Ingia

Sema Jambo

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  artist

MIMBA YA BESTMAN 13

7th Jun, 2025 Views 49

MIMBA YA BESTMAN 13

Baada ya muda mulky alishituka baada ya kushikwa mabegani .
"Vipi mke wangu mbona umeniacha mwenyewe kitandani umekuja kusimama huku mwenyewe?
" Sina usingizi nikaamua kuja huku kupunga upepo. Alijibu mulky huku akionekana kuwa na wasiwasi.
" Vipi mbona kama una hofu?
Ni kweli mulky alikuwa na hofu lakini alificha kwa tabasamu alimgeukia mume wake na kuweka mikono yake juu ya mabega ya Yasini na Yasini aliushika kiuno cha mulky huku wakiwa wanaangaliana usoni.
Mulky akasema
" Unasema nina hofu? Kwani naonekana kuwa hivyo?
" Nahisi hivyo.
" Nawezaje kuwa na hofu ikiwa wewe upo pamoja nami hapa?
Yasini alitabasamu kisha akasogea karibu na shingo ya mulky na kumbusu kwenye ngozi yake nyororo ambayo ilimpa msisimko Yasini .
" Hivi ni kweli umekosa usingizi au kuna jambo lingine mke wangu?
Hili swali kilimshitua kidogo mulky mpaka akahisi huenda Yasini kamsikia alivyokuwa anaongea na simu.
" Unahisi nakudanganya?
Yasini alimuangalia vizuri kwenye macho alafu akasema
" Mbona kama ulikuwa unalia?
" aaaaah....
" Aaaaah nini mke wangu kipenzi? Aliuliza Yasini huku akiwa ameshika mulky mashavu.
Mulky alipata jibu la haraka akajibu
" Nilipata ndoto mbaya usingizi ukakata ,sikupata tena usingizi ndio maana nikaja hapa japo nipigwe na huu upepo.
" Umeota nini?
" Ndoto za ajabu tu.
"Pole sana mke wangu.
" Asante"
" Wakati mwingine ukijisikia vibaya , iliita ndoto mbaya , ikikosa usingizi basi usisite kuniamsha.
" Sawa.
Yasini alimshika mkono wakaenda kukaa kwenye kiti, Yasini alimgeukia mulky na kumshika viganja vya mikono yake kwa upendo mkubwa alafu akasema.
" Mulky Unajua wewe ndio ulimwengu wangu nahisi siwezi kuishi bila wewe mulky kila siku naomba Mungu uwe wewe tu sina ubavu mwingine na siwezi kubadili ubavu natamani unizike nikitokea na huo ndio uwe mwisho wetu.

Maneno ya Yasini yalikuwa mazito sana yaliugusa moyo wa Mulky na kufanya machozi yatililika machoni kwake. Yasini alimfuta kwa kutumia kiganja chake cha mkono , Mulky alishindwa kuficha hisia zake alimkumbatia Yasini na kumwambia kuwa anampenda sana.
Yasini alitabasamu huku akiwa anampapasa mgongoni na kumjibu.
" Nakupenda zaidi ya sana umenibimipia kwa mengi mke wangu na kuwaficha mapungufu yangu.
Hapo moyo wa Mulky ulimsuta alijihisi kufanya kosa kwani haikuwa kweli moja alisaliti pili akimsimulia kila kitu rafiki yake Hamida.
Yasini alivunja kumbatio na kumwambia
" Bado ni usiku twende tukapumzike mke wangu.
Walinyanyuka wakaelekea chumbani .
Walipanda kitandani wakalala huku Yasini akiwa kamkumbatia.

Muda ulienda walikuwa kimya na kila mmoja alikuwa macho, Mulky alikuwa kajilaza kifuani kwa Yasini huku akiwa anasikiliza mapigo ya moyo ya Yasini yalivyokuwa yanadunda .
" Baby...
Mulky aliita kwa sauti ya chini na Yasini akitikisa
" Naam, niambie mke wangu.
Mulky alinyanyua uso wake akamuangalia Yasini .
" Kwa mapenzi unayonionyesha nahisi nitakuwa kupagawa.
Yasini alitabasamu kisha akanyanyuka kidogo na kumbusu kwenye paji la uso huku mikono yake ikiwa imemkumbatia vizuri.
Mara simu ya mulky ilitoa mwanga Yasini akaona.
" Simu yako imewaka . Alisema Yasini huku alinyoosha mkono na kutaka kuchukua, mulky aliudaka mkono wa Yasini na kumzuia.
" Hapana achana nayo.
" Kwanini , itakuwaje kama umetumiwa ujumbe kuna mtu anashinda?
" Mume wangu huu ni muda wangu mimi na wewe sipendi kusumbuliwa hata kidogo hata kama kuna tatizo nitafanya nini muda huu? Alafu nahisi ni watu wa mitandao ni kawaida yao kunitumia messege usiku.
" Sawa .
Yasini alikubali , Mulky alisogeza midomo yake karibu na midomo ya Yasini wakaanza kukiss na kujikuta wamezama kwenye huba zito baada ya hapo walipitiwa na usingizi mzito kwaajili ya uchovu na hekaheka za kupeana burudani
[5/20, 10:43 PM] K. Hassan: Kesho yake asubuhi wahudumu wakiwaelekeza kifungua kinywa chumbani kwao walikula pamoja baada ya hapo Yasini alimtaka watoke wakazungumze kwaajili ya kuangalia mazingira.
Walikodi gari kwaajili ya kuwazungusha sehemu za kuvutia na kufanya manunuzi ya vitu vilivyowavutia.
Mulky alifurahia sana baada ya kuzunguka sana waliingia kwenye restaurant kwaajili ya kupata chakula .
Wakiwa wanakula chakula ghafla Mulky alikuwa mbali sana kimawazo mpaka aliacha kula akawa kazubaa tu.
" Hey... Yasini alimuongelesha lakini bado alikuwa mbali mpaka akaanguka ndipo Mulky akashituka.
" Una matatizo gani?
" Hapana.
" Hapana wakati nakuomba kabisa upo mbali sana kimawazo.
" Achana na hayo tuendelee kula.
Alijibu mulky huku akiendelea kula . Yasini alimuangalia akagundua mke wake hayupo sawa.
" Mulky kuna kitu unanificha?
Mulky alimuangalia kisha akasema
" Sijawahi kujificha jambo .
" Sasa mbona haupo sawa? Inamaana mimi ni mgeni kwako sijui kama upo sawa au una shida? Kumbuka tuna miaka miwili kwenye ndoa yetu nakujua vizuri sana.
Mulky aliacha kula alishusha kijiko kwenye sahani alafu akashusha pumzi na kusema.
" Jana nilipata ndoto ya kutisha sana labda ndio sababu ya mimi kuwa hivi
" Ni ndoto gani hiyo ambayo hutaki kuniambia

Full 1000
Whatsp 0784468229.
   

SIMULIZI NA SAUTI
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork

HONGERA WEWE NDIO MSHINDI WA VOCHA YA LEO VOCHA NAMBA (499712343590381) MTANDAO VODACOM TUMA NENO NIMESHINDA KWENDA NAMBA 0768304821


mjukuu rewards 100 Comments 0
 

MSHANGAZI EPISODE 1

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

MIMBA YA BESTMAN 13

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

MIMBA YA BESTMAN 10

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

YAMENIKUTA

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

MIMBA YA BESTMAN 9

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

JINSI YA KUTUNZA UKE

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

PART 5 MY HEART

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

MY HEART 03--04

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

*MY HEART* *1---2 *

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

MIMBA YA BESTMAN 7

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

ANIPHA 6--7.

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

MIMBA YA BESTMAN 05

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

side chick episode 3

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

SIDE CHICK EPisode 2

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 18

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 17

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 16

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 8

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

CAREEN Sehemu ya 1

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

RATIFA Sehemu ya 32

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

JINA LANGU SHAMSA EP3

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

JINA LANGU SHAMSA EP2

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

JINA LANGU SHAMSA EP1

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

BOYCHILD PART 3

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

DRAMA OF LOVE part 4.

mjukuu rewards 100 Comments 0
 

DRAMA OF LOVE part 3

Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest