UTANIITA SHEMEJI SEHEMU YA 20
Macho waliyo angaliana kipindi anaondoka yalinifanya nikabaki nasema moyoni ohooo it about to down ๐ฅฒ.
Samuel baada ya kuondoka Alvin alinifuata na kufika ananikwapua foil ilikuwa na nayama na kutupa pembeni , nilimuangalia kwa mshangao na kumuuliza .
"We vipi mbona umetupa nyama zangu ๐ง" kwa hasira akanijibu .
" Kwa hiyo kwasababu ya vijinyama hivi ndo vinafanya ushindwe kupokea simu yangu si ndio !?"
๐ง๐งaaaa jamani huyu anazungumzia simu gani? Na hata kama amepiga simu nikaacha kupokea ndo anitupie nyama zangu ?๐คจ
Kwamba nyama na simu vinahusiana nini kwa mfano ๐ง, ukweli sikupendezwa na jambo hilo hata kidogo๐.
"Sikia Alvin sijaona simu yako na hata kama ingekuwa ni kweli umepiga bado hauna mamlaka ya kuja na kufanya huu ujinga ulio ufanya "
"Ooooh ina maana hiki nilichofanya ni ujinga ila wewe kulishana na huyo muhuni sio ujinga si ndio "
" Kabla sijakujibu futa neno muhuni,Samuel si muhuni na yes nilikuwa nakula nae kwani kuna shida au siruhusiwi ?"
"Hilo lilipaswa kuwa jibu na si swali, Wardah umekuja hapa kufanya kazi nasio kupoteza mda wako na watu wasio jielewa .
Kumbuka nilikwambia nini na uliniahidi nini?"
"Excuse me! Ni lini nimeingia makubaliano na wewe kwamba sitakiwi kuongea na watu ?"
"Acha kupunguza ukali wa jambo ,sema mlikuwa mkilishana ๐"
"Ndio tulikuwa tukulisha so shida iko wapi ?"
"Oh kumbe huoni shida si ndio ? ,sikia Wardah mimi si rafiki tu kwako bali ni zaidi ya ndugu na mimi ndio mtu pekee kwenye maisha yako.
Kwa hiyo lolote ufanyalo ambalo ni kinyume na maadili lazima nikukanye , na toka siku ya kwanza nilikwambia jilinde na vijana wapuuzi kama huyu .
Ila no hukunielewa Zaid unazidi kupita kwenye kila njia niliyokwambia usipite, na nikuulize unaona ni sahihi kufanya huu ujinga sehemu yako ya kazi ?"
Nilishusha pumzi ndefu nikainuka na kusema" Alvin Nakuelewa na najua ndio wewe ndo mtu pekee nilie nae kwenye mji huu .
Lakini haina maana kuwa utasimama kama mwamuzi kwenye kila kitu nifanyacho na nikukumbushe mimi ni mtu mzima ,hivyo kila nifanyalo nafanya nikiwa na akili zangu timamu"
"Wow ,hahahahha unajua unani furahisha sana , hivi unajisikia lakini au unaropokwa tu ? Ila sawa haina shida so nambie hivyo ndivyo umeamua kucheza na maisha yako?"
"๐ฎโ๐จAlvin tafadhali embu achana na haya maana naona unatafuta kukwazana na mimi "
"Hapana Wardah sina mda wakutafuta kukwazana na wewe ila tu naomba nikukumbushe wewe ni yatima usie na support ya ndugu wala marafiki .
Hivyo njia pekee ya kukufanya uishi maisha mazuri ni kazi kwa maana hiyo unatakiwa utumie akili yako yote kuhakikisha unailinda kazi yako.
Kingine nilikwambia wanaume si ndugu zako , Wardah wanaume wako kwaajili ya kuharibu maisha yako wala si kingine.
Sasa jifanye ushaujua mji ,jifanye umeshapendeza na hilo shape lako likukuzue uyavagae nakwambiaje utalia machozi ya damu"
Aliongea na kuweka mfuko aliokuja nao mezani na kuondoka kwa hasira, nilimuita lakini hata kugeuka hakugeuka ndo kwaanza akapanda boda na kusepa.๐
Kichovu nilishusha pumzi na kuuchukua ule mfuko alioacha mezani nikataka kuuweka chini nikasita na hii ni baada ya kusikia vitu vikinukia ๐ฅฒ.
Bila kupoteza mda nilifungua na kukuta nimewekewa kuku choma mzima ๐, ukiachana na kuku kulikuwa na chips yai iliyoshiba haswaa ๐๐.
Niliachia tabasamu na kuchukua kifuko kingine ambacho hakikuonekana kuwa na chakula , nika fungua pale na kukuta ni mitandio mitatu pamoja na vipini vya kufingua ushungi.
Nilitabasamu lakini moyoni nilijisikia vibaya kwa kilichotokea ๐ช lakini sikutaka iwe hivi wala sioni kama kuna kosa nililofanya ๐ช๐ฅ.
Basi kinyonge nikiviweka vizuri na kutoka nje nikaokota zile nyama zilizotupwa na kuziweka kwenye dustbin kisha nikarudi kukaa .
Mda ulisogea kidogo nikaona nimtafute Alvin ili nijishushe maana nikisema najifanya kichwa ngumu kitanilamba maana ni kweli sina mtu mwingine zaidi yake๐.
Sijui alikuwa bado na hasira na mimi maana nilipiga simu hadi nikachoka ila hazikupokelewa , nikaona nimuache hasira zikitulia tutaongea .
Kweli bhna nikaacha na kutulia, mda ukaenda ikafika usiku nikafunga , sasa siku hiyo nyumbani tulibaki mimi na Daria tu hivyo nilivyofunga tu.
Tukaingia zetu ndani na kuanza kupiga story huku tukila kuku na chips alizokuja nazo Alvin ๐, sasa baada ya kula na kupiga story za hapa na pale Daria akaniuliza.
"Hivi Wardah nikuulize ikitokea Alvin na Samuel wote kwa wakati mmoja wakakutaka utafanyaje coz naona wote nikama wameshazama penzini"
'" Penzin? Embu acha pombe binti ,yaani unataka kusema kwamba Alvin ananipenda mimi !?"
"Sio Alvin tu na Samuel"
"Unawazimu wewe"
"Sio wazimu Wardah hawa watu wa nakupenda na ninaona dalili za kuzuka tatizo sasa kwa ushauri mdogo tu ni kwamba ndugu yangu wewe.
Angalia yule unaempenda ndo ubaki nae huyo usie mpenda vunja mazoea nae kabisa laa sivyo kutakuja kutimka kivumbi hapa hutaamini "
" Sikia bibie mimi hapa sina hisia na mtu yoyote kati yao, na sio mimi tu hata wao hakuna mwenye hisia na mimi so habari za nimuache yupi na nikae na yupi zipotee kabisaa "
"Haya me nakwambia unaona kama nakutania ila ndo hivyo ,maana huwezi kunambia ukaribu aliutengeza Samuel kwako eti niwa kirafiki tu.
Binti huyu mtu ni anakutengenezea mazingira tu ila ukweli anakupenda , na Alvin pia hivyo hivyo sasa endelea uje kupoteza wote"
Nilimuangalia nikaona huyu acha nimkalie kimya tu maana simuelewi hata kidogo๐.
Basi baada ya Daria kuona nimemkalia kimya alibadilisha mada na kuongea vitu vingine, mda ulienda ikafika saa ya kulala kila mmoja akaingia chumbani kwake.
Mimi kufika tu nikatoka kibalazani na kumkuta Samuel amekaa kama vile ananisubiri ,alivyo niona tu akasimama na kunipungia mkono huku akitabasamu ๐.
Ujinga tunaofanyaga tukiwa huku juu ni kupigiana simu na kuongea huku tukiangaliana ๐๐ eeeh maana hatuwezi kuongea moja akiwa kule na mwingine akiwa huku .
Lazima watu watajua na kusikia tunachoongea so tunachofanya ni nini ? Tunapigiana simu na kuongea , mda mwingine anawasha mziki kwenye kiredio kidogo sauti inakuwa si kubwa Sana alafu anacheza yaani ilikuwa ni full vibe ๐ฅฐ๐.
ITAENDELEAUTANIITA SHEMEJI
SEHEMU YA 21
Basi bwana tuliongea karibu masaa mawili ndio tukaagana na kila mmoja akaingia chumbani kwake, sasa mimi ile nimeingia naangalia simu nikakuta Alvin alinipigia wakati nikiwa naongea na Samuel. ๐ฅฒ
Si nikasema nimpigie ๐ฅฒkwani alipokea ๐? Huyu kijana naona leo nakisirani pro ๐ , haya kama hataki kupokea basi hasira zake zikiisha atanitafuta.
Haya mtoto wakike nikapanda kitandani ili nilale zangu mara nikakumbuka nina zawadi ambayo sikuifungua na niliambiwa niifungue nikiwa mwenyewe.
Chap kwa haraka nikaamka na kuchukua kibox kile , nikasogea kati kati ya kitanda na kuanza kufungua hapo karoho kanadunda kutaka kujua kilichomo ndani ๐ฅฒ mara buuum nikafungua ๐ฅฒ jamani nyie ๐ฅฐ๐.
Embu kaka kuna wakuotea aote ni kitu gani nimepewa ๐ฅฒ๐, nyie my wenu nimepewa simuuuu๐ tena sio kasimu ni simu ya viwango vya juuu ๐ฅฒ๐ฅฒ.
Moyo ulilipuka kwa furaha nikatamani kupaa lakini sikuwa na mabawa ๐ฅบ, nikatamani kupiga ukelele ila siwezi nitaamsha walio lala ๐ฅฒ.
Sasa nifanyaje ๐ฅฒ, niliwaza chap na kuamka nikachukua kiswaswadu na kumpigia nikamwambia please naomba utoke kibalazani , bila kuuliza kunanini akatoka .
Uliza kitu nilifanya ๐๐ฅฒ,? Mwenzenu baada ya kutoka tu nilituma mabusu ya hewani kama mia na uchafu๐ alafu nikawa kama namkumbatia ila ndo nakumbatia hewa ๐.
Na yeye alivyo jinga akawa anayapokea ๐คฃ๐ , nilifurahi na kumwambia asante sana , akajibu " anything for you mamaa"๐ฅฐ uwiiii jamani nafwaaaa๐ฅฐ๐.
Nyie niseme tu siku hii ilikuwa ni siku bora kuliko zote kwenye maisha yangu ๐, nililala usingizi mnono kuliko kawaida na kwa mara ya kwanza nikaingia kwenye ulimwengu wa smartphone tena kali kama mtoto wa mshua ๐ฅฒ๐
Aa Mungu please bless this man for me๐๐,maana anajua kunipa maraha bwana ๐ฅฒ๐.
Basi bwana siku hiyo ilipita kiivyo, kesho yake asubuhi nikamuonesha Daria simu yangu akaendelea kukazia kuwa kijana kashazama kwangu.
Kama kawaida nikapuuza na kuendelea na mishe zangu ,mchana Samuel akaja dukani na kunifungulia baadhi ya mafile pamoja na kunionesha vitu vyote muhimu.
Baada ya hapo nikabaki ni mwendo wa kuperuzi tu bando linatoka wapi ? Kwake mwenyewe ๐ eee sikujua hata bei ya bando likiisha tu naungwa juu kwa juu .
Maisha yakasonga ,ukaribu ukazidi Alvin nae akaachaga hasira zake pembeni akawa ana anakuja kuniona karibu kila siku sema alikuwa si mkaaji .
Sasa bwana baada ya wiki kadhaa kupita siku hiyo Alvin akampigia boss wangu na kumuomba of ya siku nzima , boss wangu hanaga baya akasema sawa.
Nikashangaa nafatwa kuuliza nikaambiwa kashapewa ruhusa kitambo, so nikajianda kisha haoo tukaokaondoka tulienda wapi beach โฑ๏ธ ๐.
Kufika huko tukaogelea na kuenjoy kwa sana , na ilipofika jioni akanambia tutalala pale nilishangaa na kumuuliza kwanini tulale pale ila hali tunaweza kurudi nyumbani.
Akanijibu eti anataka kukaa na mimi siku nzima , nikabaki okay๐คจ ila kichwani nilihisi kuna kitu sema nikaona acha nibaki tu maana toka nilivyo Anza kazi hakuna siku tuliyokaa pamoja hadi siku ikapinduka.
So atakuwa kanimiss actually hata mimi nimemmiss ๐ฅฒ ndio nikweli nimemiss ukaribu wake kwani ni vibaya ๐ฅฒau ndo nishaanza kufikiliwa vingine ๐ฅฒ.
Nisifikiliwe vibaya bhna ni kawaida sana so achane tuenjoy ๐.
Basi nilikubali akachukua chumba ,nikauliza tena kulikoni achukue chumba kimoja akajibu kwakuniuliza " nimesema nataka kutumia siku hii nikiwa na wewe je kuna shida tukishare chumba kimoja?
Au sasaivi huwezi kwa kuhisi labda naweza kukufanyia kitu kibaya?"
"No sina maana hiyo ila nimeuliza tu"
"Basi jibu ndo hilo na kama huko tayari kuwa huru kusema,siwezi kulazimisha so nikachukua viwili"
"Haina shida chukua tu " eeeh Mungu nilinde lolote lisitokee maana dah sijisikii poa kwa hili kwakweli ๐.
Niliwaza na kubaki nikiigiza kutabasamu, kweli bhna akalipia chumba kimoja ,baada ya kula tukaenda chumbani sasa madai tunaenda kupumzika .
Uliza kama kulikuwa na pumziko ๐ ๐ ila Alvin ๐ yaani tulifika chumbani nikiwa roho juu juu kwa hofu nikihisi huenda nitaenda kutafunwa.
Lakini haikuwa hivyo bhna ila sikulala elewa sikulala๐ฅฒ, yaani usiku kucha ilikuwa ni michezo, story kuangalia movie na mambo kibao and then buuum asubuhi hii hapa.
Watu ndo kukumbuka kwamba ohoo tulitakiwa tulale , ikabidi aongeze masaa tukalala weee saa nane ndo tukaamka ,tukapata chakula cha mchana .
Kisha tukajiandaa kuondoka , sasa baada ya kukweka kila kitu tayari kwa kuondoka Alvin akaniita na kunambia " Wardah naweza kumwambia kitu?"
Bila wasi wasi nikamwambia " yeah nambie"
Akasema" nimepata kazi "
"Weeeeee๐ mbona habari njema hizi na ulikaa nazo ๐ฅฒ, mh kabla ya hongera nambie ni kazi gani uliyo somea au"
"Yeah "
"Wow kweli Mungu ni mwema, hongera sana "
"Asante ,,aaam naweza kukuomba kitu ?"
"Yeah omba chochote"
"Utakubari?"
"Yeah kwanini nikatae "
"Okay , tunaweza kuondoka wote?"
"Kwenda wote wapi?"
"Mwanza ,huko ndiko niliko pangiwa kufanya kazi , so naomba twende wote "
Alivyo sema hivyo nilimuangalia na kubaki kimya , maana sikujua niongee nini yaani twende wote kiaje na vipi kuhusu kazi yangu?๐ค
Alvin baada ya kuona nimekaa kimya alinishika mikono yangu na kunisemesha kwa upole sana .
"Wardah tafadhali naomba useme ndio ,si tamani kuwa mambo na wewe hivyo tafadhali usiseme hapana"
"LA la lakini Alvin ni ngumu mimi kuwa na wewe huko ,maana ni......"
"Kama ni kazi nitakutafutia nyingine na kwasasa kazi yangu ni nzuri so nitahakikisha unapata kila unacho hitaji kwa wakati "
Nilikaa kimya huku nikiwa sielewi nimjibu nini , moyo ulisema nenda nae ila akili ilikataa huku mawazo kuhusu Norvin yakizunguka kichwani.
Alvin kuona nimezama kwenye dimbwi la mawazo akanambia " ni sawa unaweza kufilia then utanipa jibu ila usichukue mda mrefu "
Nilijibu ndio kwa kutikisa kichwa , akanishika mkono tukatoka na safari ya kurudi nyumbani ikaanza .
Sasa bwana wakati tunatembea kutoka eneo lile la beach tukakutana uso kwa uso na Shuu mdogo wake Alvin, kitendo cha kuniona nikiwa na ndugu yake kilimshtua sana.
Akataka kuongea ila Alvin akamkatisha na kunishika mkono vizuri kisha tukaenda kupanda bajaji tuliyo request na kumuacha Shuu akituangalia kama vile haamini anachokiona.
SEHEMU YA 22
SONGA NAYO....................
Basi bwana safari ya kurudi nyumbani iliendelea nikafika nyumbani , hakutaka kuingia ndani hivyo nilimuaga na kushuka mwenye bajaji akageuza wakasepa.
Mimi si ndo nigeuke ili niingie ndani ya geti nikashangaa kumuona Samuel akiwa juu ananiangalia , nikampungua mkono kwa mbali na kutaka kuingia ndani akanipa ishara nisiingie ndani.
Sikuwaza nikasimama kumsubiri ,ajabu alitoka nje na gari kunifikia akanambia ingia kwenye gari , nikauliza tunaenda wapi nikaambiwa ingia chap.
Eeh sawa nikaingia ,akaendesha na kwenda mbali na nyumbani kisha akasimama na kukaa kimya kwa mda kisha akaniuliza.
" Ulikuwa wapi jana ?" Uliza yake na namna uso wake ulivyo onesha hasira ilinifanya nijiulize kanichukia kwasababu yangu au kuna mtu kamkwaza.
Basi kwa upole nikamwambia " nilikuwa kwa shangazi "
"Shangazi yako ! Una uhakika ?"
"Yeah kwani vipi mbona kama hauko sawa ?"
"Yeah siko sawa, Wardah toka jana nakupigia simu yako lakini ulikuwa unaongea kana kwamba ulikuwa na mtu pembeni yako?"
Kwa hiyo kachukia kisa alipiga nikawa naongea kwa uoga au ana mambo yake ๐๐ค niliwaza na kumjibu .
"Hapana bhna utakuwa ulihisi vibaya ila mbona nilikuwa naongea kawaida tu "
"We unaona vile ni kawaida na why umerudishwa na huyo kaka ina maana ulikuwa nae pia? "
Nilitaka kujibu ndio nikasita na kusema " hapana nimeonana nae wakati narudi tu , mh kwanini umenileta huku au ndo ulitaka kuniuliza hivyo tu "
" Nimekuleta huku ili nikwambie kuwa na kupenda "
"Eeeh๐ณ!?"
" Ndio nakupenda na si kama rafiki bali kama mpenzi na mwanamke ninae tamania kuishi nae maisha yangu yote "
" Samuel! embu acha masiala na turudi nyumbani, nina kazi nyingi ujue "
"Sitanii Wardah , nakupenda na ninakuhitaji "
Nilikaa kimya na kuishia kumuangalia usoni, moyoni sikuamini kama kile ninachosikia ni kweli ama anaamua kunizingia ,kunipenda mimi Wardah kupendwa na Samuel hapana bhna.
Samuel kuona nimekaa kimya alifungua mkanda akanisogelea zaidi na kunambia huku akiniangalia usoni bila kupepesa macho wala kusita sita .
"I love you Wardah , nakupenda kuliko neno lenyewe so please naomba uwe wangu I promise nitakupenda na kukulinda maisha yangu yote I swear "
Huyu mtu atakuwa serious๐, " aaam Samuel naomba turudi nyumbani "
"Tunarudi ila nijibu kwanza "
"Samuel!"
"I love you "
"Lakini......" sikumaliza kuongea alinisogelea karibu zaidi tukawa zero distance, taratibu aliinua mikono yake na kuushika uso wangu na kwa sauti iliyojaa hisia kali akanambia.
"Lakini nini Wardah, sisi ni marafiki ! Je ni kosa marafiki kuwa wapenzi? No Wardah ni kawaida hisia za mapenzi kuzaliwa ndani ya urafiki wala hakuna ubaya wowote .
And unatakiwa kujua kuwa hisia za mapenzi hazina mipaka so please usinikatae kwa kigezo cha urafiki wetu kwanza hii ndo nzuri coz bond yetu si rahisi kuvunjwa ."
"Samuel ๐ฅบ!"
"Please be mine ,Wardah nilikupenda toka siku ya kwanza kukuona na hata sasa bado nakupenda so mamaa sema ndio , fungua moyo wako na uache nikupende"
Aisee nilivurugwa kuliko kawaida, moyo wangu ulibaki njia panda nisielewe nimkubali Samuel au Alvin na je nikimkubali Alvin itakuwaje maana siwezi kumkubali huyu alafu nikaishi na yule japo Alvin hajafunguka kunihitaji kimapenzi.
Ila nado haitaingia akilini nikimchagua Samuel alafu nikaishi na Alvin, au nimkatae niende na Alvin ila je moyo wangu unataka nini ?
Niliwaza sana ila sikupata jibu , Samuel hakukaa kimya ndo kwaanza alizidi kunichombeza kwa maneno matamu na ahadi kede kede.
Kitu kilichozidi kunifanya nizidi kuvurugwa , aaaa sasa nimpende yupi na yupi nimuache ๐ค๐ค
Kazi ipo sijui binti atachukua uamzi gani, au ngoja nikuulize mpendwa wangu we unafikili yupi anapaswa kubaki na Wardah je ni Alvin au Samuel
Na itakuwaje kama akimchagua Alvin mwanaume ambae amemsaidia na kumshika mkono kwa mda mrefu, je akiondoka nae huko mwanza je maisha yao yatakuwa sawa?
Na hadi mda huu Alvin hajafunguka kuhusu kumpenda ila tu kaomba kuondoka nae , lakini pia ikitokea mama yake Alvin akijua kuwa Wardah yuko na kijana wake tena wanaishi pamoja unafikili atakaa kimya.
Na vipi kama akiamua kubaki na A
Samuel je Samuel atampenda na kumthamini ? Ama na yeye ndo atakuwa wakupita ?
Yote hayo tutayafahamu katika msimu wa pili wa kisa hiki ,so mpendwa wangu usibaki nyuma twende wote sambamba tumalize kisa hiki pamoja love u byeeee
*MWISHO WA SEASON ONE*
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi

Maoni