UTANIITA SHEMEJI* SEHEMU YA 09
SONGA NAYO..................
Haraka nilijilaza na kujifanya nimelala, aunt Vero ambae ndo alifungua mlango aliingia na kufika anasimama bila kuongea wala kufanya kitu akaniangaliaa karibu dakika tatu.
Kinyonge akashusha pumzi na kuondoka , baada ya kuondoka nikainuka na kukaa kitako , mawazo na maswali vilikuwa vingi kichwani mwangu na hakuna jawabu nililopata .
Mwisho nikajilaza na kuanza kuusaka usingizi, haikuchukua mda nikalala n kuja kuamka kesho yake alfajiri nikaingia jikoni na kuanza majukumu yangu ya siku.
Mda ulienda ikafika saa mbili Alvin akaja jikoni na kufika anasimama pembeni yangu, mimi kimya akawa ananiangalia mwisho akasema .
"Hatmae umeshinda mtihani wangu" alivyo sema hivyo nilimuangalia na jicho la upande kisha nikaendelea na kazi zangu, akatabasamu na kunambia .
"Bwanaee tusichukiane me nilikua naipima akili yako nione kama inakutosha , naona kweli inafanya kazi vizuri sana na kwa maana hiyo umefanikiwa kuwa rafiki yangu"
Bila kuinua uso nikamwambia " ingekuwa vyema kama ungechukua kilichokuleta ukaondoka maana unanitia uzito tu"😏
"Eeeh usijifanye matawi sasa, me kuja kukwambia nilikuwa nakupima kusifanye ukaniona boya sawa ?"
"Kwani unashida gani?"🧐
"Ukiniangalia naonekana nina shida? Msichana embu acha kiburi kwanza nina habari mbaya juu yako ,fanya unavyojua mwezi huu uwe wamwisho kuwa hapa.
Maana mipango inayopangwa juu yako si rafiki kwa kesho yako , sasa jitie kiburi upuuzie ukianza kunyooshwa tu hakikisha unalilia uvunguni."
Maneno yake yalinifanya nikamuangalia kwa mshangao na kumuuliza " una maanisha nini kusema hivyo?"
"Achana na kumaanisha nini we kaa ukijua sehemu hii si salama kwa kesho yako kwa hiyo anza kujikusanya taratibu kisha potea kama mchawi ."
Aliongea nikataka kumuuliza ila nikasita baada ya kusikia sauti ya Madam boss akisema " nyie ndo upuuzi gani mnafanya ?"
Wote tuligeuka na kumuangalia , Alvin bila uoga akasema "kumbe kuongea nako ni upuuzi ? "
Madam akamjibu " ushaanza madharau yako ya kijinga ,we huoni kama anafanya kazi huyo ?"
"Naona ndio ila inayofanya kazi ni mikono si mdomo ndo maana unaona anaongea huku akiendelea, kwanza achana na gubu naona uko na dada mpya?"
Madam alisonya na kumwambia " embu tupishe huko, na habari za kuingia jikoni kama mtoto wa kike ukome "
Alvin hakujibu kitu akaondoka na kutuacha wenyewe, madam baada ya kuona Alvin kaondoka akaingia nikamsalimia akaitikia na kunambia.
"Kama kuna kazi ambazo hujafanya muelekeze mwenzako afanye "
Niliitikia sawa huku nikimuangalia yule binti ,madam hakuongeza neno akageuka na kuondoka na kuniacha na binti yule.
Bila kuchelewa nikamuonesha baadhi ya kazi ambazo zilikuwa hazijafanywa kisha nikarudi kuendelea na chapati zangu, ilivyo fika saa tatu na nusu nikaanda meza.
Na kuwaita watu wote mimi kama ilivyo kawaida yangu nikarudi zangu jikoni na kuchukua kikombe cha chai kisha nikakaa chini tayar kunywa chai.
Ajabu nikiwa nimepiga pafu moja tu madam alikuja na kunambia kwanzia leo nitaanza kula nao mezani ,nilishangaa mbona ghafla au ndo kashaanza mipango yake?.🤔
Nikaona acha nianze kupangua mapigo mapema ,kwa upole nikasema " Asante madam ila nafurahi kupata chakula huku jikoni "
Nilivyo sema hivyo alikunja uso na kusema " sijaja hapa kukuomba hii ni amri ,haya amka haraka na hii iwe mwanzo na mwisho kukuona unakaa jikoni wakati wengine tukiwa mezani."
Sauti aliyoitoa hakuruhusu mimi kubaki nimekaa wala kuongeza neno ,haraka niliinuka na kutangulia mbele ,sasa yule binti mpya akataka na yeye kuja maana tulikuwa wote jikoni.
Ile anataka kuinuka tu akatulizwa " 👉we baki hapo "🥺masikini kinyonge akainamisha kichwa chini sisi hao tukaenda mezani.
Nafika tu Shuu akaachia sonyo na kusema " mmeshaanza kutia meza nuksi, sasa kulikuwa na haja gani ya kuileta hii simbilisi mezani ?"
Alvin kwa hasira akamjibu " alafu we👉 choko wewe nilishakuonya kudharau watu eti simbilisi hivi umejiangalia vizuri? Lione sura mbaya kama mtoa roho za watu."
Shuu alitaka kujibu ila akakatishwa na madam na kuwataka wakae kimya🤐 , basi nikavuta kiti na kukaa bila kuinua uso wala kupepesa macho yangu pembeni nikaanza kunywa chai.
Kimya kilitawala hadi tukamaliza kunywa chai,Shuu akawa wakanza kutaka kuinuka mara mama yake akamwambia " we Shuu utampeleka Wardah salon , uhakikishe anaoshwa nywele na kusukwa vizuri.
Akimaliza kusukwa utampeleka kwa yule kaka wa kucha nimeshampa maelezo yote "
Maneno ya madam yalimfanya Shuu akasimama kama amepigwa shoti na kwa sauti iliyojaa mshangao akamuuliza " umesemaje!!?"
"Kwani siku hizi unamatatizo ya masikio ? "
"Aaah kusikia nimesikia ila sijaelewa ,yaani hii taka taka ndo unataka niipeleke salon ili iweje na kwanini?"
"Shuu nadhani unanijua vizuri, sasa endelea kujitoa ufahamu na ninatoka nikirudi nimkute yuko hivi uone moto wake "
Shuu alichukia na kuondoka kwa hasira , madam nae akataka kuinuka Alvin akamuwahi kwakumuuliza " kwani mama mnataka kumpeleka wapi Wardah ?"
Madam bila kujibu aliinuka na kupiga hatua mbili Alvin akamuita " Mama " kwa hasira madam alisimama na kumgeukia Alvin na kumuuliza.
" Kwani Alvin unashida gani?"
"Shida yangu nataka kujua kuna nini mbona ghafla tu unataka kumjali mtoto wawatu "
"Kumbe unajua kuwa namjali sasa kujali nako ni tatizo ? Na kwanza mambo yangu hayakuhusu kwa hiyo funga domo lako na uishie kutazama "
Alvin alitabasamu akainuka na kusema " natumai hauna mpango wa kumpeleka kwenye uchafu wenu ?"
"Uchafu wetu!!? Okay tusema ndio nataka kumpeleka kwa hiyo utafanya nini au inakuhusu nini wewe?"
"Nilijua tu huwezi kukaa na amani kuona mtoto wa mwanamke mwenzio akiishi maisha mazuri.
Sikia mama kwa heshima yote ninaomba msimuingize mtoto wawatu kwenye maisha yenu ya kipuuzi , Shuu umemuharibu inatosha ila huyu muache kama alivyo "
"Umesema!!?"
"Umenisikia , Wardah hutaenda kokote unanielewa?"
Nilishindwa kuelewa niitikie ndio au nikae kimya maana sikuwalewa wanazozana kuhusu nini ,naona akili yangu bado ilikuwa gizani.😥
Basi madam baada ya Alvin kusema hivyo alicheka na kusema " naona umeonesha ni kiasi gani unanidharau ,labda nikukumbushe kitu kidogo tu Alvin , mimi ni mama yako na hapa ni nyumbani kwangu.
Kwa hiyo maamuzi au kitu chochote ninachotaka ni lazima kifanyike kama ninavyotaka unanielewa we mpumbavu "
"Huna haja ya kunikumbusha ila katika hili nahofia kusema kwamba niko mbali na wewe ,Wardah hataenda kokote na kama umeona hafai kufanya kazi za humu ndani mrudishe kwao ."
"Alvin narudia tena m......"
"Ndio wewe ni mama yangu ila umama wako kwangu hauna maana yoyote kiasi cha kunifanya nikae kimya huku ukitaka kuharibu maisha ya mtoto wawatu.
Na nikuulize we ni mwanamke uliezaa kwa uchungu au ulitutoa kwa kupiga chafya? Kwasababu kila ninapokuangalia naingia katika tafakari yenye maswali yasiyo na majibu.
Mama kwa umri wako unapaswa kumtumikia muumba wako na kuwa mfano bora kwetu ila hamna zaidi uko bize kuwapeleka watoto wawatu kuzimu .
Au mwenzetu unachembe chembe za ushetani labda ndo maana hushtuki? "
"Alvinnnn🗣"
"Haendi kokote😡"
"Ha ha ha ha ha ,Vero unamuona huyu chizi aaah unamuona 😠, eee Mungu nitaua mtu mimi wallah Alvin 👉 nakuita tena Alvin!! "
"Tuliza koo lako usije kupasua mishipa ya shingo maana imeshikilia laana hadi haina sehemu ya kupitisha damu "
Maneno ya Alvin yalimchefua madam akarusha mkono akitaka kumpiga kofi Alvin akaudaka kwa hasira na kumwambia " nakuheshimu kama mzazi laa ningeuvunja huu mkono kama kijiti cha kuzuia mimba , we Wardah inuka hapo"
Nikiwa nimejawa na hofu taratibu nikarudisha kiti huma ili niinuke mara madam akanambia " wewe👉ole wako uinuke hapo 😡"
Alvin nae akasema " Wardah nimesema inuka hapo 😡" eeeh hii sasa kali 😥sasa hapa nisikilize yupi niache yupi?😢
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi