MADAM NIPE KIDOGO BASI 7
Yule nurse alimuangalia Yule kijana kwa dakika kadhaa kisha akasema “ wewe ni mdogo sana kendric bado haujaelewa kabisa unachokiongea, kisha akasimama na kuondoka zake….
Kendrick alijisikia vibaya sana, maana hana udogo wa kushindwa kumpa furaha mwanamke ambae alikuwa anampenda…
Hakutaka kuongea sana, akaanza kupambana kujitengenezea mazingira ya Yule mwanamke kumuona kuwa yuko bora sana, basi maisha yakaendelea, na kwakuwa amedharaulika kwa umri wake, hakutaka kubishana nae tena, siku za Yule kijana kuendelea kukaa pale hospital zikaisha, siku anaondoka nurse veronica akamfata kwa ajili ya kumuaga kisha akasema “ wewe ni mwanaume mzuri na bora sana, na kweli ulikuwa unamaanisha maana halisi ya mwanaume bora, laity kama ungekuwa una umri mkubwa kidogo ningepambana sana niwe mkeo, maana ni miongoni mwa wanaume bora sana ambao nimeshawahi kukutana nao…
Basi Kendrick akaondoka zake…
Kw upande wa veronica akawa anaendelea na maisha yake pia, alikuwa ni mtu mpweke sana, umri wake ulikuwa unamkosesha wanaume, maana ilisemekana kuwa alikuwa ana zaidi ya miaka thelathini, na kama tunavyojua ni kuwa mwanamke akishafika umri flani anakuwa ana hofu sana kuhusu kuolewa na kwa nurse veronica ikawa ni hivyo hivyo…
Alikuwa ni mpweke mwenye majonzi na huzuni kubwa sana, alikuwa hata kazi zake haziendi vizuri, alikuwa kuna muda anamkumbuka Kendrick kutokana na bashasha zake pamoja na tabia yake njema, kuna muda akawa anamkumbuka kwa sababu ya uchapakazi wake, akiwa anajua kuwa laity kama Kendrick angekuwepo kwa kile kipindi ambacho ana msongo wake wa mawazo basi angemsaidia sana majukum yake…
Kwa upande wa Kendrick nae akaenda kumalizia masomo yake maana alikuwa anapambana sana kuja kupata lesseni ya udaktari, na alikuwa anasali na kumuomba mungu sana apangiwe kazi kwenye hospital anayofanya kazi nurse veronica, tasiwra yake ilikataa kabisa kuondoka kwneye kichwa chake, moyo wake ulikuwa unadunda sana kila ambapo angekumbuka jina lake, upendo wake kwake ulishindwa kuondoka kabisa, ingawa aliona wanawake wengi na wenye umri mdogo na wenye mvuto sana ila moyo wake ulimchagua nurse veronica….
Basi aliamini hakuna mwanamke ambae anamtaka mwanamke ambae hana malengo na hawezi kupambana , aliamini akiwa na mafanikio basi anaweza kumpata mwanamke yoyote Yule ambae anamtaka…..
Basi kweli Mungu sio Athumani , Kendrick akapangiwa kazi kwneye kituo ambacho alikuwa anafanya kazi nurse veronica akiwa kama mganga mfawidhi wa maswala ya watoto, na akaajiriwa kabisa pale…
Nurse veronica alipomuona alifurahi sana, kwa maana alikuwa mfariji wake mkubwa sana kipindi ambacho alikuwa ameenda pale hospital kwa sababu ya field…..
Basi wakasalimiana na majukum yakaanza, Kendrick alikuwa amebadilika sana, ingawa kilikuwa kimepita kipindi kifupi sana ambacho hakikuwa kimemaliza hata mwake, ila alishaanza kutoka ndevu, na alikuwa anakifua cha mazoezi, zile ndevu pamoja na mwili wake zikambadilisha kabisa ,muonekano wake, ile sura yake ya ukijana mdogo iliondoka na ikaja sura ya mwanaume kamili….
Alikuwa anavutia ila alikuwa anamisingi na misimamo yake, hapo wakati wanaigiza, kweli Kendrick akaenda kubandika ndevu na ni kweli muonekano wake ulikuwa umebadilika sana…..
Kuna mvuto alikuwa nao, ila hilo halikubadilisha jambo lolote kwangu, niliendelea kumuona kama mwanafunzi wangu, tena kijana mdogo ambae alikuwa ana ndoto zake kubwa, na kiukweli sikuwa tayari kuzikatisha kwa namna yoyote ile…………..
ITAENDELEA….
Full 1000
Whatsp 0784468229
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi












Maoni
Tangaza biashara yako bure hapa >>> https://www.gonga94.com/tangazo