๐๏ธ WALIMWOZESHA NA CHIZI KUMBE NI TAJIRI! ( Part 6)
ILIPOISHIA...,
Baada ya Turi kuwasili kwa mama yake , alikaribishwa kwa tabasamu nzito la Mama Vero pamoja na Vero mwenyewe ,
mpaka Turi alihisi hofu moyoni mwake, maana isingeweza kuwa rahisi kiasi hicho kwa mtu ambaye aliyemzoea miaka mingi na hata baada ya kupewa pesa bado alionyesha kinyongo,
sasa inawezekanaje amchekee mapema kiasi hicho!?.
Lakini,
Turi alijipa moyo na kuomba mungu amsaidie maana yeye ndiye mjuzu wa kila shari na kheri.
Alipofika hadi ndani, mama Vero haraka haraka kuriko kawaida, akamkaribisha Turi maji ya kunywa,
" karibu maji haya mwanangu Turi, maana na joto hili duuuuh!, ebu ona unavyo vuja jasho , Loooh! pole binti yangu kipenzi Loooh",
Turi hakuweza kukataa maji hayo ingawa nafsi yake ilikuwa ina wasiwasi sana!, ila kutokana na heshima na adabu aliyojaaliwa binti Turi,
aliona kama atakuwa anamdharau mama Yake akikataa maji hayo,
hivyo,
akaamua kupokea kikombe cha maji na kuanza kunywa tone moja baada ya lingine!.
Mama Vero akamkonyeza mwanaye Vero, huku akionyesha ishara ya mikono kama mkasi akimaanisha kwamba kazi imekwisha!.
Na haikupita muda mrefu baada ya Turi kunywa maji hayo, mara simu yake ikaanza kuita,
na alipochukua akakuta ni Amani!, lakini chakushangaza baada ya Turi kupokea simu hiyo! ,
Amani alianza kumfokea kuriko kawaida tena , hakutaka kumpa hata nafasi ya kujitetea,
" we mwanamke una akili timamu kweli wewe!?,
yani mtu unaweza kusema umepata mke mwema kumbe ni kibuyu kilichopasuka, unajua kabisa mimi nimetoka na wewe umetoka bila kupika na nguo zangu za kuvaa kesho zote umeziloweka kwenye maji,
una akili kweli wewe, kumbe ndo maana hata mama Yako wa kufikia huelewani naye wewe, halafu lawama unarudisha kwao,
bora hata mwanzo ningemchumbia Vero tu ,daaah!"
Turi huku akiwa analia kilio kisicho na majibu akajibembeleza kwa mumewe Amani,
" tafadhari Amani naomba unisikilize, mbona chakula niliacha na nguo ni mimi ndo nimekupigia pasi!".
Lakini,
Amani alizidi kucharuka kwa hasira isiyo ya kawaida kabisa ,
" wewe kinyago!, usinifanye mimi sina akili timamu kama ulikuwa hunitaki ungesema , kuriko nimeteketeza pesa zangu bila faida, njoo huku, mamba wee!".
Turi akiwa haelewi hayo yote yametoka wapi maana kila alichokiaema Amani , hakuna hata kimoja ambacho amekifanya ,
Turi akiwa ameduwaa kwa dakika kama tano hivi , akajisemea kimoyo moyo,
" mbona sielewi Mimi jamani, au alikuwa chizi kweli, au ni mwezi mchanga nini ndo urchin umeanza tena?!, ila si wangenambia ukweli tu!".
Mama Vero naye, akamsihi Turi arudi nyumbani akamsikilize mumewe , " mwanangu Turi!, usijali ,
kila kitu kitakuwa Sawa tu, atakuwa kachoka Tu huyo, si unajua wanaume wakirudi kazini na njaa,
weee! hata baba yako alikuwaga hivyo hivyo! mmh..! mmh...!".
Turi alikuwa kama mtu aliyechanganyikiwa, maana ndoa Yake ndo kwaanza ilikuwa na wiki moja tu!, na ukizingatia mumewe alikuwa ni mtu mwenye upendo mkubwa na huruma kwa Turi kutokana na mazito aliyopitia kwenye maisha yake,
sasa inawezekanaje ghafla hivyo eti mumewe aanze kumkaripia!, tena kwa kosa ambalo hajatenda!.
Turi bila kupoteza muda, akaamua kutoka nje na kuondoka kuelekea kwa mumewe Amani.
Baada ya Turi kuondoka, mama Vero akiwa na furaha tele huku akipeana mkono yeye na mwanaye Vero, akasema,
" yaani mwanangu!, Yule mtaalam ni kiboko, Yani hata lisaa halijafika, kitendo tu cha Turi kunywa maji , Yani kila kitu kimejipa looooh!, lazima nimpelekee kuku yule babu mweeeh!".
Vero naye akamjibu Mama yake, " daah !, mama we hatari, sasa yule Babu alikuonesha nani!?,
eti mpaka Amani anasema Bora angenichumbia mimi!, yaani siamini mama, mmmmmh!".
Mama Vero Akasema, " umeona sasa , ndo maana nilikuambia usijafanye huruma, wewe hujazaliwa naye tumbo moja yule,
wanaume wenyewe siku hizi wachache , huo wakati wa kuringa unautolea wapi!?, sasa hii ndo fursa yako usilembe".
ITAENDELEA...,
JE WAJUA kwamba unaweza kukamata sms za mwenza wako anazochart na watu wake na ukazisoma kupitia simu yako bila yeye kujua??
Kwa huduma hii ya sms tracking ncheki whatsapp 0710204647 nikuunge kwenye group letu
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi




Maoni