GENERAL SILI SILALI JUU YAKO SEHEMU YA 04 Kulipokucha tena alfajiri namapema, filimbi ilipigwa, wote tuliamka na kwenda mazoezi
Baada ya ukaguzi kukamilika, tuliruhusiwa kwenda kupata breakfast chap chap, dakika kadhaa wakati tunapata breakfast, nilijikuta nimeshika kikombe cha chai kinamoto kweli kweli hata kunywa nishida, nilipiga funda mbili tuu, kengere ikapigwa hapo hapo, ikabidi niache kunywa chai nakukimbia, nilijitahidi kiukweli, tukaanza kufanya mazoezi mbali mbali ya kijeshi, nikiwa kati kati ya mazoezi nilisikia naitwa, nikaitikia na kwenda alikuwa kiongozi wa kambi zote:
"Naam mkuu"
"Unajukumu lako ambalo tuliwapa jana, linaendelea hadi atakapo ondoka muheshimiwa General, hivyo unapaswa kwenda kufanya maandalizi ya mchana wake"
"Sawa muheshimiwa"
Japo kimoyo moyo nilikuwa najisemea mwenyewe,
"huu niuonevu mbona mwenzangu jana usiku hakuja, lakini kila mala mimi tuu, na wangejua huyo General simpendi hata kumuona"
Kisha niliambiwa niende kufanya maandalizi, niliondoka na kuelekea jikoni niliambiwa kitu cha kumuandalia, nikafanya kama walivyo sema, na nilipo maliza nilibeba na kukipeleka mezani tayari kwa kuliwa, muda ulikuwa umefika wa yeye kupata chakula, alienda kuambiwa, baada ya dakika chache alikuja kupata chakula, alipo fika na kuniona alinitizama na kisha alitabasam, nilimkaribisha:
"Karibu chakula"
Nilijawa na hasira kweli nilipo muona, lakini nikajikaza tuu, baada ya kumkaribisha akakaa, na kisha nilisogea kumchotea chakula kwenye sahani, nilipo maliza nilimkalibisha ale, nae akanikaribisha namimi, nilimjibu:
"Asante"
Kisha niliendelea kusimama pembeni, baada ya kuchota chakula na kukiweka mdomoni akaniambia:
"Laura, kwani wewe ulisomea mapishi"
Nilimjibu huku nikiwa makini:
"Hapana"
"Chakula chako nikitamu sana, na nakuomba ukae hapa tule wote sasahivi"
Nikamjibu:
"Asante bado ninashibe mkuu, wewe endelea tuu"
"Sasa hii ni amri sio ombi, kaa hapa na ule chakula nami"
Nilikaa kwa hasira na kisha nilichukua sahani na kupakuwa chakula kidogo sana nikaanza kula muheshimiwa akaniambia
"Pamoja na yoote, Laura mimi sio mchoyo, tafadhari furahia chakula chako, na naomba usinichukie namna hiyo sawa"
"Asante, ila mbona sikuchukii mimi"
Nilimjibu tuu, lakini ndani ya moyo wangu najua mimi mwenyewe, kisha niliendelea kula, nilikuwa nimechota chakula kidogo sana, alivuta sahani yangu na kuniongezea tena chakula huku akisema:
"Unasafari ndefu sana, na ili ufanikiwe uwe mkakamavu, unapaswa kula zaidi usionje, utafia kwenye mazoezi bule, sawa bint mdogo"
Milimtizama na kisha nilimjibu:
"Ila hiki sio chakula cha kruta, hichi ni cha muheshimiwa General, ndio maana sina uhuru nacho muheshimiwa"
Ksha alitabasam na kunijibu:
"Umekiandaa wewe mwenyewe, mimi sina roho mbaya hivyo, na kingine nimezoea kula na familia, hivi ninavyokula mwenyewe huwa naboreka tuu, nafurahi nikipata kampani kama hivi, tafadhari mambo ya kazi tusiyaweke mezani basi Laura eeh!
Kiukweli nilijisikia kutabasam, baada ya kusikia maneno yake, kisha aliniambia:
"Hupendenzi kununa nuna kabisaa, na kingine unasauti nzuri ya upole, kama sio binti mkorofi niliyemkuta jana anampiga mwenzie"
Nilimtizama machoni tukakutana macho kwa moacho nikajikuta naona aibu kwanza anajicho zuri limelegea linaita hatari ukikutana nalo lazima uhisi kitu lakini ni jicho lake lilivyo tuu nikainamisha uso wangu kwa aibu chini akaniambia:
"Laura, ninaonekana mkorofi sio, lakini mimi sio mkorofi bwana, arafu nafurahi utakuwa rafiki tangu, nisamehe kama nilikukosea sawa"
Nilishindwa hata kumuangalia tena, nilibaki nimeinamisha uso wangu chini tuu, huku nakula akanyoosha mkono na kunishika kidevu changu, na kuniinua huku akiniambia:
"Usinionee aibu, mimi tayari ni rafiki yako sawa Laura"
Nilitabasam tuu na kuendelea kula kisha alipomaliza kula aliniambia
"Asante kwa chakula kitamu sana, nakuacha ninakazi nyingi sana ofisini kwangu, nitawaona jioni huko mazoezini sawa Laura usinichukie tena"
"Sawa muheshimiwa"
Kisha aliondoka na kuniacha mwenyewe mezani, nilimalizia kula baada ya hapo nikatoa vyombo, na kupeleka jikoni kuvisafisha, nilipo maliza nikaelekea moja kwa moja mazoezi nilipokuwa, niliendelea na mazoezi kwa amani kabisa, kwani tayari muheshimiwa General kaniomba msamaha, kwa alicho nifanyia jana, hivyo niliona kweli pamoja na yoote sina budi kumsamehe, kwanza alikuwa ananikomaza kimazoezi, kwanini alinizingatia mimi tuu, nadhani kunanamna anataka niwe, hivyo sina budi kumchukia, nilikuwa najiambia mwenyewe kimoyo moyo tuu, sikuhiyo nilifanya mazoezi kwa morari nzuri sana, hadi mkuu wa kikosi changu alinifurahia, na kuniambia:
"Sikutegemea kama leo ungekuwa wa moto namna hii, kutokana na hali uliyokuwa nayo jana usiku, hivyo nilikuwa nahofu kuhusu siku yako ya leo itakuwa mbaya sana, lakini tofauti na nilivyo fikilia asante mungu haya endelea kupiga tizi"
Nilitabasam na kisha siku mjibu chochote, niliendelea tuu na mazoezi tuu, hatimae muda ulikuwa tayari umeenda, tunakaribia kwenda kwenye pared, nilijikuta nashauku ya kutaka kumuona muheshimiwa General tu, muda wote nilikuwa nageuka geuka tuu kutaka kumuona je amekuja kutuona, kwa gafla wakati nainua uso wangu kutizama kama kaja nilikutana nae uso kwa uso, nae alikuwa akinitafuta anione tulikutana macho kwa macho, nikajikuta naona aibu tena, sikujua ni hali gani tena inanitokea kwa huyu General, nikawa najisemea kimoyo moyo:
"mmh! Mbona wote nawatizama vizuri tuu, na sijikuti katika hali hii, kwanini iwe kwa General"
Kisha nikajisemea:
"Niujinga wangu tuu, hembu niendelee na mazoezi mimi"
Niliendelea kufanya mazoezi kisha General alitabasam na kuondoka zake, kwenda kuendelea kukagua vikosi vingine, nilitabasam pia nilipo muona anaondoka huku akitambasam, makruta wenzangu hawakuelewa ana tabasam kwanini, baada ya muda mfupi firibi ilipulizwa, tukatoka na kwenda moja kwa moja pared, tulipofika tufanya pared yetu hapo, kisha alitoa matangazo General na kuturuhusu tukaoge, kisha tukale chakula na kwenda kupumzika, nilikuwa nimechoka sana nilienda moja kwa moja bafuni kuoga, na nilipomaliza nilitoka na kwenda bwenini kwetu kubadili nguo, nilivaa suruali yangu na tisheti zote ni zahapo kambini, kisha nilikaa kitandani kujisomea vitabu vyangu, jioni hiyo alienda yule mwenzangu tulie chaguliwa wote, kwaajili ya kazi hiyo kumuandalia chakula muheshimiwa General, na mimi niliambiwa na mkuu wangu wakikosi nipumzike, hivyo nilikuwa nasoma kitabu changu lakini nikimkumbuka General najikuta natabasam pekeangu, mpaka kina Catrine na wenzie wakawa wananitizama, sikujali nilipo waona wakinitizama, niliendelea kujisomea mwenyewe, muda wa kwenda kula ulifika tukaenda kula chakula, na tulipo maliza kula tulirudi bwenini kupumzika, nikiwa nimejiegemesha kitandani nahuku ninasoma kitabu changu, alikuja mwenzangu yule tulie chaguliwa wote kwa kazi ya kumuuhudumia General, na kuniambia:
"Laura, unaitwa na General yupo kule kwake tulipomuandalia siku ile, sasa hivi"
Nikainuka na kuanza kwenda kina Catrine na wenzie wakaanza minongono na huku wakicheka walikuwa wakisema:
"Atakuwa anaenda kupewa adhabu tuu lazima, maana huyu hasikii, na General hampendi kabisa"
Sikuwajibu hata, nikaondoka zangu tu tulipofika nje, nilimuuliza yule mwenzangu:
"Nancy kwani ninaitiwa nini na General?
"Kiukweli sijui, na mimi tayari nimesha maliza kazi yangu, hivyo nakuacha nikapumzike sasa, haya usiku mwema Laura "
"Sawa usiku mwema Nancy"
Nilijiongelea mwenyewe kimoyo moyo:
"Mmh! Mimi tena mzee wa majanga, haya sijui nimefanya nini tena na leo, na sijui naenda kupewa adhabu gani huko tena ehe! Mungu nisaidie"
Endelea kufuatilia...............
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi