UTANIITA SHEMEJI. SEHEMU YA 19
Mda ulienda na ratiba zangu zikisonga kama kawaida, jioni ikafika Samuel akatoka kazini ,naona leo mood yake ilikuwa vizuri maana alifika karibu yangu akasimama na kunisalimia .
Kisirani nilichokua nacho kwa siku hii hakikuniruhusu kuitikia salamu yake kabisa ,na sio salamu tu hata kuinua uso kumuangalia tu sikuthubutu.
Ndo kwaanza nilijiweka bize kubonyeza kiswaswadu changu π, akaniangalia kwa mda nikaona anapandisha kioo na kuondoka , huku nyuma nikamsindikiza na sonyo π
Yaani jitu jana lilinipita kama halinioni ,bado usiku likalala bila kuniona alafu leo bila mshipa wa aibu linanisalimia kama vile hakuna kilichotokea ππ.
Akwende huko π kwanza staki mazoea na yeye tena ,eeeh ataki kabisaa ,kama ni maisha kila mmoja aishi maisha yake nyambafu ππ.
Nilikuwa nimekaa nje ila kwa hasira niliinuka na kuingia ndani , mood ya kuchezea simu nayo iliondoka nikabaki naongea mwenyewe kama chiziπ.
Dakika kadhaa zilipita nikasikia geti dogo la nyumbani kwao linafungwa kakubamizwa nikahisi huyu anaweza kuwa yeye ,haraka nikajifanya nimelala.
Kweli sekunde chache mbele nasikia harufu ya manukato sijakaa sawa nikasikia anaita kwa upole " Wardah! " me kimya ,akaita tena " Wardah mama "
Bado nilikaa kimya , akaita tena sikuitika kwa sauti iliyojaa upole akasema " Wardah najua nimekukosea sana mamaa ila please naomba unisamehe "
Pamoja na kuongea kwa upole bado sikujibu akaongea tena mimi kimya , masikini kwa huzuni akaniuliza "Wardah umenichukia mamaπ₯"
Sikuwa na mpango wa kufungua macho ila ongea yake ilinigusa nikaona mbona kama namuonea kaka wawatuπ₯², taratibu nikafungua macho nakujifanya kama nataka kulia π₯²π₯Ί.
Nikaona mtu anaingia hadi nilipo na kuchuchumaa mbele yangu na kunambia " tafadhali mamaa niko chini ya miguu yako naomba unisamehe and I promise hata nikiwa na siku mbaya kiasi gani sitarudia kukuumiza tena.
But please usininunie hivi ,sitaweza kuishi ikiwa moyo wako una hasira juu yangu π₯²"
"Muongo na umekuwa na tabia mbaya sana Samuel kweli wewe niwa kunipita mimi au umenichoka"
"Noo Wardah usiseme hivyo ,me sio muongo wala sijakuchokaπ₯"
"Kumbe nini kulifanya unipite au ndo ushapata kisichana kinakuzuzua akili"
"Hapana mamaa hakuna mtu yeyeyote anaweza kufanya niacha kuongea na wewe,ila sikuwa sawa na nakili kuwa ni kosa nimefanya so unaweza kunisamehe tafadhali π₯Ί?"
"Mmmmmh nipe mda nifikilie π₯²"
"Acha zako bhna , alafu nimekuletea zawadi "
"Wewe sasa na zawadi zako π na hii tabia hakikisha unaenda nayo hadi uzeeni ,sio unanizoesha saizi alafu kesho unaacha wallah nitakuroga π"
"Umesema uzeeni ? Ina maana umeshaamua kuwa utakuwa na mimi maisha yako yote ?"
"Yeah kwani kuna shida gani au mwenzangu ushasain mkataba na Israel π€¨"
" kwanini nisain na nikisain nitakuachia naniπ"
"Utamuachia mume wangu π"
"Unahisi ni rahisi eeh ? Kwanza tuachane na hayo weekend hii tutaenda wapi maana nimemiss kula raha na wewe π"
"Mmmh kuhusu hilo tutaona siku ikifika ,sasaiv nipe zawadi zangu kwanza maana roho yangu ishakaa juu juu kama bundi anusae hatari"
Nilivyosema hivyo alicheka na kuinuka akatoka na kuchukua mfuko aliokuja nao , akanipatia mpenda zawadi nikapokea huku meno yote yakiwa nje π.
Kabla hata ya kusema asante nilianza kufungua ili nijue kuna niniiπ, bwanee mfuko wa kwanza kabisa ulikuwa na mbuzi choma π.
Nikatoa mwingine umejazwa chocolate kama zoote π huu wa mwisho ulikuwa na kibox ambacho kilifungwa kama zawadi special.
Nilikiangalia na kumuangalia akanambia " usifungue hapa , subiri ukishaenda kupumzika ndo utafungua "
"Kuna nini mbona kama unanitisha maana huchelewi kuweka bomu π£ "
"Usijali ukitaka kwenda kwa mtu mwingine ndo nitakuletea bomu ila kwasasa hapana utakula vitamu tu ππ"
"Mmmm!βΉοΈ huaminiki wewe, ila fresh nikilipuka utabaki unaishi maisha magumu kuliko ugumu wenyewe maana hakuna mtu kwenye hii dunia ambae anaweza kukaa na wewe kama mimi "
"Eti π embu kwenda huko ,kwanza achana na hilo box la mlipuko na ule nyama kabla hazijachuja utamuπ"
Sikujibu nikaweka pembeni na kuchukua mfuko wenye nyama nikafungua na kutaka kula akanishika mkono na kusema.
"Eeeeh binti huna haya wewe,yaani unakulaje bila kunawa"
"Wee bwana niache ,kunawa kwani naimeshika nini kichafu π"
"Hata kama bhna nawa huko "
"Sinawi sasa utanifanya nini π"
Alitabasamu na kuchukua maji akaninawisha kwa lazima π, basi baada ya kunawa nilianza kula ,aajabu akawa ananiangalia kwa huruma huku akimeza mate ππ₯²
Bila kuongea nilichukua kipande cha nyama na kufanya kama nampa akafungua mdomo aaaπ΅, nikasogeza karibu kabisa kisha nikatoa haraka na kula mwenyewe ππ.
Akajifanya kanunaπ π nikamwambia " sasa unataka kula chakula cha mtoto huoni aibu au ndo wale wakunywa uji wawagonjwaπ"
Kwa upole akasema " nionje kidogo tu π€π₯Ί"
"Staki π"
"Please π₯Ί"
"Eeeh basi nisije kukabwa bure" niliongea na kumlisha moja na mimi nikachukua nikala ,alivyo meza tu akafungua mdomo eti anataka tenaππ
Sinaga roho ya uchoyo ,nikawa nampa moja nakula moja , basi akawa anacheka mwenyewe kama chizi ππ.
Sasa tukaanza story akawa ananipa umbea wa huko kazini kwao , na mda huo tunaendelea kula mdogo mdogo mara ghafla bin viuu nikasikia "Wardah!!" Sauti ilikuwa ya Alvin na namna alivyo niita ilinishtua nikaunua uso kuangalia mbele nikakuta kasimama uso umefura kwa hasiraπ‘.
Moyoni nikasema"" wema nishautia maji nini"" Samuel bila kujali alinishika mkono na kujilisha nyama niliyokuwa nimeshika na kuinuka akasema.
"Nitarudi baadae " kisha huyooo akaondoka.
ITAENDELEA
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi

Maoni