DOZI NI SAA 7:00 MCHANA 03
"Oscar kamwambie huyo doctor wako akupe dawa haraka sana siwezi kuishi kwenye hii hali",Martha aliongea.
"Lakini mke wangu.....
ENDELEA NAYOO..
"Lakini mke wangu tulia kwanza nikupe habari njema",mawazo yetu yalikuwa haya fanani ata kidogo,mke wangu yeye alikuwa anataka arudi kwenye hali yake alafu mimi nilikuwa nataka aendelee kuwa na utamu uleule nilichofanya niliamua kumtuliza Martha baada ya kuona amepandisha hasira zake.
Palepale simu iliita ikabidi nipokee mbele ya mke wangu,
"biashara gani tunayofanyiana Oscar, nyumba imepatikana lakini umeondoka bira kunipa tarifa zozote zile", alikuwa ni dalali niliyemwacha ili nimuwahi mke wangu.
"nilipata tatizo dalali nakuja chap hapo sasa ivi tu"
Tuliamua kuondoka wote mimi na mke wangu huku tubeba begi letu la pesa tulilokuwa nalo.tulifika sehemu husika na kuiangalia nyumba na kila mtu alilithika nayo, niliona ni bora kuishi hapo kuliko kwenye maisha ya upangajini.
Mwanasheria alikuja siku hiyohiyo na tukafanya makabiziano ya hatimiliki na tukulipa pesa kama makubaliano yalivyo kuwa na sasa kilicho kuwa kimebaki ni sisi kununua vitu kwa ajili ya kuipendezesha nyumba yetu.
"Mume wangu mda umeenda sana ni vyema tutafute gest ya karibu tulale ili kesho tufaye kazi ya kununua furniture", Martha aliongea na mimi niliunga mkono wazo lake.
Siku iyo ikapita na siku nyingine ikafika kama tulivyo kuwa tumepanga mimi na mke wangu asubuhi ya siku hiyo tuliamkia kwenda kununua furniture na vitu vingine vya ndani ya nyumba sasa ilikuwa kwenye mwonekano wa kuvutia.
Huku mkononi tukiwa tumebakiza milion kama 40 na sehemu ivi.
Simu yangu iliita ikabidi niangalie kwenye kioo ni nani anayepiga na hakuwa mwingine bali alikuwa jamaa yangu Max ikabidi nipokee,
"Hello, niambie Max"
"Safi jamaa yangu emu njoo getoni kwangu hapa kuna tatizo kidogo", Max alikata simu bira kunipa nafasi ya mimi kumuuliza ni tatizo gani alilonalo nilimgeukia mke wangu na kumuaga,
"Martha sitachelewa kurudi "
"Oscar saa ivi ni saa 5 angalia usije kuchelewa na mimi nikakutwa na matatizo"
"Usijali mke wangu masaa mawili ni mengi mno na uzuri kwa Max nikaribu lazima nitawahi tu kurudi"
Nilikuwa na uhakika huo kuwa sitachelewa kurudi niliondoka pale nyumbani na kumwacha mke wangu akiwa na wasiwasi kidogo.
Nilifika mpaka kwa rafiki yangu Max aliyekuwa kasimama mlangoni akinisubiri mimi,
"Oyaaa Oscar ndugu yangu, kuna tatizo nimelipata hapa", Max aliongea.
"Tatizo gani ilo Max"
Max kwanza aliangaza huku na huku na kuniambia niingie ndani ile nafika tu nakuta kuna mdada amelala kitandani na hajitambui,
"Tatizo ndio hilo kaka, nimeshangaa kipindi nafanya nae mapenzi amezimia na nilijaribu mno kumuasha ila mpaka sasa ivi bado"
"Huu msala ndugu yangu",nilisogea na kusikiliza mapigo ya moyo ya yule mdada yalikuwa yanakisikika kwa mbali sana kumaanisha kuwa bado alikuwa mzima.
"Ndugu yangu huyu bado mzima hapa inatakiwa tumpeleke hospital akatibiwe tu".
Tulikubaliana nakuanza kuhangaika kutafuta usafiri na bahati nzuri tulifanyi kiwa na kumpeleka yule mdada hospital ambapo alipelekwa kwenye chumba maalumu baada ya sisi kumfikisha, huku rafiki yangu Max akiwa ni mwenye wasiwasi.
palepale mke wangu alipiga simu ikabidi nipokee,
"Upo wapi wewe huoni kama mda umekaribia bado nusu saa tu"
"Asante kwa kunikumbusha mke wangu nakuja sasa ivi tu", nilikata simu nakugeuka mahali alipokuwa amekaa Max ajabu nilishangaa kutokumwona.
"Huyu kaenda wapi au itakuwa kaenda kwa doctor huko!!" Nilijiuliza pasipo kuwa na majibu ila niliamua kwenda nyumbani na nilivyo anza kuondoka tu nilishanga naitwa na nesi,
"Wewe kaka njoo hapa"
"Mimi"
"Ndio wewe"
Nilimsogelea ili nisikilize kaniitia nini,
"Mwenzako ameondoka na amesema wewe ndio mwenye huyu mgonjwa mbona na wewe unataka kukimbia tena kama mwenzako"
"Heeeeeee",niliguna mana sikuamini maneno ya yule nesi kwanza alikuwa ana nipotezea mda na Max nae sikuelewa kwanini aliamua kunifanyia ule mchezo niliamua kujiongeza kama mwanaume ili nipate nafasi ya kutoka pale,
"Hapana nesi umefikilia vibaya hapa naenda kutoa pesa ili nije nilipie garama za matibabu, yule ni mke wangu siwezi kumuacha"
"Hapo sawa waweza kwenda",Nesi yule aliongea na iyo ikawa kama afadhali kwangu,
Nilivyoangalia simu yangu tayali nilikuwa nimeshatumia dekika 7 sasa zilibaki dekika 23 kufika saa 7:00 kamili safari ilianza yakutoka pale hospital ili nimuwahi mke wangu ila bahati mbaya ikawa kwangu tena siku iyo nikiwa naangalia bodaboda kwa ajili ya kuwahi nyumbani nilishangaa nimeshikwa bega langu kugeuka nyuma nakutana na mama mkwe wangu yani mama wa mke wangu Martha,
"Shikamoo mama"nilimsalimia mama mkwe wangu.
"Haujambo kijana wangu mbona kama una wasiwasi?",aliniuliza mama mkwe.
"Nasubiri usafiri wa kwenda nyumbani mama"
"Ooh basi ni vizuri ata mimi nina mda mrefu sijamuona binti yangu tunaweza kuongozana wote mpaka nyumbani kwako",Mama mkwe wangu aliongea.
Kijasho chembamba kilianza kunitoka kwa alichokisema ety tuongozane mpaka nyumbani niliangalia saa yangu sasa zilibaki dekika 14 tu kwa ninavyo kumbuka.
"Mwanangu mbona umezubaa kuna tatizo huko nyumbani"
"Heee unasemaa",nilijikuta nikisindwa kuongea vizuri mbele ya mama yake na Martha...ITAENDELEA..