PILOT SITAKI INANIOGOPESHA SEHEMU YA 16
Nikawa Sina budi kukubali nilivokumbuka ndoto ya Jana nikaogopa asije Freeman akafa kwasababu yangu Mimi, nilivokubali yule baba alifurahi akataka Hadi kunibeba ingawa alikuwa Hana nguvu akaniambia twende sasa na ujifanye kama ulikuwa hujui kama ameanda surprise, nikamuuliza ila baba hapa si hospitali kwaiyo kaanda surprise hapa hospitali yule baba akasema Yan mwanangu safari hii amekupenda kweli kweli na hajapona vizur ila kalipia mahela mengi ilikupewa kibali afanye hichi kitu hapa hospitali, nikamwambia sawa eeeh Aya sawa. Nikaingia sas kama mtu haelewi Nini kinaendelea nikamuona mama kakaa pale kitandani ila sikumuona Freemani nikauliza mama freeman yupo wapi Hapohapo mlango wa chumba cha pembeni ukafunguka akatoka Freeman akiwa kavalia suti akaja moja Kwa moja kwangu akanipigia magoti akaniuliza will you marry me nikamjibu ndio uku natoa machozi ya uongo maana sikuwa najinsi alifurahi akanivika Ile Pete watu sijui hata walitokea wapi wakaanza kushangilia wengine wakawa wanarusha vile vimelemeta kumbe alikuwa kawaita Hadi wafanyakazi wenzangu wakina Jane, pendo, John watu kibao duuh.
Sema nikamkubali na kiss juuu, yule baba akauliza kwani Kendrick yupo wapi ndo hapo nikakumbuka Kendrick sijui ni Nini kilipata ghafla Raha ikapotea tabasamu likashuka Hadi Freemani alilingundua Hilo akaniuliza shida Nini mpenzi nikamwambia hamna kitu akaniambia basi usiwaze akanipiga kiss lingine pale mbele za watu ila hii mara ya pili roho iliniuma nikakumbuka kiss la Kendrick daaahπ nikawa najutia kidogo kidogo. Na Freeman hakutaka kuchelewesha Hapohapo akawatangazia watu waliopo hapo hospitali kuwa kesho kutwa Mimi na yeye tukafunga ndoa na kuhusu taratibu zengine na huku Tanzania zitafanyia kwasasa watu wameshatumwa nyumbni kwetu. Mmmh π³ nikamgeukia dada mbona haya mambo mengine siyaelewi Mimi, dada akanionesha ishara kuwa nitulie ila natuliaje wakati vitu vinavoongeleka sivielewi nikaomba nitoke njee nikawa nikatoka kuongea na dada, eti akaniambia wazazi wake na Freeman walimuomba namba ya mama na baba Toka muda na wameshayaongea Toka muda na Kila mtu anajua kuwa utaolewa hata uko nyumbani na kuhusu mahari Leo hii watoa mahari ndo wanatarajia kutua Tanzania.
Yan nilimkata jicho ilo hivi uyu dadaangu anakuwaje mbona ana kiherehere hivi Yan ananikeraaa, nilipandwa na hasira nikamuuliza kwani wewe mbona unahekaheka hivi na hii ndoa akaniambia mdogo wangu na Mimi nilikuja kuombwa kama wewe na ao wazazi wa Freeman, Yan sikutaka hata kumsikiliza nikatoka nikapiga simu nyumbani akapokea mama nikaanza kumlalamikia kumbe anajua Kila kitu ila usiku nampigia hakuniambia chochote Yan nilikasirika π‘mama akaanza kunibembeleza akawa ananiambia mwanangu we mkubalie uyo mkaka kuhusu kupendana mtapendana mkiwa kwenye ndoa maana anaonekana anaheshima sana, hakuanza kukutongoza wewe alianza kwanza na ushauri kutoka kwetu alishawai kumpigia babaako simu na hiki kitu ata dadaako hajui aliongea nae vizur babaako ndo akamshauri aongee na dadaako, juzi Tena wazazi wake wakatupigia ndo maana hatukuona sababu ya kwanini tumkatae mwanangu. Nikamjibu sawa mama ila moyoni moto ulikuwa unawakaπ₯, nilikuwa nawaza mengi sana sema nikaona Bora nisikilize wazazi.
Ingawa nilikuwa nampenda sanaaa Kendrick siku iyo ikapita nikarudi nyumbani shamra shamra za kesho uchumba wenywe sasa kuvalishana Pete sasa Kila mara Freeman ananipigia simu mpaka anakera, ila ndoa ikapelekwa Kwa siku moja ili wazazi wangu wapate muda wa kusafiria kuja uku marekani nilipo. Kipindi chote icho nikawa nikikutana na Kendrick anafanya kama hanijui na Iko kitu kilikuwa kinaniuma sanaaa Yan sanaaa. Ilikuwa ni siku moja kabla ya ndoa wazazi wangu walikuja Kila mtu ndugu zangu na yule dadaangu mkubwa. Nikawa nimetoka nimeenda kwakina Freeman muda uo alikuwa kashatoka hospitali.
Itaendelea...
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi