MR GENERAL : KUMBE ULINIPENDA EEE SEHEMU YA 17
Nikasimama na kumsalimia kwa heshima, na mume wangu aliuona wasiwasi wangu, akaniangalia kisha akatabasamu na kusema, “Najua hamjawah kukutana na mke wangu kipenzi, Happiness hii ndio familia yangu, na wazaz wangu walipata bahati ya kuwa na watoto wawili tu wa kiume mimi Erick na mdogo wangu Fredrick , na huyu hapa mbele yako ndio Fredrick na hawa ndio wazaz wangu…
Tusamehe kama familia, maana ni aibu kusimulia mambo mengine ila nakupenda sana mke wangu, na familia yangu yote inajua, mpaka mzee wangu kuamua kuchukua jukum la kwenda kuposa na kuoa kwa niaba yangu haikuwah kuwa kazi rahisi, kabisa, nashindwa kukusimulia ilikuwaje mpaka baba yangu akakubali kuja kuoa kwa niaba yangu, ila elewa ni baada ya kuona mapenzi makubwa ambayo nilikuwa nayo juu yako, ni baada ya kuona kuwa nilikuwa nakupenda kuliko kitu chochote kile kwenye maisha yangu….
Nikatabasamu kwa heshima, maana ndio nimeletwa mara ya kwanza ukweni, sitakiwi kuwa na kidomo domo, kisha nikasema “Nafurah sana kuwafahamu…
Wote wakatabasamu na kuanza kupiga story nyingine, ambaz kwa akili zangu ndogo nikawa najua ni story za kifamilia tu, huenda hata mimi mwenye hata hazinihusu…
Basi imefika usiku mama yake akatuandalia chumba ila mdogo mtu akataka kuanza kupiga story na mimi, nikaona ni sawa tu, kwa sababu kwanza ni shemeji yangu, nikaona kama hana shida hata kidogo…
Basi bana mume wangu akawa ametoka na baba yake, sijui hata walikuwa wameenda wapi wakati huo..
“Hivi umempa nini mshkaji maana anaonekana kama amepagawa sana na wewe, hapa juzi kati alikuwa anafanya vituko, mpaka tukawa tunashangaa general mzima kweli anapagawa kiasi hichi, embu tuambie umempa libwata gani, ili na mimi nikitaka kuoa nije nimtume mke wangu kwako, aje kupata recepi ya mahaba…
Nikajikuta naanza kucheka maana alikuwa mcheshi sana, na kusema kwa sauti ya aibu
“Ni yeye mwenyewe tu, maana hakuna kitu chochote kile cha maana ambacho huwa nampa…
“Itabidi nikutafute unambie bana, haiwezekani, kwa sababu bro alikuwa mtu flan kauzu, yaan hanaga mbili kwenye moja, ila akaanza kulia hapa kama kuku bwege akisema
“Namtaka Happiness, namptaka Happiness mpaka familia nzima tukawa tunataka kujua huyo Happiness ni nani, ila tuache utani shemu wewe ni chombo, bro ana haki kabisa yakupagawa kabisa…
“ Acha utani wako bana, mimi sina cha ajabu, ila embu nambie alifanya nini?..
“Siku hIo ilikuwa kama saa kumi na moja, tunashangaa bro ameingia ndani, akaanza kuimba na kusema
“Am in love, mama am in love…
Mimi na mama tukashangaa huyu mwamba vipi, kwanza tunajuaga hanaga muda kabisa na mademu, sasa anakuja kutuimbia sisi maswala ya am in love, hata kama ni wewe utaacha kushangaa kweli, akaendelea kusema shemu wangu wa ukwee…
Basi mama akamuuliza “Huyo mwanamke ni nani na anaishi wapi, sasa kabla hajamjibu mzee akatoka na kusema “Wewe Erick umechanganyikiwa au, haujui kwamba kuna muda watu wanalala, embu tuambie huyo binti ni nani? Maana swala la kuoa wewe hatujawah kulisikia, na tulikuwa tunataman sana uwe na mke maana umri wako unaenda, ndio akasema kuwa kuna mwanamke ana mpenda ila hajui kama huyo mwanamke anampenda pia au laa…
ITAENDELEA ….
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi