Sikujibu chochote ni machozi tu yakawa yananitoka, alinifuta machozi mpaka akachoka akaamua kunilaza tu, apo simu yake ikaanza kuita alikuwa ni bi mdogo Asha, Amir aliogopa ata kupokea hio simu,akihofia ninaweza kupanic zaidi, aliamua kumjulisha mke wake kwa sms, avumilie hatoenda siku tatu hizi zipite ndo watakutana, Asha alipanic akaanza kulalamika, Amir aliona kabisa atapasuka kichwa akaamua kuzima kwanza simu, amalizane na mimi...
Mimi sikujua chochote nilikuwa namengi kichwani, siku 10 zilipita nikawa nimepona, niliamua kuigiza niko sawa ili nipelekwe kwetu, lakini Amir alikataa akadai nitakaa kwa Bibi yake, nikiwa sawa nitaenda kwangu, nilijikuta nazidi kuchukia tu, uzuri pia muda wa kurudi kazini ulikuwa umefika, Amir alienda kwa bi mdogo, alipokerewa na lawama, alijuta kuoa, alijitahidi kumuelewesha pia na kumbembeleza, alikaa saba zote, akamaliza ila ni kwa masharti hakuna kunipigia simu mpaka saba ziishe kama yeye alivyokaa kimya bila kutusumbua, kwangu nilikuwa naumia, na sikutaka kupiga simu kila nikicheki ata sms tu ya kunijulia hali hamna nikawa naumia mno...
Najikaza tu, nilikuwa ni mtu wa kujifungia tu ndani, sona story na mtu, mama angu alikuja na ushauri nisikirizie kama mwanaume atakuwa mbaguzi ndo nidai taraka nijipe muda swala la taraka sio dogo,nilimuitikia tu, make sikuwa nimeeelea chochote,aliondoka na kunitakia kazi njema nake ilikuwa bado siku mbili niende kazini, siku moja kabla ya kwenda kazini, Amir alilidi, alikuta watu wengine wote wake sebren kasolo mimi tu, aliniulizia, akaambiwa nipo chumbani, akaja kugonga nilijua ni bibi niliinuka kwenda kufungua, apo nimekonda atari,nafungua tu ivi...
Nakutana na Amir, ata sikujisumbua kuongea nikaachia tu mlango na kuludi kuendelea na kazi zangu, aliingia ajanikumbatia kwa nyuma nakuuliza maendeleo yangu, nilijibu tu kifupi, niko sawa, nikajitia kwenye kumbato, nijaendelea na mambo yangu, Amir alisogea nakuniomba msamaa kwa kuwa kimya mda wote, mimi ata sikujibu chochote wala kuliweka akilini, akajua nkimechukia pia, akaanza kunimbembeleza nikawa nahisi ananipigia tu kelele, niliamua tu kuongea niliona kabisa atanipasua masikio, Amir mimi ata ukikaa mwaka bila kunitafuta sio tatizo hivyo acha kuongea ongea mimi saiv siwazi ubayo yawazi wala sihitahi mashindao na mtu ya kusalimuwa wala kutembelewa, we ni mtu mzima aisee, amka ukaoge ule ulale kesho uko zamu, niliongea nikatoka Amir alikosa amani kabisa, akatamani ata nimgombeze, nilalamike, ila ata dikujisumbua nilienda nikaanda chakula chake, nijaludi chumbani nikamuandalua pajama za kulalia nikamuandalia na nguo za kutokea, nilikuwa sijisikii kuongea nikaona uvivu kumuuliza kama atalala au anatoka nikaandaa zote ili yeye mwenyewe achague, huwa siku zote nashinda chumbani, ila leo alivyokuja tu, nikaamua kwenda kushinda bustanini tu peke yangu...
Itaendelea....π₯
Full 1000
Whatsp 0784468229.
Hakuna ratiba iliyopangwa kwa sasa.
Maoni
Click here to login and comments