Chombezo....Oooh anko Mudy usichomoe.24 Dar es salaam SEHEMU YA ISHIRINI NA NNE ENDELEA. . . Muddy ali yashuhudia hayo mbele ya macho yake
“ Shiiiiiitttttt ujinga gani huu ”
mkurugenzi mkuu wa kampuni alipiga ngumi juu ya meza kwa jazba alizokuwa nazo alikuwa akihema juu juu chini hapa kukalika jasho lilianza kum tiririka gafla hasira zilifika ukomo wake ni dhahiri tangu kampuni ianzishwe hawakuwahi kuoata hasara kubwa kama hii
“ mpelekeni huyu mbwa hospitali akiamka lazima awe na maelezo ya kina ya kunipa ”
mkurugenzi alitoa oda kisha akafungua mlango kwa hasira na kutoka nje. . kikosi chote cha ulinzi kilicho husika kwenda kuchukua mzigo ule kili shukiliwa chini ya mikono ya polisi ali subiliwa bwana Mohamed azinduke ili atoe maelezo ya kina
baada ya nusu saa kupita bwana mohamed alikuwa amezinduka alijikuta juu ya kitanda chenye mashuka meupe kumaanisha alikuwa hospitali alipotupa macho upande wa kushoto alikutana na askari wapatao watano wakiwa wameketi juu ya sofa hapo ndipo alivuta kumbu kumbu vizuri
Daaa machozi yalianza kumtoka baada ya kukumbuka jinsi mashine ya kuhesabia fedha ilivyokuwa inatema mamilioni ya pesa alizokuja nazo kutoka benki kuu ya mkoa alijua wazi ana maswali ya kujibu mbele ya kizimba cha polisi lkn akifikilia kuwa hajui lolote kuhusiana na upotevu huo wa fedha alibaki kulia tu alijua wazi huo ndio mwisho wa maisha yake ya ulaiyani alijua yeye ni mtu wa kuozea jela tu
“ aaah bwana mohamed umezinduka habari yako bwana ” ili sikika sauti ya askari mmoja kati ya wale waliokaa aki msabahi . .haukupita muda uongozi wa hospitali ulifika kwa ajili ya kuangalia maendeleo ya mgonjwa wao
“ aaah sasa ndugu zangu nadhani mmeona kuwa mgonjwa na mtuhumiwa wenu amesha zinduka lkn bado ana onekana hayupo sawa kiafya hivyo niwaombe mtupatie walau siku mbili ili tuendelee kumchunguza afya yake ”
“ aaah sawa docta sisi hatuna shida hapo kikubwa ni kuongea na mkuu wa kituo inspecta Kibona ili yeye ndio awape ruhusa ”
basi baada ya mazungumzo mwishowe pande zote mbili wali kubaliana kuwa mgonjwa abaki kwanza hospitali akiwa chuni ya uangalizi wa madocta na polisi mpk pale atakapo kaa sawa
Zilipita siku mbili hatimae bwana mohamed alikuwa chini ya mikono ya polisi alifikishwa kwanza mahabusu kusubiri siku ya kupelekwa mahakamani kwa ajili ya kusomewa kesi
Siku ilipo wadia Familia nzima ya bwana muddy ikiongozwa na baba yake mzazi pamoja baadhi ya ndugu bila kusahau mke wake
bwana Muddy akiambatana na walinzi watatu walikuwa ndani ya kizimba cha mahakama wakisubiri kusomewa mashitaka yao . .
jaji alifika mbele ya mahakama na sasa wote walipaswa kunyanyuka kwa ajili ya kutoa heshima baada ya taratibu zote kufatwa kesi ilianza na shitaka lili somwa
“ Bwana Mohamed Kg unashtakiwa kwa tuhuma za ubadilishaji wa fedha halali kwa fedha bandia ulio ufanya mnamo siku ya juma nne tarehe 03 majira ya saa saba mchana ukiambatana na walinzi watatu wa kampuni ya kisongo security je una kubali shitaka hili..?”
“ hapana siku baliani nalo ”
baada ya kukana shitaka wakili wake nae alikazia kwa ajili ya kutoa utetezi kwa mteja wake lkn utetezi huo hauku saidia kitu kwani sahihi ilionekana ni ya bwana muddy akithibitisha kuwa pesa alizopokea zilikuwa ni za halali sasa iweje afikishe pesa bandia
pia uwepo wa cctv camera uli saidia kuonyesha mienendo ya pesa tangu ina sainiwa mpk ina ingizwa kwenye gari sasa swali je ni wapi pesa zili badilishwa na nani ali badilisha hapo hata muddy mwenyew alishindwa kuelewa
kwa asilimia kubwa kesi ile ilimbana bwana muddy kwa kila secta baada ya kesi kuunguruma takribani miezi sita hatimae siku ya hukumu ili wadia
“ Bwana Mohamed mzombe kwa mujibu wa kifungu cha sheria namba 34 ibara ya 15 katika kifungu cha pili na kwa idhini niliyopewa kisheria una hukumiwa kifungo cha miaka kumi na Tano jela pia mali zako zoote zita taifishwa kufidia hasara uli ingiza kampuni kesi imefungwa na haina rufaa ”
Ilikuwa ni siku ya majonzi kwa Familia ya bwana mohamed nguzo ya familia ilikuwa ime anguka hata wakilia haita saidia kitu bwana muddy alienda jela na huku nyuma mali zake zote zili taifishwa ikiwemo nyumba gari na shamba pesa iliyo patikana walipewa kampuni kama fidia ya hasara waliyo ipata. .
Miaka kumi na tano jela kumbuka hapo bwana mudi alikuwa na miaka therasini na mbili sasa uki jumlisha na miaka kumi na tano jela mpk akitoka atakuwa na miaka arobaini na saba ni karibu na utu uzima
itaendelea. . . .
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi