MFALME KIPOFU Sehemi..ya............14
Huyo hawezi kuishi bira wewe mana haoni na nafasi ya mwisho ni kuondoka katika huu ufalme nisione sura zenu tena hapa......
KUPATA MWENDELEZO ZAIDI WA SEHEMU INAYOFYATA BONYEZA LINK YA HAPO CHINI ππππ usisahau kunifollow ππ
https://www.facebook.com/profile.php?id=61550632115006
ENDELEA NAYO........
Mfalme Tengu aliwafukuza Prince Yao na Lindiwe katika ufalme wake hakuwapa ata mda wa kujiandaa na walinzi walipewa maagizo ya kuwa sindikiza na kuhakikisha wameondoka katika ufalme wa YUNDI.
Princess Nailet hakuamini kama baba yake anaweza kumfanyia maamuzi kama yale bira kumpa nafasi ya kumsikiliza,
"Nakuchukia sana baba!!!! nakuchukia!!"
"Sawa ata unichukie ila nafanya ivi kwa ajili yako huwezi kuwa karibu na kipofu na wewe ni binti wa kifalme"
Alikimbia huku akilia kuelekea chumban kwake.
"akikisheni mnakuwa naye karibu huyo asitoke kwenda popote"
"Ndio mfalme"
Yalikuwa ni maagizo ya mfalme juu ya kumuangalia Princess Nailet
Yunde alijiona mkosaji baada ya kusikia tarifa zile za Yao na Lindiwe kufukuzwa kwa wivu wake wakijinga.
"Nimefanya nini mimi Yunde,natengana na mwanaume niliyekuwa nampenda kwa ujinga wangu mwenyewe, alijutia nafsi yake"
***************
Katika kijiji cha Nyengweli kilicho ndani ya ufalme wa ADELI,
Binti Amma akiwa polini anatafuta dawa za matibabu kwa ajili ya wagonjwa alikutana na yule mzee aliyepiga magoti mbele yake ile siku aliyomtazama kwenye mkono wake.
Kwa mara nyingine tena mzee yule alipiga magoti mbele yake kama kutoa heshima kwake.
"Leo ni mara ya pili unapiga magoti mbele yangu kwani kitu gani kinachokufanya upige magoti?"
"Wewe ni mtu mkubwa sana kwenye hii falme ya ADELI lazima nikupe salamu yako kama inavyostahili"
"Hapana nahisi umechanganya mzee wangu mimi ni tabibu tu"
"Ni ngumu kuelewa ila mda mwafaka utafika na utaelewa"
Mzee yule alisimama na kuondoka zake na kumuachia Amma maswali mengi kwenye ubongo wake.
Amma baada ya kumaliza kuchimba dawa alirejea nyumbani kwao na kumkuta baba yake, alimweleza kila kitu kuhusu yule mzee juu ya kumpigia magoti kwa mara nyingine walipokutana huko polini.
"Unajua binti yangu mama yako aliwahi kusema ivi, ukiona mtu mkubwa anakuheshimu ujue kuna vitu vya maana vipo ndani yako".
"Umeongea kuhusu mama na umenikumbusha,ivi yupo wapi mama yangu???"
"Ni simulizi ndefu binti yangu"
Amma alisimuliwa kila kitu kuhusu mama yake na alihuzunika sana kusikia kwamba alishafariki zamani, pale yeye alipozaliwa .
***************
Asikari kutoka katika ufalme wa YUNDI baada ya kuwafikisha mpakani Prince Yao na Lindiwe waliwaacha wenyewe waendelee na safari yao na waliwakumbusha kuwa hawatakiwi kuonekana tena katika ufalme huo.
"Mama huku tunaenda wapi???"
"Usijali huku tunakoenda ndio nyumbani na sio huko tuliko toka"
"Unamaana gani kusema ivyo??".
"Utafahamu kila kitu tukisha fika Prince"
"Umeniita Prince?????"
"Kwasababu unafanana na prince"
"Mmmh",Prince Yao aliamua kuguna tu kwa majibu yale ya mama yake.
Lindiwe aliamua kupindisha baada ya kuona anaelekea kulopoka kila kitu kuhusu Prince Yao.
****************
Ndani ya ufalme wa ADELI mambo yalikuwa yameharibika kila kitu kilienda ndivyo sivyo mfalme Kojo alikuwa kwenye kipindi kigumu sana,
"Mfalme naomba ukae umesimama mda mrefu sana, Malikia andwaa aliongea kumtuliza Mfalme Kojo.
"Emu niache ni siku mbaya sana kwangu, General katoroka alafu nimemtambulisha mtoto ambae sijui ata limetokea wapi hilo litoto??".
"Ni sawa mfalme tutatafuta njia ya kumtafuta Prince wa kweli,hakukuwa na njia nyingine ya kufanya zaidi ya hii mfalme".
Walipokuwa wakiongea maongezi yale, kuna mtu alikuwa akiwasikiliza.
"Mnasema Prince mliyemtambulisha sio Prince wa kweli??? ilikuwa ni sauti ya Yanite"
"Tatizo jingine hilo"
"Baba mimi kuuliza nilichosikia imekuwa tatizo????,Princess Yanite aliongea.
"Ongea na mama yako akwambie kila kitu",Mfalme aliondoka kwa hasira chumbani na kuwaacha Malikia Andwaa na Yanite............ITAENDELEA
Lindiwe na Prince Yao wanaelekea wapi baada ya kufukuzwa na Mfalme Tengu?? na je?Malikia Andwaa atamweleza ukweli Princess Yanite kuhusu Prince Yao???,sehemu ya 15 inamajibu zaidi
Story.....................MFALME KIPOFU
Mtunzi...................Zooper
Sehemi..ya............15
Whatsapp.............0748697173
Ilipoishia sehemu iliyopita......
Baba mimi kuuliza nilichosikia imekuwa tatizo????,princess Yanite aliongea
"Ungea na mama ako akwambie kila kitu"
Mfalme aliondoka kwa hasira chumbani mle na kuwaacha malikia andwaa na Yanite.....
ENDELEA NAYO....
Hakukuwa na siri tena Yanite alisikia maneno yote waliyokuwa wakizungumza.
Malikia Andwaa aliona ni wakati sahihi wa kuweka kila kitu wazi mbele ya Princess Yanite hakuona haja ya kuendelea kumficha tena.
"Maongezi uliyoyasikia niya kweli yule sio Prince halisi tuliye mtambisha".
"Mama una chosema ni cha kweli?"
"Ndio mwanangu"
"Na Prince wa kwel yupo wapi???"
"Prince wa kweli anaitwa Yao na ni kipofu, alizaliwa akiwa na tatizo la macho tuliamua mimi na mfalme akalelewe mbali kisiri,na wenye hii siri ni mimi na mflame tu".
Malikia andwaa alimkalisha Yanite chini na kuanza kumpa historia nzima jinsi ilivyokuwa mpaka Prince Yao wakaamua kuchukua mamuzi ya kumuondoa.
Yanite alihuzunika kusika story ya kaka yake.
"Ni makosa yenu haikutakiwa kumtenga Prince na sizani kama atarudi hapa ila mimi nitaenda kumtafuta mwenyewe kaka angu".
Alinyenyuka na kuondoka, jumba la kiflame sasa amani ilikosekana ilikuwa siku mbaya kwa Mfalme Kojo na Malikia andwaa baada ya siri nyingine kugundulika.
******************
Cheki yeye alikuwa anazunguka tu katika jumba la kifalme kutazama uzuri wa jengo lile na kupishana na wafanya kazi mbalimbali wa kike na wakiume.
"huku kuna wanawake wazuri kuliko ata Yunde niliyemuacha YUNDI huku sitoki na acha aolewe na yule kipofu,alisema na nafasi mwenyewe".
Walinzi waliokuwa kwenye ile mipango ya kumtafuta Prince feki walimuona nakuanza kumteta bira yeye kujua.
"Huyu jamaa anabahati sana kupata nafasi ya kuwa prince"
"Ongea taratibu kumbuka hii ni siri tunajua sisi tu"
"ata kama ni siri lakini jama kapata bahati sana natamani iyo na nafasi ya Prince feki angenipa mimi mfalme"
Kipindi wanaongea rafiki yake na Nzegi alikuwa anasikia kila kitu na hapo alitambua siri nyingine katika jumba hilo la kifalme.
Aliondoka taratibu bira kusikika na kwenda msituni kuwatafuta General na Nzegi ili awape tarifa zile.
Haikumchukua mda mrefu mlinzi yule kuweza kufika msituni kwa ajili ya kutoa tatifa ile aliyoisikia kuhusu Prince aliyetambulishwa.
Wakiwa mafichoni general na nzegi walisikia mluzi ukipigwa na ilikuwa ni ishara Nzegi anayoitambua walisogea maeneo husika ya sauti ile ilipokuwa inatoka.
"Kuna tarifa mpya na nzuri kutoka katika jumba la kifalme"
"Tarifa gani izo?"
"Inasemekana Prince yule aliyetambulishwa sio Mwana wa Mfalme wa kweli".
"unasema kweli????,Nzegi aliuliza wakati huo General yupo kimya tu akisikiliza mazungumzo yao"
"Ndio na uhakika na ninacho ongea".
"Wewe rudi katika jumba la kifalme na umshawishi huyo kijana kuja nae hapa,tumeshapata mtu wa kusaidizana nae tayali"
"Sawa General"
Asikari yule aliondoka na kuwaacha General na Nzegi.
"Mda wa kukaa sasa umeisha leo usiku waziri mkuu tunaanza nae hana ulinzi wa kutosha lazima afe usiku wa leo,
General sasa alipanga kuingia vitani lasimi na Waziri mkuu ndie atakaye anza nae"
.
*********************
Tangu Prince Yao na Lindiwe waondoke Princess Nailet aliamua ajifungie chumbani kwake na Mfalme alianza kupata mashaka baada ya ukimya wa binti yake.
"Fungua mlango Princess"
Baada ya kuona hakuna mwitikio wa mlango kufunguliwa Mfalme Tengu alitoa amri,
"Vunjeni mlango haraka".Mfalme aliongea akiwa na wasiwasi mkubwa juu ya usalama wa binti yake.
Walinzi walifanyikiwa kuvunja mlango na mfalme kuingia ndani akiongozana na walinzi wake,
ilikuw ni kama bahati tu walimkuta anataka kujinyonga hapo ndipo mfalme alijua kuwa binti yake amezamilia kweli.
"Kwanini unanifanyia ivi binti yangu??"
"Nimechagua kufa kuliko kuona Yao anaenda mbali na maisha yangu".
"Unajua kabisa wewe ndie mtu peke uliyebaki kwenye familia yangu unataka huu ufalme ubaki mikononi mwa nani???"
"Mimi ilo sijali, baba naomba uniambie una mrudisha Yao au humrudishi??"
Lilikuwa ni swali gumu sana kwa mfalme tengu na ukizingatia ndie mtoto pekee alienae,
"Asikari",mfalme tengu aliita kwa hasira
"Nendeni mka warudishe haraka"
"Mfalme tayali wameshavuka mpaka"
"Nimesema nendeni mkawarudishe",Mfalme aliongea kwa hasira na mboni za macho yake zilibadilika na kuwa nyekundu hali iliyo waogopesha walinzi wake.
Hawakuta kupoteza mda tena waliondoka na kumuacha mfalme akiendelea .............ITAENDELEA.
Asikari wa Mfalme Tengu watafanyikiwa kuwapata Prince Yao pamoja na Lindiwe??,na Je?Yanite atachukua uamzi gani juu ya tarifa alizopewa na Malikia andwaa kuhusu kaka yake???,tukutane sehemu inayofata.
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi