PILOT SITAKI INANIOGOPESHA SEHEMU YA 17 - 18
Sasa wakati uo nimeenda nikaja kufunguliwa mlango na Kendrick, na ilikuwa inaonekana nyumbani walibaki wao wawili tu na wafanya kazi, Alivonifungulia mlango mie nikapita moja Kwa moja mpaka ndani sikutaka kuongea nae maana yeye sianafanya kama hanijui ila Leo uvumilivu ukamshinda akaniuliza kwaiyo ndo unaolewa kesho n kakaangu, nikajifanya kama simsikii akaniambia Lailat usiolewe Mimi Nakupenda uku analia nikamgeukia nikakuta analia macho yashakuwa mekundu nikamwambia ungekuwa unanipenda sikuile ambayo babaako alikuwa anaongea na Mimi usingeondoka ungemwambia unanipenda na unataka kunioa ila wewe ukachagua kuondoka kwaiyo niache niolewe na mtu anaenipenda. Nilivosema ivo Kendrick akapiga magoti nikawa Bado naelekea chumbni Kwa Freemani, Kendrick akainuka akaja kunikumbatia Kwa nyuma akaanza kuongea uku analia ananiambia Lailat usiolewe Bado Nakupenda Lailat, Kuna namna nililimiss kumbato lake na ilikuwa inaniuma sana kuolewa na mtu nisiempenda sema ntafanyaje na ndoa ishatangazwa.
Siku Ile angeizuia ndoa sawa ila Leo kashachelewa nikawa najaribu kumtoa mikono ila wapi kaning'ang'ania mpaka nikamuuliza we umenikumbatia hivi shemeji yako kakaako akikukuta hapa akasema Lailat Kwa stage niliofika Mimi hata kaka akinikuta sijali Wala Nini nikamwambia sasa Mimi najali sitaki mpenzi wangu na mume wangu mtarajiwa akukute kwasababu ataninunia, nilivyomwambia Ivo Kendrick akatoa mikono polepole Yan kama mtu ambae hakutarajia jibu ilo kutoka kwangu, akaanza kuniuliza vipi kwani kanizidi Nini anakufanya zaidi ya nilivokufanyia Mimi au ananini kigeni Mimi Sina, hapo machozi na mie yashaanza kunitoka kabla sijamjibu floor ya juu Nikamsikia Freeman ananiita Lailat, nilishtuka na Kendrick nae alishtuka akafuta machozi haraka haraka na Mimi pia Kisha nikaaangalia juu Freeman akauliza oooh umekuja mpenzi nikajua hakusikia ivo nikamjibu ndio Kisha nikafata kwakule juu alipo nikamuacha Kendrick kanyong'onyea uyo Hadi huruma.
Freeman akaniuliza mbona umekawia kupanda huku juu nikamwambia Amna kitu, nilikuwa tu naongea na shemeji hapo chini, Freeman akasema sawa ila alionekana kapoa sana, nikamuuliza shida Nini akasema hamna kitu usijali nikamwambia sawa, nilikuwa nimeenda kwake kumuangalia akivaa suti anafananaje na yeye mwenyw aliomba niende nione anavopendezea akivaa suti kwaiyo sikuwa na budi kwenda akaavaa suti yake na alipendeza hapo nikaanza kuwaza hii suti kama angeivaa Kendrick daaah sema ndo haiwezekani Tena iyo nikabaki tu Nacheka Kwa uchungu, alivyomaliza kuijaribu tukakaa kama kidogo Kisha akanisindikiza mpka njee akamwambia dereva mmoja anirudishe nyumbani. Nikafika nyumbni nina stress ila mkubwa ni mkubwa tu, mama akaniuliza kwani shida ni Nini mbona umechange ghafla wakati umeondoka hapa vizuri tuu mwanangu, nikamjibu hamna kitu naomba nikapumzike ili kesho make up ikae vizur mama akasema sawa kwaiyo nikaenda kulala ila usiku mzima namuwaza Kendrick tuu.
Mpaka kesho yake asubuhi nikaamshwa mapema Tukaanza kuelekea saluni nikaandaliwa vizuri mama alikuwa anafuraha uyo Nilivyomaliza kufanyiwa make up sasa ikafata muda wa kuvaa nguo ya harusi ili tuelekee kanisani, mama wakt uo watu wanaanda nguo na yeye akapata muda wakuongea na Mimi mambo mawili matatu Kisha akaanza kupiga vigelegele kama mnavowajua wamama wakiafrica kwenye sherehe, ila nilikuwa Sina Raha kabisaπ.
Itaendelea...
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
