UTANIITA SHEMEJI* SEHEMU YA 07
SONGA NAYO.................
Taratibu nilifuta machozi na kuinuka nikatoa vyombo na kuendelea na ratiba zingine, sasa wakati nikiwa bize na kazi Alvin akaja na kusimama pembeni yangu.
Sikutaka kumsemesha ndo kwanza nikawa bize na mambo yangu ,akaniangalia mwisho akasema ""umeona nilichokwambia lakini?""
Bila kumuangalia nikamwambia "unaongea kuhusu nini??"
"Acha kujifanya unaweza kupambana na mateso ,we sema neno moja tu nimekubali baasi yote nitayabeba mimi sawa mrembo wangu "" aliongea na kunishika bega jambo ambalo lilinikwaza kupita maelezo.
Bila uoga niliinua uso wangu nikamuangalia usoni kwa hasira sana na kushika mkono wake ulio begani kwangu nikautoa kwa nguvu na kusema .
"Alvin iwe mwanzo na mwisho kwako kunishika na kuongea upuuzi mbele yangu, na ndio nimekataa kuwa karibu na wewe kama ni mateso nipe ila kunishika sehemu yoyote ile ya mwili wangu ni kosa .
Na kama utaendelea kufanya huu ujinga utajua upande wangu wa pili ukoje mshenzi wewe "
Niliongea kwa hasira sana ajabu aliniangalia na kucheka sana kisha akasema "wow nimependa vitisho vyako,, ila unajua nini?? sikulazimishi kukubali sawa ,we fanya mambo yako kwa amani.
Ila kama utaona unanihitaji njoo nipo kwaajili yako,, kwa hiyo yote yanabaki juu yako "
Aliondoka nikabaki namuangalia kwa hasira sana, unajua mimi ni bora mtu anitukane au hata kuniweka kofi nitavumilia ila si kunifanyia uzalilishani kwa kuuchafua mwili wangu.
Hapo siwezi kukaa kimya, sasa naona huyu Alvin anataka vita na mimi na kwa mikono miwili hii vita nimeipokea shenzi zake 😒.
Basi bwana niliendelea na kazi zangu siku ikaisha ,kesho yake tena kama kawaida nikaamka na kupiga kazi ilipofika jioni nikaingia chumbani na kupumzika kidogo.
Baada ya kupumzika nikaingia bafuni na kuoga nilivyo maliza nikatoka na kuanza kuangalia nguo ya kuvaa ,mara mlango ukafunguliwa.
Nilishtuka nikizania ni Alvin hivyo nikainama kujificha maana nilikuwa uchi, ila baada ya mlango kufunguliwa akaingia Shuu na shoga ake .
Walivyoona nimeinama Shuu akasema " embu inua milonjo yako hapo, eti unajificha unakitu gani cha maana hadi ujifiche?😏 "
Bila kuongea neno niliinuka na kusimama kusikiliza wanataka nini ,nikashangaa hawaongei zaidi wako bize kuniangalia , nikaona mmmh embu nijifunike mie maana dunia ishaota miguu.
Nikavuta shuka na kujifunika ndo nikaona Shuu anaangalia pembeni kwa aibu ,rafiki yake akamshtua kwa kumwambia aniambie kilichomleta ili waondoke .
Bibie kuambiwa hivyo akajifanya anakohoa na kusema " wewe leo mama atakuja na mgeni so upike chakula kingi na sio mama tu hata mimi nina wageni wangu sasa kazana kukaa uchi uchelewe kupika"
Niliitikia sawa wakaondoka ,me nikaendelea kuangalia nguo .
Sasa baada ya wao kutoka chumbani kwangu walienda hadi sebleni wakakaa ,mara rafiki yake Shuu akasema " mmmh ila Wardah anashape nzuri balaa, yaani tumbo kama hajawahi kula ,kifua sasa ni saa tano kasoro maana sio kwa dodo lile .
Unajua nimejikuta naganda kumtazama moyoni nikasema kweli kuna watu waliumbwa halafu kuna sisi hapa tukinywa maji glass moja tu tumbo linakuwa kama tumemeza puto. "
Shuu alichukia na kumwambia " kwa hiyo unataka kusema nini kwa mfano?"
"Nataka kusema nini ukimaanisha nini dada??,, halafu mbona kama umechukia 😁 "
"🙄Aliekwambia nimechukia ni nani 😏, na kwanini nichukie ile hali jitu unaloliongelea ni bovu kama hoho iliyooza"
"Weeee shoga angu pale huingii, kwa Wardah aaah uko nyuma sana hivi umemuangalia vizuri lakini au unamuangalia kwa jicho la husda.
Dada binti wawatu kanyooka kama rula,, si sura si rangi si kifua wala shundu vyote hakuna unachomzidi na hivyo unavyo muona ndo hajajua kuoga .
Ee jiji bado halijampokea subiri ajue kujitunza uone ,yaani utakuwa unapitwa kama kigagula wala wakukuangalia hatakuwepo .""
"Eeeh basi maana naona unajimaliza 😏"
"Niukweli sio kujimaliza pale hufui dafu dada"
"We nae sinimesema basi au ndo unataka tukelane basi 😡"
"Aaah haya dada nimefunga mdomo🤐" wote walikaa kimya , huku kwangu nilimaliza kujipaka mafuta nikatupia kijora changu cha elfu sita huyo mdogo mdogo kuelekea jikoni.
Nikapita sebleni bila hata kuongea neno kwa sauti ya chini nikasikia rafiki yake Shuu anasema " ona hapo liko kwenye dera ila unaona mzigo unavyoenda "
Shuu alimkata jicho na kusema " Sasa hiyo nayo ni shape ya kukufanya umlinganishe na mimi? Huyo anatako sio shape"
"We unalo 😁 aaah tusiende mbali shape sio tako ndio ila we unalo?😆 na usijifariji we kubali tu humfikii"
"Umetumwa eeh 😡maana unaropoka ropoka tu kama umempenda nenda kaongee nae unitolee uchuro hapa😏"
"Hahahah😆 haya nimekaa kimya🤐 "
Shuu hakutaka kuendelea kukaa akainuka na kuchukua pochi yake kisha huyoo akaondoka, rafiki mtu nae akainuka na kumfuata.
Wakatoka nje na kusimamisha bajaji wakaanza safari yao , karibu njia nzima walikuwa kimya mwisho Shuu akavunja ukimya na kumwambia rafiki yake.
"Hivi rafiki yako bado ana mawasiliano na yule dada anaeuza dawa za kuongeza shape ?"
Rafiki mtu kusikia hivyo alimuangalia Shuu na kumuuliza " ndio bado wanaongea kwani unamtaka ??"
"Achaga kuuliza maswali ambayo unamajibu nayo, we nipe namba za huyo rafiki yako nijue nampataje yule dada basi "
"Subiri kwanza ,,Shuu unataka kuongeza shape udugu wangu!!?"
"Kwani kuna shida gani au ni mwili wako"
"Kheee makubwa 😆yaani nilijua umekuwa ila bado akili za kitoto hazijaisha,, yaani kisa Wardah ndo unataka uanze kunywa midawa eti unaongeza shape?"
"Alafu Esma naona leo unataka kunitibua , kwani sangap nimesema nafanya hivi kwasababu ya yule mpuuzi😡 ?"
"Hakuna Shuu nakujua vizuri ndugu yangu ,hapo roho yako inakuuma kuona mwenzio anasifiwa ,labda ni kushauri kidogo tu jikubali na ujipende kwa jinsi ulivyo.
Hayo mambo ya wivu yatakuja kuua bure na usifikiri utaja kunywa au kufanya kitu ikafanana na yule binti ,yeye mwenzio kaumbwa vile hata ukisema leo ukamtoe lile shape lake bado kwa sura tu hutamfikia.
Haya nambie utaenda kufanya hadi surgery ya uso ?? Embu acha ujinga bwana "
"Esma narudia tena sifanyi kitu kwasababu ya mtu na kama hutaki kunipa namba za huyo shoga ako mchawi uache "
"Eeeh ukome kumuita shoga angu mchawi,mchawi ni wewe na roho yako 😏"
"Kwa hiyo umegoma kunipa namba ?🤨"
"Unanilazimisha 🤨!!"
"Eeeh ukitaka uache namba tu unataka kujifanya kama naomba figo😏"
"Ndo nishaacha ,dereva niache hapo hapo"
"Sasa unaenda wapi 🤨?
"Achana na mimi" dereva alisimamisha Bajaji Esma akashuka na kuondoka huku nyuma bibie Shuu akabaki anaita tu Esma hakuitika wala hakugeuka.
Kwa hasira Shuu akamwambia dereva bajaji ageuze ,, dereva hakuwa na neno akageuza kufika nyumbani akamlipa hela yake na kushuka huku akiwa amerefusha mdomo kama chuchunge .
Kwa mwendo wa haraka haraka aliingia ndani ya geti na kubamiza mlango kwa nguvu ,kisha akazunguka upande wa gardeni na kwenda kukaa.
Kwa mbali akaniona nikiwa bize kuanua nguo, aliniangalia kwa macho yaliyojaa hasira kali haraka akainuka na kutaka kunifuata mara honi ya gari ikasikika nje.
Akaishia kusonya na kwenda lilipo geti akafika na kusimama pembeni ,mlinzi akafungua gari likaingia na kwenda kunako maegesho .
Bibie akalifuata kufika tu mama mtu akashuka wakakumbatiana na kusalimiana kwa furaha ,maana mama mtu alikuwa hayupo nyumbani kama siku mbili hivi.
Basi mimi baada ya kusikia honi niliingiza nguo nilizoanua ndani chapu kisha nikatoka kwenda kupokea mizigo, nafika tu nakuta mama na mtoto ndo wanamaliza kusalimiana.
Nikaona mlango wa gari unafunguliwa akashuka mwanaume ambae kwa haraka haraka alikuwa kati ya miaka 30 hadi 35, Shuu alivyo muona mwanaume yule alikimbia kwa furaha na kwenda kumkumbatia.
Ajabu mwanaume yule hakupokea kumbato la Shuu akawa bize kuniangalia ,jambo ambalo niliona limemkwaza mama mtu Shuu nae kuona hajapokelewa aligeuza uso wake na kuniangalia kwa hasira sana.
Mtoto wawatu nikainamisha kichwa chini😔.
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi