Ingia

Sema Jambo 2025

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  gonga94 official track

KICHAA NA MIMBA YA BOSS SEHEMU YA KUMI NA TANO*

18th Sep, 2025 Views 25



Shahidi alinyamaza kidogo.

Nilmekuuliza nataka jibu Shahid.

Mama naomba kesho nije tuongee kwenye simu hatutaelewana.

Nataka kesho mapema kabisa uje, yani kabla haujaenda kazini. Baba yako anahitaji kujua hili kwa kina

Sawa mama. Shahid alikata simu na kuendelea kucheza na Shania.

Kesho yake Shahid aliamka mapema sana huku Shania akiwa Kalala pembeni Akimuangalia na kujisemea. yake

Hakuna mtu wa kuvunja upendo wetu Shania, nitapambana, nitakupigania wewe na mtoto wangu sitakubali uwende mbali na mimi.

Baada ya kufikiria alinyanyuka akaenda jikoni, alimkuta Tessy anaanza kufanya usafi.

*Habari Tessy.

*Salama baba kijacho mmeamkaje?

Shahidi alitabasamu

Salama, vipi umeandaa kifungua kinywa?

Bado nafanya kwanza usafi ndipo niandae.

Achana na mambo ya usafi nilikwambia

ukitamka tu anza kuandaa kifungua kinywa

unajua Shania huwa anaamka na njaa sana.

Sawa Boss naandaa sasa hivi. *Fanya haraka tafadhali.

Sawa.

Ilipofika Mida ya saa tano Shahid aliondoka na kuelekea nyumbani kwao kwaajili ya kuongea na

wazazi wake.

Alifika nyumbani kwao na kusalimiana nao baada ya hapo kikao kilianza.

Shahid kuna kitu gani cha ajabu umefanya ? Mama yake aliuliza.

"Hakuna kitu cha ajabu nilichofanya.

Kwahiyo unataka kusema kuishi na kichaa ni

kitu cha kawaida? Baba yake alidakia.

Wazazi wangu naombeni mnipe muda kidogo. niweze kujielezea.

*Utatuambia nini tukuelewe wakati unatusibisha

na kushusha heshima yetu? *Sio kweli wazazi wangu kumbukeni hata kichaa

nae ni mtu anatakiwa kupendwa na

kuthaminiwa. *Toa maneno yako ya kipuuzi hapa huyo kichaa

wako sitaki kumsikia. Mtanisamehe wazazi wangu nampenda sana

Shania na yeye ni mama wa mtoto wangu anayetarajiwa kuzaliwa mwezi ujao tu. Shahid mwanangu hivi kwa wadhifa wako ni

wakiwa na mwanamke kichaa kweli? Mama nilipokuwa na Aisha ulikuwa uliniambia ni mwanamke jeuri, hana heshima, ufujaji wa

pesa hafikirli maendeleo yeye ni anasa na starehe. Na mimi niliona hilo na nikakubali tabia

zake japo kuwa nilikuwa nakupa muda nikidhani atabadilika lakini kabla sijasikia nilipokuwa natarajia kufika ikatokea bahati mbaya kwa

Shania na akapata ujauzito.

*Hivi mwanangu watu si watasema Ulimboka kichaa kwasababu ya kupata pesa. *Wacha waseme mama ukweli najua mimi.

*Sisi hatumtaki.

"Wazazi wangu siwezi kumuacha.

Sikiliza wewe kama huwezi kumuacha huyo

kichaa wako basi hatutafikia kwako. Aliongea baba yao kwa hasira kisha akanyanyuka na

kuingia ndani.

Shahidi umeona baba yako kakasirika shauri yako upate radhi ya baba yako.

*Mama hakuna radhi ya aina hiyo.

Sasa kaa na ubishi wako litakalo tokea na huyo kichaa wako sisi hatupo. Ngoja siku moja ukiwa

usingizini akunyonge mpaka ufe.

Shania ni kichaa kweli lakini sio mkorofi. Hakuna kichaa ambae sio mkorofi nyie ndio

wale mnaambiwa mke wako kipofu unasema hapana ni chongo, sasa endelea kumlea huyo chizi wako likikukuta ndio utaelewa tulikuwa tunaongea nini.

*Lakini atakuwa mama wa mtoto wangu. Hiyo sio sababu ya wewe kung'ang'ania nae akijifungua tunamnyang'anya mtoto

anaenda zake mtaani.

Haiwezekani hatuwezi kufanya dhuruma atamlea mtoto wake kwanza vichaa wanajua

malezi.

"Eeeee... Sasa kaa na ujinga wako pumbavu. Mama yake pia aliondoka na kumuacha akiwa amekaa.

Shahidi alikaa kwa muda huku akiwa anafikiria ni

jinsi gani atamsaidia Shania na kurudi kwenye hali ya kawaida maana maneno ya wazazi wake yalimuumiza sana alipamani kuibuka mshindi

kwenye swala la Shania. Baada ya muda alinyanyuka akaenda kupanda kwenye gari lake na kuondoka.

Alielekea moja kwa moja kwa shangazi yake Shania.

Shikamoo shangazi.

*Marahaba. Shahidi kuna usalama kweli, mbona asubuhi asubuhi?

Ni salama shangazi ila kuna baadhi ya mambo kuhusu Shania nataka kuyajua ili yaweze

kuwawakilisha kwa daktari kabla ya kuanza matibabu yake.

Eheee unataka kujua nini?

*Kuna sababu iliyosababisha Shania kuwa vile? Ndio kuna sababu iliyofanya Shania kuchanganyikiwa na kuwa kichaa.

Itaendelea....

Full 1000
Whatsp 0784468229.
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

KICHAA NA MIMBA YA BOSS SEHEMU YA KUMI NA TANO*  >>> https://gonga94.com/semajambo/kichaa-na-mimba-ya-boss-sehemu-ya-kumi-na-tano

#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

Maoni

You're not logged in
Click here to login and comments
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
gonga94 official track
ZETU
SIMULIZI NA SAUTI ZETU
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
Tangazo - PROMOTE YOUR BUSINESS FOR FREE
PROMOTE YOUR BUSINESS FOR FREE
PROMOTE YOUR BUSINESS FOR FREE

RATIBA YA SIMULI ZETU

Hakuna ratiba iliyopangwa kwa sasa.


Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest