Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  Afande sele ft Belle 9 dini tumeletewa

BILIONEA NDANI YA HOTEL SEHEM YA 08

31st Jul, 2025 Views 64

SEHEM YA 08

MWANDISHI ::HURU MEDIA


Baada ya vipimo kuisha Rahul akamuomba Vicky wakapate chakula pamoja , Vicky hakuwa na shida na hilo lakini swala la Rahul amtegemee kwenye matatizo yake hata halikumuingia akilini

Hakutaka kubishana na Rahul akamkubalia tu
Walitoka mpaka kwenye hotel moja Rahul ndio alimuaguzia chakula

"Vicky naomba muda kidogo nahitaji kuongea na wewe!!"

"Sawa nakusikiliza "
Rahul alikaa kimya kama anafikieria aanzie wapi , Vicky nae akamkazia macho hapo alishamwandalia majibu ya kumpa kama yote mana alijua wazi anataka kuizungumzia mimba yake

"Vicky, naomba tuongee kuhusu masha kuna vitu nataka kukuomba msaada"

Vicky akashusha pumzi akamuuliza vitu gani??
Rahul akajiweka sawa akainua maji akanywa wakati anaweka mezani akamtazama Vicky

"Unajua Vicky wewe upo cool sana kuliko dada yako, najua unaweza kuongea nae baadhi ya vitu, masha ni hana zile sifa za wasichana wa Africa nilizo kuwa nasikia kipindi chotee ,

Mr Alberto sio mtu wa hivyo kama anavyomchukulia yeye anaweza kumuendesha hivyoo ,asimchukulie udhaifu wake akajua ameshinda , Hapendi kufanya kazi ,Kusoma hataki,Anatumia pesa hovyo hovyo sanaa kiasi kwamba hata kama mtu unamiliki kisima cha pesa zinaweza kukauka ,
Embu jaribu kuongea nae Vicky wewe ni mtu makini sana nakuomba uongee na dada yako"

Mr Alberto na Mashaa??? Vicky alishtukaa

"Yaan huyo mchumba wa Masha ni Mr Alberto???"

"Ndio , kumbe hakuwaambia hili??"

"Mh,walikutana wapii??"
Swali hili lilikuwa gumu kwa Rahul , wakati Vicky anasubiri jibu , Yeye alikumbuka maneno ya Masha

Masha alimwambia "fanya ufanyavyo hii siri ibaki kati kati yetu sitaki aibu watu wajue mie nilibakwa au nimefanyishwa mapenzi kwa nguvu kama ukimwambia yeyote hata ndugu zangu naapa naenda kuwashtaki police "

Rahul akacheka kidogo akamwambia Vicky muulize dada yako mwenyewe mana yeye ndie anajua ukweli walivyokutana mie sikuwepo

Vicky akasema sawa namie siwezi kumchagulia maisha yeye akiamua kufanya kazi atafanya naomba unipeleke nyumbani!"

Rahul hakutaka kuendelea kubishana lakini la moyoni alitoa hampendi hata kidogo mashaa anatamani hata kurudisha siku nyuma tu ili kumsaidia kwa njia nyingine Boss wake

Akamrudisha Vicky nyumbani kwao , yeye akaondoka zake

Vicky anaingia tu chumbani akakutana na masha na alikuwa anamsubiri muda wotee

Alimvuta kwa nguvu akamtupia kitandani

"Ulikuwa unaongea nini na Rahul?? Ulikuwa unaongea niniiii!!? "

"Masha mbona hatujaongea kibayaa??"

"Hicho kizuri ndio nataka kusikia hayaa nambie ulionge nae nini??"

"Alinisaidia tu kule nilienda kumtafuta Moze nikaishia kugombana na Lydia basi hivyo tu"

"Mlienda wapi siku nzima na sahizi ndio unarudi ukanizimia simu"

"Kwani ulikuwa unanifatilia?? "
Masha akampiga bonge wa kibao hakupenda swali kama hiloo

"Na kwanini nikufatiliee" akamuongeza tena kibao kingine akaanza kumpiga anamwambia sitaki njaa zako usogeze kwa watu wangu wa karibu watu muhimu sitakiii sitakii mjinga kwanza toka kwetu tokaa "

Mama yake na masha akaja mbio baada ya kusikia kelele

"We masha ninii??"

"Simtaki humu ndani huyu simtaki"

"Kwani kwako humuu?? Si unakwako wewe?? Si umeamua kuwa na maisha yako huko umetukimbia humtaki hata mtoto wako tu sio wewe ,"
Mamaaa Vicky anamimba kaokota huko mtaani hamjui baba wa mtoto anataka kumpa mzigo Rahul mie sitaki mnataka tuonekane maomba omba ??"

Mama masha akashangaa , Siku zote anamjua Vicky ni mstaarabu anajua hana mahusiano yeye mwenyewe alisema mpaka atakapo maliza chuo

Akamgeukia akamwambia et ni kweli
Vicky akabaki kulia akasema ndio akamuuliza baba wa mtoto unamjuaa??

Vicky kabla hajajibu masha akasema amjue wapi analala na kila mwanaume mie siwezi toka hapaa

Duuh mama masha akabaki tu mdomo wazi
"Sina uwezo wa kukuhudumia wewe na mwanao Vicky sinaa" mama masha akajitetea

"Haina shida mama hata usijali mie bado kijana naweza kutafuta "

Masha akamfukuza huku anamwambia marufuku kabisa kumsogelea Rahul.marufukuuu
Akampokonya simu kukagua labda kuna namba ya Rahul na kweli alikuta namba ya Rahul
Masha alicheka kwa hasira yaan Rahul hajawahi kumpa namba yake yeye lakini amempa Vicky aliiblock halafu akaifuta kabisa ndio akampa simu yake Vicky ...

Vicky akakumbuka Rahul aliweka namba yake kwenye simu yake ili aipate namba yake akajipigia lakini hakukuwa na salio akamwambia naomba utanipigia niipate namba yako ukiwa na tatizo lolote nambie

Vicky akakubali lakini hakumtafuta ba hiyo namba ndio masha akaifuta haraka ...

Vicky alichukua nguo zake akampigia simu rafiki yake ambae wanasoma nae chuo akamuelezea kuwa amefukuzwa anapo ishi hana pa kwenda ,

Rafiki yake akamwambia haina shida njoo nyumbani kwetu,
Masha akajiapia moyoni hawezi kuruhusu huyo mtoto azaliwe mana atamuharibia kila kitu

Vicky akaenda moyoni anampango akimaliza tu chuo bado miezi michache atafute kibarua cha kufanya kuliko kurudi kijijini kwao tena na mimba atamvunja moyo baba yake

Hapo ndio maisha ya Vicky yaligeuka kuwa magumu sanaa mimba ilikuwa inamsumbua

ITAENDELEA....
KWETU morogoro.
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

BILIONEA NDANI YA HOTEL SEHEM YA 08  >>> https://gonga94.com/semajambo/bilionea-ndani-ya-hotel-sehem-ya-08
#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

Afande sele ft Belle 9 dini tumeletewa
SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+
Mambo ya wakubwa hayo soma kwa uangalifu 18+

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


majario rewards 100 Comments 0
 

MTOTO WA MAMA LISHE

majario rewards 100 Comments 0
 

MY LUNA SEHEMU YA : 06

majario rewards 100 Comments 0
 

NDOA YA MIE ... 8...

majario rewards 100 Comments 0
 

LUVIE binti wa malaya

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest