MIMBA YA BESTMAN 9
Mara kwa mara Sameer alikuwa akimtembelea Mulky na walifurahia penzi lao bila mtu yoyote kujua kwani hata mlinzi hakuweza kushituka sababu tangia hapo mwanzo Sameer alikuwa akienda nyumbani kwa Yasini.
Siku moja wakiwa wamekaa sebleni Sameer alikuwa kajilaza mapajani kwa Mulky huku mulky akiwa anampapasa uso wa Sameer na waliongea mambo yao ya kimahaba kifupi ilikuwa ni furaha sana kwao.
Wakiwa wamejisahau walisikia sauti ya viatu ilimaanisha kuna mtu anaenda.
" Nahisi kuna mtu anakuja.
Alisema Sameer baada ya kusikia.
" Hakuna mtu ambae anaweza kuja kunitembelea muda huu.
Sameer alikosa amani alinyanyuka haraka akakaa.
" Hebu jitulize bwana hofu ya nini kama mlinzi hawezi kuja huku muda huu hata likitokea tatizo atapiga simu, Yasini bado sana kurudi.
" Niamini mimi kuna mtu yupo mlangoni.
Mulky aliamua kunyanyuka akaenda mpaka mlangoni akafungua kweli alimkuta Hamida kasimama mlangoni.
" Wewe umekuja saa ngapi?
" Mbona kama una wasiwasi , haujapenda mimi kuja kwako?
" Sina maana hiyo sio kawaida yako kuja kwangu bila kunipa taarifa .
" Basi ndio imetokea leo.
" Sawa Karibu ndani.
Mulky alimpisha Hamida akaingia ndani huku nyuma mulky alifunga mlango,Hamida alisalimiana na Sameer kisha akakaa.
" Nilikuwa na shemeji yangu ananichangamsha hapa. Mulky aliongea hivyo baada ya kumuona Hamida anamuangalia Sameer kwa jicho la kumtilia shaka.
" Sawa. Alijibu Hamida huku akitoa tabasamu.
Wakati huo Sameer hakuwa na amani alihisi hamida kawashitukia pale alipo anawachora tu akaamua kuaga.
" Sasa shem acha muda wangu wa kukaa hapa umeisha acha niwakimbie.
" Sawa.
" Ujio wangu ndio unakukimbiza? Aliuliza Hamida.
"Hapana nilikuwa hapa muda mrefu sana.
" Sawa.
Sameer alinyanyuka na kuondoka. Hamida alimgeukia Mulky na kumkazia macho usoni.
" Vipi mbona unaniangalia hivyo?
" Nahisi kuna kitu kinaendelea kati yako na huyo bestman wa .....
Kabla Hamida hajamaliza kuongea Mulky alimkatisha kwa kuuliza
" Kitu gani unachokihisi?
" Mulky sitegemei kama unafikiria kujificha kitu wakazi kuna kitu nahisi nimekoshuhudia kwa haya macho yangu mawili.
Mulky alishituka na mapigo ya moyo wake yakienda mbio.
" Umeona nini?
" Una mahusiano na Sameer.
" Unaongea nini wewe, Sameer ni rafiki mkubwa wa Yasini hivi kama mtu akija akasikia unaongea hayo maneno si itakuja kuleta shida na kwa upande wangu utakuwa umeniweka kwenye wakati mgumu sana unajua dhana sio kitu kizuri alafu mimi na Sameer tunaheshimu ana sana.
Mulky alilalamika ili kumuaminisha Hamida kuwa hakuna chochote kinachoendelea kati yake na Sameer.
" Sawa nimekuelewa shoga yangu.
" Naomba usije ukaingia tena kitu kama hicho.
" Nimekuelewa mama.
Waliamua kuachana na hizo habari wakaendelea kuongea mambo yao mengine.
Siku zilisogea Uhusiano wa Sameer na Mulky ulipamba moto muda ambao Yasini hakuwepo waliutumia vizuri sana hiyo nafasi walikutana hotelini kwaajili ya uhuru zaidi na kumaliza shida zao.
Siku moja wakiwa kwenye chumba cha hotel Mulki akiwa Kamlia Sameer kifuani alisema
" Si Unajua Yasini anarudi kesho ?
Sameer alishusha pumzi kisha akasema
" Najua . Sasa itakuwaje kuhusu uhusiano wetu ?
" Unataka kuniambia tutaachana?
" Sitamani hata kidogo iwe hivyo nakupenda sana Mulki na endapo ikatokea ukatoka kwenye ndoa yako basi nitakuwa.
Mulky alimuangalia Sameer huku akiwa anacheka
" Unacheka nini sasa kwani mimi siwezi kukuowa?
" Kumbuka una mchumba uneshamvalisha pete na unamalengo nae sasa usitake kunidanganya nikavunjika ndoa yangu kwa mikono yangu.
" Kwani uchumba si huwa unavunjika?
" Kwenye hilo swala hapana bora tuendelee tu kufanya siri na kila mmoja abaki kwenye mipaka yake.
" Unataka kuniambia utavumilia kwenye hiyo ndoa ?
" Kwa sasa wewe upo hivyo sina shaka nitakuwa napata kila nitakachokuwa nataka shida yangu imeisha sitaumiza tena kichwa .
Sameer akitabasamu na kukubaliana nae.
Waliongea mambo yao mengi kuhusu uhusiano wao baada ya hapo Mulki alinyanyuka akaingia bafuni kuoga kisha wakaagana akaondoka alirudi kwake na kumuacha Sameer pale kwenye chumba cha hotel.
Kesho yake mapema sana Mulky aliamka akiwa kachangamka na kuanza kufanya maandalizi ya kumpokea mume wake. Aliweka sawa mazingira ya chumba chake cha kulala na kuonekana na mvuto , harufu nzuri ya kuvutia . Alipomaliza aliingia bafuni akaoga alipomaliza alijifunga kipande kimoja cha kanga nyepesi na kwenda kusimama mbele ya Kioo cha dressing table alijiangalia kwenye kioo huku akisema.
" Anakuja sasa sijui nitaweza kujigawa vipi maana kumiliki na bwana wawili kwa wakati mmoja ni mtihani mkubwa sana kwangu na wote naona kila mmoja anafaida kwangu
Mume wangu Yasini japokuwa ana mapungufu lakini nampenda sana na Sameer ni mwanaume anaeniliwaza na kunipatia kile ninachotaka sasa hapa natakiwa kucheza kwa akili sana na siri mno.
Hivi nitaweza kweli tamaa ndio zinanihadaha?
Lakini Sameer ndio pumbazo la moyo na Yasini ni mume na ndio mwanaume aliyestahili kunipa kile ninachopata kwa Sameer sasa hapo nafanyaje jamani kwani hiki ninachofanya nitalaumiwa?
Mulky akiwa bado anawaza na kuwazua simu yake iliita. Aliekuwa anapiga alikuwa Sameer.
" Hallow.
" Habari yako asali wangu.
" Salama. Alijibu mulky huku akiwa anatabasamu.
" Uko wapi muda huu?
" Nipo nyumbani najiandaa kwenda kumpokea Yasini.
" Oooh sawa . Nimekupigia simu kukukumbusha kuwa ufute msg zote usiache ushahidi wowote .
" Nimeshafanya hivyo mapema sana.
" Safi sana nakupenda.
" Nakupenda pia.
" Ok bye.
Mulky alikata simu na kuanza kujiandaa kwaajili ya kwenda kumpokea mume wake.
Yasini alifurahi kuonana na mke wake.
" I miss you my wife.
Alisema huku akiwa kamkumbatia.
" Nilikukumbuka pia karibu tena nyumbani mume wangu.
" Asante.
Waliongozana kwenye gari yao na kuanza safari ya kurudi nyumbani kwao.
Walipofika nyumbani Mulky alifanya majukumu yake kama mke alimuandaa mume wake kwaajili ya kuoga alafu yeye akaenda jikoni kuandaa chakula .
Baada ya Yasini kutoka kuoga alitoka bafuni akakuta mke wake amemuandalia nguo za kubadili .
Alichukua zile nguo akavaa baada ya hapo alitoka na kwenda kuungana na mke wake kwenye meza ya kulia chakula.
" Vipi mke wangu kila kitu kipo sawa ? Usalama upo?
" Ndio usalama upo " "unauhakika hakuna ambae alikuwa ananisaidia majukumu? Aliuliza Yasini huku akiwa anamuangalia Mulky usoni.
Mulky alishituka, mapigo yake ya moyo yalifunga kwa kasi alihisi huenda Yasini anajua kitu kuhusu yeye na Sameer pale pale mawazo yake yalipelekwa kuwa Hamida anaweza akawa kamueleza kitu Yasini kwani hakuna mtu mwingine aliekuwa anawashuku zaidi ya Hamida.
" Inamaana Yasini kakutana wapi na Hamida mpaka akamwambia ......
Ukimya wa Mulki ulimfanya Yasini aulize
" Vipi mbona umeshituka inamaana ni kweli kulikuwa na mtu ambae ananisaidia majukumu yangu?
Full 1000
Whatsp 0784468229.