VYOTE NDANI GONGA94
Story.....................MFALME KIPOFU Sehemi..ya............10
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
Ilipoishia sehemu iliyopita........
Maongezi yote yaliyokuwa yanaendelea pale Lindiwe alikuwa akisikia kila kitu..
"Hii haiwezekani yani mfalme ameamua aje amtafute Prince mwingine, hapana hii haiwezekani.....
ENDELEA NAYO.......
Hapana hii haiwezekani,Lindiwe alijikuta akiongea kwa nguvu na kuwafanya asikari wa ADELI pamoja na kijana Cheki wasogee eneo ilipotokea sauti ile na kuangalia ni nani huyo aliyeongea.
"Jamani emu tufanye mambo yaliyotuleta hapa ayo mengine hayatuhusu sisi, asikari mmoja aliongea"
"Wewe huoni kama huyu mtu alikuwa anasikiliza mazungumzo yetu????"
"Huo ni wasiwasi wako tu kama mtu mwenyewe ameshapatikana tuondoke nae tusipoteze mda".
Walikubaliana na wakaamua kuondoka maeneo yale na iyo ikawa ni ahueni kwa Lindiwe aliyerudi kwenye makazi yake kwa kasi sana kama mwizi anayekimbizwa.
"Mama mbona unahema ivyo tatizo nini???".
"Hamna tatizo lolote ila kuna sehemu tutaenda siku sio nyingi"
"Wapi tena huko???"
"Utafahamu tu mwanangu usiwe na haraka".
Lindiwe kuna kitu alichokifikilia nakuona ni sahihi kuja kukifanya kwa badae.
*******************
Katika jumba la kifalme Princess Yanite akiwa amekaa na mdogo wake Princess Yanni,
"Ivi dada kwel kaka atakuja tucheze nae wote???"
"Sahau kabisa kama una kaka,Yanite alimjibu mdogo wake".
"Ujinga gani huu unaondelea hapa,Malikia Andwaa aliingia baada ya kusikia mazungumzo ya mabinti zake"
"Mama huyu Yanite anasema nisahau kama nina kaka"
"Una matatizo gani wewe Princess Yanite na ndie mkubwa unaetakiwa uwe mfano kwa mwenzako????".
"Nini nifanye ikiwa mnatuficha sisi watoto wenu tusijue kinachoendelea"
"Nimekuambia kuwa na subra utajua kila kitu badae".
"Kwani kufahamu ndugu yetu yupo wapi limekuwa ni kosa nalo????".
Princess Yanite alinyenyuka kwa hasira na kuondoka, kitendo kilichomfanya Malikia Andwaa ashangae mana hajawahi kumuona binti yake akiwa kwenye hasira izo tangu alipo mzaa.
Upande mwingine Malikia Andwaa aliona wao wazazi ndio wenye makosa kwa kushindwa kuwaelezea ukweli mabinti zao kuhusu ndugu yao.
******************
Baada ya sherehe kumalizika ndani ya jumba la kifalme Princess Nailet hakuacha kumuwaza Prince Yao, sura ya kijana yule ilikuwa haifutiki katika ubongo wake,
Alimfata mtumishi wake aliyemuahidi atampeleka sehemu anayokaa Prince Yao.
"Lakini Princess ndio kwanza sherehe imeisha huoni kama mfalme Tengu atakuwa na hasira akisikia umetoka????"
"Naona tumeanza kupangiana sasa umesahau kati yangu mimi na wewe nani mkubwa???".
"Hapana princess"
"Aya ongoza njia".
Licha ya kigiza kuanza kuingia siku iyo Princess Nailet hakujali zaidi ya kutaka kufika nyumbani kwa Prince Yao safari ilianza akiwa na msaidizi wake mpaka nyumbani kwa Prince Yao.
Lindiwe akiwa ameka na Prince Yao alishangaa kusikia mtu akibisha hodii,alinyenyuka na kwenda kufungua mlango.
"Heeeeeeh Princess ni.... wewe???, aliinama ili atoe heshima kwa Princess lakini Nailet alimuwahi na kumshika.
"Hapana inatosha haina haja ya kutoa heshima kwangu".
"Ka...ribuni, Lindiwe aliwakalibisha kwa tabu Princess Nailet na msaidizi wake mpaka ndani".
Katika jumba la kifalme baada ya mfalme Tengu kugundua binti yake hayupo alipata mashaka na kujua, huenda atakuwa katika mikono isiyo salama sababu haikuwa kawaida kuondoka bira kuaga aliagiza vijana wake wamtafute haraka na upesi...........ITAENDELEA.
Tsh 1000 unapata mwendelezo mpaka mwisho wa simulizi hii tamu lipia sasa kupitia namba 0613083801 HALOPESA Jina john Bugumba kisha njoo WhatsApp kwa namba 0748697173 upate simulizi yako mpaka mwisho
Mfalme Tengu atafanya maamuzi gani akigundua kuwa binti yake Nailet yupo katika nyumba ya Lindiwe????sehemu inayofata inamajibu zaidi
Umesoma kwa utulivu · dakika chache tu Asante Endelea kusoma chagua hapo chini
Umependezwa ?? Asante Soma Zaidi story-mfalme-kipofu-sehemi-ya
Story.....................MFALME KIPOFU Sehemi..ya............08 Ilipoishia sehemu iliyopita........ "Tarifa gani???" "Inasemekana baada ya siku tatu Prince
Story.....................MFALME KIPOFU Sehemi..ya............04 Ilipoishia sehemu iliyopita........ Farasi ilifika Lindiwe pamoja na prince Yao walipanda na safari ikaanza kutoka katika jengo