi sitokuumiza kabisa maishani kwangu, General Ethane nakupenda sana"
"Asante Laura"
Tuliongea mengi sana, japo kuwa mwanzo nilikuwa na hasira nae, lakini katika maongezi yake, alinifanya nikalegeza maamuzi, na kukili upendo wangu kwake, kiukweli Ethane ni mwanaume mwenye kila sababu yakupendwa na wanawake wengi, alikuwa nimzuri mwenye kuvutia kwa kila kitu, muonekano tabia yake na anajali sana, baada ya kuongea sana tulilala usingizi, hadi palipokucha nikiwa nimetoka kuoga navaa nguo ilinitoke, nilisikia mlango wangu unagongwa, hivyo nikatoka na kuufungua, kumbe alikuwa mjomba, nilimsalimia na kisha akaniuliza:
"Vipi hali yako kipenzi changu?
"Salama mjomba sijui wewe?
"Mimi nipo salama kabisa '
"Nafurahi kusikia hivyo, natoka sio muda tupate breakfast pamoja"
"Ok sawa lakini nilitaka nikapate mbele ya safari lakini kama unakuja basi nitapata nawewe nipo nakusubili dining"
"Sikucheleweshi lakini mjomba?
"Hakuna chakuharibu ratiba yangu kama upo wewe kipenzi changu"
"Asante mjomba"
Kisha nilienda kumalizia kujiweka sawa, na kisha nikatoka na kuelekea dining, shangazi nae alikuja na alipotukuta akasema:
"Inawezekanaje hamunialiki na mimi kwenye hii breakfast nzuri ya pamoja, eeh! mtu na babaake mna roho mbaya sio?
"Hapana sisi hatuna roho mbaya, kama upo tayari karibu nawewe ujumuike nasisi, maana kutokea huwa ni nadra sana, au sio mjomba?
Aliongea mjomba ila mimi nilibaki nikitabasam kisha nika sema:
"Kabisa mjomba, naomba iwe ni sheria sasa kilasiku asubuhi, muda saa moja kamili tukutane mezani itakuwa nzuri sana hasa kwa anaewahi kazini sio mjomba?
"Hakika kipenzi changu, nitakuwa naondoka na upendo wote duniani, na nitakuwa nafuraha sana"
"Wow! Ninzuri eeh! Safi sana haya dada naomba niletee maziwa ya moto yenye kahawa"
Aliongea shangazi tulitabasam tuu mimi na mjomba, kiukweli ilikuwa niasubuhi yakipekeee, kilammoja alikuwa na furaha haswaa, tulipata breakfast ya pamoja na kisha mjomba alituaga na kwenda kazini, tulibaki mimi na shangazi hapo mezani, shangazi akaniambia:
"Haya kipenzi changu, niambie kuhusu Ethane wako natamani kusikia"
Nilitabasam na kisha nikamuambia:
"Mama! Ethane ni mtu mstaarabu sana, mwenye upendo wakweli anaejali mno, na nimtanashati kwelikweli na sijui nimuelezee vipi, lakini nimwanaume aliekamilika kilasifa yupo vizuri"
"Mmh! Kwahiyo yupo vizuri kumzidi baba eeh!?
"Aaah! No hapana mama hafiki kwa mjomba bwana"
Tulicheka wote kwa furaha kisha shangazi akaniambia"
"Nafurahi kukuona unafuraha mpenzi, kiukweli nidua yangu siku zote upate mtu utakae mpenda wewe mwenyewe"
Niliinuka na kumfuata kwenye kiti chake shangazi na kumkumbatia, kisha nikarudi kukaa na kuendelea kuongea mambo mengine, tukiwa hapo kwenye viti vya dining, alikuja dada wa kazi akamuambia mama kuwa kunamgeni sebreni, hivyo mama aliniambia:
"Haya kipenzi baadae"
Aliinuka na kuondoka, namimi niliinuka na kwenda chumbani kwangu, alipofika sebreni shangazi alishangazwa na mgeni aliekuja, alikuwa ni mamayangu mzazi nimuda mrefu sana, leo ndio kakumbuka kama anamtoto ndio kaja kuniona, alimsalimia shangazi kisha akamuambia:
"Wifi zasiku nyingi?
"Salama sijui wewe?
"Nisalama kiukweli, sijui nyie pamoja na Laura nae anaendeleaje nisiku sijamuona sijui atakuwaje sasa?
"Mh! Leo ndio umemkubuka?
"Nimambo mengi yameyokea, ila leo nimeona nije kumuona, kaka nae hajambo?
"Hajambo, kwani hujawasiliana nae?
"Hapana sijawasiliana nae maana simu yangu haina vocha ndio maana"
"Ok sawa basi ngoja nimfahamishe kuwa upo hapa"
"Sawa lakini niitie Laura kwanza, ili nimuone sikunyingi sana jamani sijamuona binti yangu, atakuwa mdada mkubwa sasa"
Shangazi slibsdilika na kumjibu:
"Naomba twende hatua kwa hatua sawa?
Mama alitia macho hakumuelewa kabisa shangazi kwanini kapaniki namna hiyo.
Je nini kitatokea shangazi yake Laura atamtuhusu Laura akaonane na mama yake kirahisi hovyo baada ya muda mrefu alimfanya Laura kuwa kama binti yake eeh unatamani kujua endelea kufuatilia...........
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi