Alikimbia kwa bashasha kisha akanikmumbatia kwa nguvu nikiwa na mimba yangu, nilishangaa imekuwaje, kwa sababu kwanza sikuwa na mazoea nae ki hivyo kuanzia amekuwa kijana mkubwa, kingine kwa anavyoonekana ni kama alikuwa ananitafuta....
mbona umekuja huku Solomon ? ikabidi nimuulize...
Nimekutafuta sana mamaa, nimekutafuta sana, sikuwa najua kama una mimba, nakuahidi nisingekuacha hata sekunde moja uteseke, ningehakikisha napambana sana na unakuwa na furaha, kwa sababu nilishaapa kwenye maisha yangu yote nitahakikisha napambana kukufanya unakuwa mwanamke mwenye bahati zaidi dunian na unakuwa ni mwanamke mwenye furaha sana....
Nilijikuta namshangaa maana sikuwa namuelewa, ikabidi Yule mama amenipokea aje, akauliza " wewe ni nani?.. ambae
"samahan sana mama, nimemtafuta sana mke wangu, mimi ni mume wake, akajibu Solomon kwa sauti ya kujiamin mpaka nikashangaa, yaan anasemaje kuwa mimi ni mke wake, na hali ya kuwa hata hatukuwah kuwa na mahusiano yoyote yale kati yangu mimi nay eye....
Yule mama akaniangalia, nikakaa kimya, solomon akawa anasisitiza tuondoke ila sikutaka, Yule mama nae hakutaka, akanifata na kuniuliza kuwa nina m,jua, nikamjibu ndio namjua na tunaishi mtaa mmoja, ila sio mume wangu kama anavyosema...
Solomon akawa amekaa kwenye ule mgahawa ananisubiri niamue, ila ni kama alishapanga kuwa hawez kuondoka eneo lile bila mimi... Muda ulienda mpaka wateja nao wakaisha kabisa kwenye lile eneo, na baada ya wateja kuisha Solomon akawa bado amekaa ananisubiri.... tunataka kufunga hapa naomba uondoke kwa sababu siwez kwenda sehemu yoyote ile na
wewe...
Niokashangaa Solomon anaanza kucheka kisha akasema nina uhakika haujui unachokiongea na haujui pia unaongea na nani? Yaan kwa taarifa yako ni kwamba siwez kutoa mguu wangu hapa bila wewe, yaan kama hautaondoka kwa hiari basi utaondoka kwa lazima...
hakuna kitu ambacho unaweza kunifanya, nikasema kwa kujiamin kisha nikaanza kuondoka, nikashangaa nimebebwa, sio taksi bega ila amenibeba kama tunavyobebaga watoto wa changa, nikawa nataka kuleta vurugu ila kwanza na hali yangu hata sikuweza kabisa kufanya kitu chochote kile, Yule mama akawa anapiga kelele za msaada ila Solomon alikuwa na gari, akanipandisha kwenye gari kisha hao tukaanza safari hapo hata sijui alikuwa ananipeleka wapi...
Tukaenda mpaka kwao, akanishika mkono na kuniingiza ndani, mama yake na baba yake walipotuona ni kama walishangaa, nikasalimia ila mama yake hata hakuitikia, ila baba aliitikia salamu na Solomon hata hakusalimia akaanza kusema mama nilikuambia, kama ni kuoa nitamuoa alice mtake mistake, mimi ndio najua nataka kuishi na nani na nani sitaki kuishi nae na hakuna mtu hata mmoja wa kunipangia wala kunizuia...
Sasa Solomon alikuwa na mdogo wake wa kike, alikuwa ni mdogo ndio alikuwa kidato channe, akaanza nay eye kuleta mdomo, akaanza kusema " kaka unaoa Malaya, sikutegemea.. Nikaona aaa weee usinitanie, hawa wazaz wake nitawaheshimu, alafu kanakuja katoto ambacho nakamudu alafu niseme namuachia mungu, weee ulisikia wapi, nikajikuta naropoka na kusema nashkuru sana umejua kazi yangu, maana nina uhakika tulikuwa tunadanga wote...
ITAENDELEA....
Hakuna ratiba iliyopangwa kwa sasa.
Maoni