ONE NIGHT ONE MISTAKE❤ chapter 4 Siku zilienda na kazi ziliendelea kama kawaida Salsa alijua Romex kaamua kupotezea nae hakuona haja ya kujielezea
Siku moja Salsa alitakiwa kupeleka ripoti ofisini kwa Romex. Alifika mlango wa ofisi ya Romex alisimama kwanza na kujiweka vizuri, alitaka kugonga akaacha na kusimama kama vile mtu aliekuwa anajishauri.
Kumbe Romex alikuwa akimuangalia kupitia kwenye kioo cha mlango lakini mtu wa nje hakuweza kuona ndani.
"Huyu msichana sijui ana shida gani na mimi.
Alisema Romex kisha akanyanyuka na kwenda kufungua mlango, Salsa alishituka.
"Vipi madam Salsa mbona umesimama hapa?
"Aaa.. nilikuwa nakuja ofisini kwako.
"Karibu. Romex alisogea pembeni akampisha njia Salsa akaingia na Romex akarudisha mlango.
Wakiongozana mpaka mezani.
Karibu ukae. Romex alimkaribisha huku yeye akienda kukaa kwenye kiti chake
"Samahani nimeleta faili.
Romex alimuandalia usoni, alihisi kuna uwoga
ndani yake.
"Salsa tafadhali kaa tuongee.
Salsa alikaa taratibu kwenye kiti na kumsikiliza.
"Inaonekana una hofu sana mbele yangu nataka tuweke mambo sawa, kilichotokea siku ile uliponimwagia rangi ni kitu cha kawaida ni kama ajali tu, yale yameshapita alafu mimi kuwa boss sio usiogope kiasi hicho.
Salsa alitambua kwa yake maongezi ya Romex
hakuwa ametambua chochote.
"Sawa nimekuelewa boss.
Vizuri sasa unaweza kwenda kuendelea na majukumu yako.
Salsa alinyanyuka tayari kwa kuondoka lakini
alipopiga jicho mezani aliona ile hereni yake. Alishituka na kuitolea macho. Romex aliishika na
wote wanaangaliana usoni.
"Mbona uneiangaoia sana hii?
Mmmm.... Hapana... Ni.. ni nzuri alafu
Inaonekana ya bei ghari.
Romex aliangalia kisha akasema
"Sio bei ghali sana, ni bei ya kawaida tu.
Salsa alitoa tabasamu la kulazimisha kisha akasema.
Kwa mtu kama mimi ni kitu cha gharama.
Alijibu salsa kisha akaondoka. Romex alichukua ile hereni na kuiweka kwenye bahasha ndogo kisha akaweka kwenye droo ya meza yake.
Wiki kadhaa zilikataa tangia Salsa tangia Salsa ahamie kwenye kwenye kampuni kubwa, maisha yakizidi kwenda lakini kuna kitu kilikuwa tofauti kwa upande wa Salsa alianza kuhisi tofauti kwenye mwili wake, alikuwa anachoka sana, kuna baadhi ya harufu za pafyumu alikuwa hataki kuzisikia.
Siku moja alikuwa amekaa nje anaota jua huku akilia kipande cha ndimu. Msichana mmoja anaitwa Nzela alimfuata na kukaa pembeni yake
akawa anamuangalia.
"Vipi mbona unaniangalia hivyo?
Na kushangaa siku hizi sijui upoje? Hivi upo sawa kweli?
Mimi nipo sawa labda macho yako ndio yanakudanganya.
"Mmmh.... Hivi ni sawa kula ndimu? "Mbona ni kitu cha kawaida sana kwanza tangia
hapo zamani nilikuwa napenda kula vitu vichache.
"Vipi midomo kukauka? "Hata yenyewe ni kawaida.
"Vipi kulala lala hovyo?
"Ni usingizi wa kawaida.
Majibu ya Salsa yalimkuta Nzela hakuona haja ya kuendelea kuuliza maswali alinyanyuka akaondoka.
Siku zilizidi kusonga mbele hali ilizidi kuwa mbaya kwa Salsa, alianza kutapika hasa nyakati
za asubuhi na usingizi ulikuwa mzito sana. Siku moja akiwa unafanya kazi ofisini kwake aliposema apumzike kidogo kwa kuegemea kitu alijikuta anapitiwa na usingizi mzito sana. Romex alifika ofisini kwake lakini hakuwa na
habari aliendelea kuichapa usingizi kama yupo kitandani.
Huyu ana tatizo gani hii ni mara ya pili sasa namkuta amelala kazini.
Romex alisogea karibu yake na kumshika begani huku akimuita.
"Salsa, Salsa...
Salsa alilisukuma mkono wa Romex na
kuendelea kulala. "Hey wewe unalala nini? Romex aliongea kwa
sauti ya ukali na kumfanya Salsa ashituke. Alipomuona Romex alikurupuka na kutaka
kukimbila, Romex alimshika mkono na kumrudisha kwenye kiti.
"Unaenda wapi?
anaenda wapi. Naenda........ Salsa hakujua hata aseme
" Kazi yangu umemaliza?
Salsa aliangalia kazi aliyopewa hakuwa amefanya hata nusu yake.
"Samahani boss.....
Samahani nini? Na unalala lala nini kazini,
huko kwako huwa haulali, kitanda kina kunguni?
Full 1000
Whatsp 0784468229
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi


Maoni