MIMBA YA DHARURA 10
Amina alibaki ameduwaa, macho yakimtazama rafiki yake kana kwamba hakuamini kile alichokisikia.
“Nadia unasema Kabir ameoa? Na sherehe ile ilikuwa ni yake?” aliuliza kwa mshangao.
Nadia alifunika uso wake kwa viganja vyake viwili, machozi yalitiririka taratibu.
“Ndiyo Amina mbele ya macho yangu nimeona kila kitu, nimeona upendo wake kwa mke wake, nimeona furaha yake. Na hapo ndipo moyo wangu ulinikumbusha kuwa mimi na mwanangu hatuna nafasi tena kwake.”
Amina alimsogelea akamkumbatia kwa nguvu.
“Pole sana rafiki yangu, lakini kumbuka hata bila kabir maisha bado yanaendelea. Hata kama Kabir ameoa, wewe bado una hazina kubwa mtoto wako Tawakal. Huyo ndiye faraja yako.”
Nadia akamvuta Amina karibu zaidi, akizungumza kwa sauti ya kubanwa na kilio.
“Lakini Amina moyoni mwangu bado kuna mapengo. Sijui nitamwambiaje mtoto wangu siku akiniuliza baba yake ni nani.
Sasa nitamwambie nini? Baba yake yupo, lakini anaishi maisha yake mapya?”
Amina alikaa kimya kwa muda, akitafuta maneno sahihi ya kumfariji. Hatimaye akasema,
“Usiharakishe majibu, rafiki yangu. Wakati ukifika, Mungu atakupa hekima ya kumjibu mwanao. Kwa sasa, jipange na maisha yako. Usiruhusu maumivu ya jana yakuvunje moyo.
Nadia alinyamaza, machozi yakiendelea kumtiririka. Kichwa chake kilikuwa kimejaa taswira za Kabir tabasamu lake, jinsi alivyoshika mkono wa mke wake, jinsi walivyocheza wakiwa na furaha isiyo na kifani. Hisia za kale zikamvamia kwa nguvu, alikumbuka jinsi alivyokuwa akimbembeleza usiku waliokuwa pamoja, kumbatio lake na jinsi alivyokuwa akimbembeleza na kumuangalia kwa jicho la huruma alipokuwa alimuomba msamaha.
Lakini licha ya yote kuna kitu kilichomshtua zaidi:
Macho ya Kabir alipomwangalia. Yale macho hayakuwa ya furaha kamili. Kulikuwa na kitu wasiwasi, mshangao, na labda… maswali.
Amina alimshika mkono. “Nadia, kuna kitu kimoja nahisi… Kabir hakuamini kile alichokiona. Naamini hakutarajia kukuona tena. Huenda bado kuna mambo hayajaisha kati yenu unatakiwa kumpa muda na nafasi .
Nadia akatikisa kichwa kwa haraka.
“Hapana Amina! Yeye tayari ana mke, maisha yake ni mapya. Mimi si kitu kwake tena. Alafu kumbuka hatukuwahi kupendana kukutana kwetu ilikuwa bahati mbaya tu.
Aliongea hivyo lakini moyoni, sauti nyingine ilimnong’oneza:
“Kwa nini macho yake yaliniangalia vile? Kwa nini alipoteza tabasamu aliponiona?”
" Nadia mimi naamini kuwa bado kuna nafasi huenda akijua ana mtoto anaweza kuwa pamoja nanyi.
" Kwani huyo mke wake hawezi kumpa mtoto?
" Aghhhhhhh tatizo unawazia mabaya tu nimesema jipe muda kwanza.
" Hakuna haja ya mimi kumfikiria nitaangalia maisha yangu na mtoto wangu basi. Sitamfikiria huyo Jabir wala nani.
Nadia aliongea kwa hasira kisha akanyanyuka na kwenda chumbani kwake.
Baada ya siku mbili akiwa kazini Jayden alimfuata ofisini kwake.
" Vipi mama....
" Tawaqal. Alijibu Nadia huku akiwa anatabasamu.
" Mtoto wako umempa jina zuri sana.
'" asante.
" Nadia kuna jambo nataka tuongee .
" Lakini ni muda wa kazi.
" Najua hiyo kazi anayoifanya haina haraka sana.
"Sawa nakusikiliza mkuu wangu wa kitengo.
" Kuna kitu natamani kutoka kwako....
" Kitu gani? Aliuliza Nadia huku akikaa vizuri kusikiliza hicho kitu.
" Unaweza kunipa nafasi nikawa baba wa mtoto wako?
Maneno ya Jayden yalilenga kwenye moyo wa Nadia na kuleta hisia tofauti tofauti.
" Samahani umesema nini?
" Nimesema unipe nafasi ya kuwa baba wa mtoto wako. Sio kwasababu najionea huruma bali ni sababu ya upendo wangu uliopo juu yako natamani kuwa sehemu ya maisha yako na maisha ya Tawakal.
" Jayden unajua unachokisema?
" Ndio Nadia na nimekifikiria kwa kina kabla ya kuja kwako.
" Lakini Tawakal ana baba yake hata kama hayupo karibu .
" Sijapinga hilo atabaki kuwa mtoto wa huyo mwanaume . Nadia nipe nafasi ya mimi kuwa wako natamani sana kuwa ubavu wangu . Sitapoteza muda nitafanya haraka sana kumiliki na kukuweka ndani kwangu tena kihalali kabisa.
Nadia alizidi kumshangaa Jayden mwanzo alihisi kama masihara lakini kila dakika zilivyo zidi kwenda aligundua kile alichoongea Jayden alikuwa anamaanisha.
" Moyo wangu bado umebeba maumivu.
" Sasa umefika wakati wa mimi kutuliza hayo maumivu yako kwa upendo wa dhati.
Nadia alisita kidogo bila kuongea .
" Nadia sio lazima unipe jibu leo una muda wa kufikiria hili na sio lazima ukubali nitaheshimu maamuzi yako.
Jayden alimaliza kuongea kisha akanyanyuka na kutoka ofisini kwa Nadia.
Nadia aliduwaza na kuona mtihani mwingine unakuja kwenye maisha yake.
Ilikuwa vocatio, ikaja kuachwa na Jawad sababu ya mimba, kabir kuowa na sasa nimpe nafasi Jayden.
Full 1000
Whatsp 0784468229
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi














Maoni