Mama Farida akibaki katia nacho kumuangalia Shahid hakuwa anaelewa kanisa kile alichokisikia kutoka kwake.
'Kijana sijui kama sijasikia vizuri au sijaelewa?
Mama ujauzito wa Shania mimi ndio muhusika. Abeee....?. Mama Farida aliishia kuitika kamal vile aliitwa.
"Mama nipo hapa kuweka mambo sawa na nipo tayari kumuowa Shania na kumuhudumia kwa kila kitu mpaka atakapo kaa sawa.
Mama Farida aliendelea kumuangalia Shahid
bila kummaliza
'Wewe mtoto wa kiume mbona inanishangaza au ni imani za kishirikina ndio zimekusukuma kufanya hivyo?
Hapana, hapana mama mimi ni mtu safi kabisa sina imani hizo hili lilitokea kwa bahati mbaya na nafsi yangu inanisuta mno kwa nilichokifanya ndio maana nipo hapa kwaajili ya kusafisha. makosa yangu nia yangu ni njema kabisa.
Mama Farida aliendelea kumuangalia Shahid bila kuongea chochote na kichwani kwake alikuwa anaongea mengi sana.
Huyu kijana mtanashati na nadhifu aliweza vipi kuwa na Shania ambae kuoga tu kwake ni
mtihani, jamani wanaume mmmh. Mama.... Baada ya Shahid kuita ndio.
akamzindua kutoka kwenye mawazo. Mwanangu hapa sina la kusema sijui nitoe jibu gani.
Kimnya kilitawala kwa muda Mara akatokea Shania, Shania alipomuona Shahid alifurahi anamkimbilia na kumkumbatia kwa furaha.
mama Farida akibaki mdomo wazi, Shahid alibaki kuning'iniza mikono huku akimuangalia mama Farida.
Mama Farida alishangaa mwishowe alipiga makofi. "Makubwa haya.
Shahid alimtia Shania mwilini kwake akamuangalia usoni kwa huruma huku akitoa tabasamu dogo kisha akamjalisha chini kwenye.
mkeka.
Marma nadhani utakuwa umeona kitu kati yetu.
Nimeona baba, nimeona nyoyo zenu zinasemekana zinaongeza rugha moja Sasa kwa leo mimi sina la kusema acha nije nikae na ndugu tuzungumze kesho jioni uje.
Sawa mama. Shahidi alitoa kadi ya namba za
simu na kumpa mama Farida.
Endapo litatokea lolote basi naomba unitafute kwenye hii namba.
Sawa. Mama Farida alitilia huku akiwa
anamuangalia Shahid usoni akiwa haamini amini. "Leo hutaki mia mbili?
Nataka.
Shahidi alimshika pia yake kisha akatoa Wallet na kumpa noti ya elfu mbili na kiasi kingine cha pesa alimpa mama Farida.
Asante baba.
Mama acha mimi niende.
Sawa
Shahidi alimuangalia, Shania aliangalia vidole
vyake vya mikono huku akivichezea.
Shania sasa unatakiwa kukaa nyumbani utulie mimi naenda kukuletea maembe.
Haya.
Baada ya hapo Shahid aliaga na kuondoka. Mama Farida alikuwa anamsindikiza kwa macho
hadi akawa anamchungulia. Alimsindikiza kwa macho mpaka alipopotea
kwenye upeo wa macho yake kisha akamuangalia Shania ambae alikuwa anaangalia. hela aliyopewa huku akicheka cheka.
Mama Farida alitingisha kichwa.
Hil dunia ina mambo kweli yani yule kijana. alivyo na huyu Shania wapi na wapi na alianzaje anzaje? Mama Farida alijiuliza maswali mengi yaliyokosa majibu.
Mara Farida alifika
Jamani mbona kila mtu kashika hela kuna gari la msaada kimepita hapa?
Shania alikuwa anamlingishia alafu anaficha. Farida mwanangu nilichokisikia na kukiona.
siku ya leo kimenistaajabisha sana. Ni kitu gani mama? Aliuliza Farida huku akitaka
kukaa.
Wala usikae ingia ndani kwanza ukanichukulie simu. Farida aliingia ndani akachukua simu na kumpatia mama yake.
Mama Farida alianza kuwapigia ndugu zake na kuwataka wakutane jioni nyumbani kwake. Baada ya kuongea na simu Farida alimuuliza
mama yake.
Mama mbona inakusanya watu kuna nini?
Mwanangu kuna kijana mmoja kaka na gari yake hapa, ni kijana safi mtanashati na mwenye akili zake timamu Amekuja hapa anasema
ujauzito wa Shania ni wake.
Farida alimuangalia mama yake na kuanza kucheka.
Full 1000
Whatsp 0784468229.
Hakuna ratiba iliyopangwa kwa sasa.
Maoni
Click here to login and comments