PILOT SITAKI INANIOGOPESHA SEHEMU YA 15
Nilivyonyamaza tuu dada akatupisha Kendrick akaanza kuniuliza kwani shida Nini dear nikamjibu hayakuhusu maana uyu nae siniligombana nae akanipigia magoti Kisha akatoa Pete kwenye mfuko wa koti alilovaa akaniuliza will you marry me? Nikabaki nimetoa macho hapo ndo machungu yakaongezeka moyoni nikatoka nikakimbilia chumbani nikaifunga na mlango nikaanza kulia, Kendrick akaja Kwa nje pale mlangoni akawa ananibembeleza ananiomba msamaha yeye kwaakili zake anajua nalia kwasababu ya siku Ile tuliogombana mpaka akaniambia Kuna mwanamke anampenda kumbe mwenzie nalia na yangu mambo mengine kabisa hata hayahusiani na hicho anachowaza yeye, akawa anasema Lailat Mimi Nakupenda wewe na hata sikuile ulionikuta naongea na John kuhusu mwanamke nilimpenda Kwa mara ya kwanz tu nimemuona alikuwa ni wewe sikuile dadaako alivokuleta ndo nikakupenda ghafla tu naomba usijiskie vibaya nilikumaansha wewe na hata kule hotelini nilikuwa nakuongelea wewe na si mwanamke mwengine yoyote lailata Nakupenda mwenzio.
Hapo ndo nikajua kumbe Mimi ndo nilikuwa naongelewa na kwel nilivoonganisha maelezo yake ni kwel sasa kumbe Kendrick ananipenda kwel hamna kipengele sasa nikimuwaza uyo kakaake ndo nachoka kabisa, dada alikuwa chumbani kwake alivyoona kelele zimezidi akaja na ufunguo mwengine wa ziada wachumbani kwangu akamfungulia Kendrick akaingia chumbani kwangu, nikashindwa kujizuia nikamkumbatia Kwanguvu maana wakati wote uo nilikuwa nimemnunia bila ya sababu nilimjudge bila ya kusikiliza akaniuliza umenisamhe nikamjibu ndio, akanikiss pale tukaongea kidogo ila sikumwambia kuhusu issue ya kakaake maana niliona hajui kitu chochote nikaongea nae kawaida pale tukapika stori zingine ila nilikuwa naonekana kabisa kuwa sipo sawa Hadi yeye alijua akaniuliza kwani Kuna shida yoyote maana nilikuwa na stress zimenizidia. Ila nikawa namjibu tuu hamna kitu akasema sawa, Tukaongea ongea pale jioni jioni akawa anaondoka akaniuliza vipi kesho kutwa unakuja kazini nikamwambia sipo sawa sidhan kama ntakuja ila sasa sijui nimuombe Nan ruhusa ya kuwa naumwa, akaniambia usijali ntashughulikia we tulia nyumbni mpaka utakapojiskia na kuhusu mshahara utakuwa unaingia vilevile.πhii ndo Raha ya kudate na mabossπ.
Alivyoondoka akaja dada sasa akawa ananiuliza sasa shogaangu utafanya Nini, nikamjibu yn hata sielewi Yan sielewi kabisa akasema we tulia tutapata tu namna usiwaze mdogo wangu nikamwambia sawa dada ila hili jambo ni kubwa na naona linaanza kunielemea mdogo wako, dada akaniambia usijali. Nikaenda kulala ila usiku nilivyolala sa sijui nilikuwa nawaza sana maana niliota ndoyo mbaya iyo nikamuote Freeman kafa Tena mbele yangu nikashtuka nikaanza kukemea uku nalia, Yan usingizi wote ukakataa nikampigia mama nikaamuadithia kuwa nimeota ndoto ivi na ivi, mama akaniambia mwanangu kemea iyo ndoto inamaanisha vibaya kuwa wewe ndo chanzo cha uyo mtu aliekufa pembeni yako. Mama alivyosema ivo nilishtuka π«’nikarudi Tena kukemea Kwa mara ya pili. kisha ndo nikalala kesho yake asubuhi dada akawa anajiandaa kwenda kazini Mimi nimekaa tuu simu ikaita kuangalia ivi ni namba ngeni nikapokea kumbe alikuwa ni babaake na Freeman, yule Mzee akaniambia mwanangu naomba uje hapa hospitali sasahivi Kisha akakata simu.
Sasa hapo ndo nikavurugwa kabisaaa ukichanganya na ndoto nilioiota usiku ndo nikavurugwa zaidi Yan mpaka dada akaniuliza Kuna Nini nikamwambia we niache kwanza ila jua naenda hospitali alipo Freeman, dada akatoka akaita Uber tukaenda hospitali kufika kule nikamkuta yule babaake Freemani yupo nje ya chumba alipo Freeman anatembea tembea anaenda anarudi Yan kama vile mtu aliechanganyikiwa alivyoniona Mimi akanifata akanipigia magoti Hapohapo njee namuuliza baba shida Nini na muda uo baba kanipigia magoti Kendrick nae ndo alikuwa amefika nilimpigia simu, baba akawa anasema mwanangu naomba umkubalie mtoto wangu Yan ukiingia tu hapo mkubalie laasivyo utaniulia mtoto Nikamuuliza Kuna Nini baba akasema Freeman kaandaa surprised akuchumbie tumemdanganya umemkubalia ndo hapo ndani anataka akuvike Pete kwaiyo naomba ukubali mwanangu hatakama sio kwaajili yangu basi Fanya kwaajili ya maisha ya mwanangu. Nikawa nashangaa kugeuka hivi nikamuona Kendrick analia Kwa hasira akaondoka nikabaki Mimi babaake na dada pale njee sielewi nichague Nini na kwanini nichague
Itaendelea....
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi