PILOT SITAKI INANIOGOPESHA SEHEMU YA 19 - 20
Nilikuwa najilazimisha hata kucheka mama aliniona ila akajua labda ni uoga tuu akaniambia mwanangu usijali bhana Kila kitu kutakuwa sawa na ndoa yako itapita vizuri tu nikawa namjibu kwakichwa saw, muda wa kuvaa nguo ukafika sema nilipendeza na nilivokazue zuri sasa mpaka raha. Ukafika sasa muda wa kwend kula viapo kanisani akaingia bwana harusi akiwa kaongozana na wadogo zake wawili ambao ni Jayson na Kendrick alafu ndo nikafata Mimi na babaangu alikuwa akinileta Yan Kila mtu alikuwa na furaha isipokuwa Mimi na Kendrick ndo tulionekana hatuna furaha kabisa. Baba akanifikisha mpaka pale mbele Kisha akanikabidhisha Kwa Freeman. Freeman akanishika mkono vizur. Akaja mchungaji pale akaubiri weee sie tuliwekea viti tukae Kwa pembeni yake na Kendrick nae alikuwa kakaa Kwa chini kabisa ukafika muda wetu wa kusimama sasa Mimi na Freeman tukasimama. Mchungaji akaanza na kuuliza je Kuna mtu anakipingamizi kabla sijaanza kuwapa viapo.
Kanisa zima likakaa kimya ila watu wote walishangaa pale ambapo Freeman alijibu ndio ninakipingamizi, watu wote wakabaki wengine wameshika midomo wengine wanatoa sauti za mishangao Mimi sasa Nikahisi labda sijamsikia vizuri nikatoka kile kitambaa cha bibi harusi ilinimsikie vizur akasema Tena Mimi Nina kipingamizi na kipingamizi changu sitaki kuoana na Lailat kwasababu zangu muhimu nikataka kuanza kulia ila Freeman akasema nataka mdogo wangu Kendrick ndo amuoe Lailat sasahiv achukue nafasi yangu. Yan Kila mtu alishangaa mpaka uyo Kendrick mwenyw alishangaa ni Nini kinaendelea wazazi wao wazazi wangu wote wakawa wanashangaa ila Kuna baadhi ya watu walikuwa hawashangai kama dada angu alikuwa hata hashangai yeye anatabasamu tu, Jayson pia alikuwa hashangai Wala nikama watu waliokuwa wakijua ni Nini kinaendelea. Dada akanifata Kwa nyuma akaniambia iyo ndo zawadi yangu kwako kweny harusi yako, nikamgeukia nikata nimuulize imekuwaje ila nikashikishwa mkono wangu na Kendrick alietushikisha ni Freeman mwenyw bila ya kulazimishwa na mtu yoyote.
Freeman akasema nyie wawili mnabaraka zangu kwenye ndoa hii Mimi kama kaka mtu nimeridhia muendelee na mahusiano yenu ambayo mlikuwa mkiyaficha Kwa muda sasa, nikamuuliza sasa vipi kuhusu wewe akasema Mimi msijali Nina wangu, anaingia sasa hivi tukaskia milango inafunguliwa tunaangalia ni nan anaingia Tena kanisani ni mdada mwengine anakuja akiwa kavalia shera na yeye kama Mimi akaja mpaka mbele kumbe ni yule mchumba wake wa mwanzo alirudiana nae na Leo hii nao wanafunga ndoa. Yan bila ata kuelewa ni nni ndoa zikafungwa na Bado sielewi Nini hicho wazazi nao walikaa kikao kifupi kabla ya ndoa kufungwa wakakubaliana kwasababu na sisi nao tulikuwa tukipendana mno ndoa ya kanisani ikapita.
Yan nilifurahi na sio Mimi tu Kendrick ndo usiseme jamani Mungu yupo mtu unaweza ukajikatia tamaa ila dakika za mwisho kabisa muda wa jioni ndo Mungu anakuonesha Mimi nipo. Tukaenda ukumbuni sasa kweny sherehe fupi Kisha baada ya hapo tukajiandaa kesho yake mie na mume wangu Kendrick tukaenda kula honeymoon kwenye hotel π¨, ambayo ilikuwa tofauti na walioenda shemej yangu Freeman na mkewe. Maisha yalikuwa mazuri Kwa upande wangu ila sasa usiku wa honeymoon jamani iv kwanini nilidanganyika π, ila anyway ndo mke wa mtu Mimi nishatumikia ndoaπ na nilimuhadithia dada Wacha asinichekeπ.
Tukamaliza saba zetu, tukarudi nyumbani tukakuta kwenye iyo nyumba yetu mpya Kuna Kila kitu Yan ndo Raha ya kuolewa kwenye familia zinazoelewa mda kama huu ningekuwa kwenye familia za chini Tena nchi za watu izi ningeteseka sana na pia Raha nyingine nimeolewa na boss wanguπ kazini naenda nikijiskia natena alikataa nisiende kazini nikafunguliwa kampuni kama mamaake alivo niahidigi kipindi cha freeman kile. Haukupita hata miezi miwili nikapata mimba π, nilikuwa naogopa kuzaa sema nilikuwa najaliwa sana mpaka Raha.
Wakat mimba yangu inamiezi minne, dadangu Jully nae shamrashamra zikaanza wakatangaza uchumba yeye na Mchumba wake boss wake. Yan mambo yalikwiva maana Kila mtu kaolewa na boss wakeπ.
Ndoa Yao pia ikapita, na pia mie na mume wangu Baada ya miezi tisa ya kumnyanyasa na mimba Nikajifungua a healthy baby girl.
MWISHO
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi