MR ARROGANT 14&15*
Hatimae Mchana ulipita, jioni ilipokaribia, Leon alimpigia Jasmine simu.
“Njoo ofisini kwangu kabla hujaondoka.”
" Sawa boss.
Baada ya sekunde chache Jasmine alifika ofisini kwa Leon alikaa kwenye kiti bila hata kuambiwa.
“Boss, umeniita?” aliuliza kwa tabasamu.
Leon alinyanyuka taratibu, akamfuata kwa hatua huku akiwa ameweka mikono yake mifukoni, akimtazama kwa macho ya moja kwa moja.
“Jasmine… nimechoka kupigana na moyo wangu Bata ka kufanya jambo la kufanya wote tuwe sawa.
Jasmine akashtuka kidogo alijua huenda ndio ikawa mwisho wa kazi yake.
Alisimama akamuangalia Leon usoni.
" Unataka kunifukuza kazi?
" kwani wewe unataka ni hilo litokee?
Jasmine alikuwa mpole ghafla alikaa kwenye kiti .
" Sijui ulikuwa mzaha au kisasi lakini katika haya yote tuliyopita pamoja kuna kitu nimezaliwa kwenye moyo wangu. Japokuwa unanionea sifai ,sina hadhi ila moyo wangu umetokea kuvutiwa sana na wewe nimejikuta nakupenda sana Leon.
Leon akimsikiliza kwa makini kisha akameza mate.
" Leon kisasi chako kwangu kinezaa upendo na kuna wakati hazina upendo wako kwangu ila wewe ni jeuri tu unajaribu kurudisha nyuma hisia zako . Ok labda kwasababu mimi ni secretary huwezi au tulikutana kwenye mazingira ya chuki na bado unajaribu kuibeba chuki juu yangu. Ila mimi bakuli kwako kuwa nakupenda japo kuwa sio rahisi kwa mwanamke kuzamia hivi mbele ya mwanaume ila acha mimi niseme lililo moyoni mwangu.
Leon aliendelea kukaa kimnya akimuangalia.
" Leon kama hili haliwezekani basi mimi nipo tayari kuaga haya mashindano.
Baada ya kumaliza kuongea kimnya kilitawala kwa muda Jasmine akaona kama anajichoresha alisimama na kutaka kutoka lakini Leon akamdaka mkono wake na kumvutia kwake Jasmine alijikuta yupo kifuani kwa Leon.
Leon alimshika kiuno na kumsogelea kwake zaidi
“Nasema nakupenda Jasmine,” Leon aliongea kwa sauti ya chini lakini kwa msisitizo.
“Nakupenda namna ambayo siwezi kueleza kwa maneno. Nimejaribu kukataa, nimejaribu kukimbia, lakini moyo wangu haunipi nafasi tena.
Jasmine moyo wake ulidunda kwa kasi, akajilaza kifuani kwa Leon huku machozi ya furaha yakitoka.
“Nilijua, Boss. Nilijua siku moja ungefika huku.
Leon akavuta pumzi nzito, akamshika mikono yake yote miwili. “Lakini kumbuka, mimi ni mkali, nina mipaka, na sitaki mchezo. Usije ukacheza na moyo wangu, Jasmine, kwa sababu hii siyo hadithi ya kawaida.
Jasmine akatabasamu kwa upole, akainua mikono yake na kugusa kidevu cha Leon. “Sichezi Boss… moyo wangu ni wako. Nilikuwa nasubiri siku hii kwa hamu kubwa sana.
Mara hii Leon hakujizuia tena. Alimbusu Jasmine kwa mapenzi makubwa, akafuta kila ukali wake na kumlaza kwenye kifua chake. “Basi kuanzia leo, wewe si secretary tu wewe ni mwanamke wangu, mwanamke wa maisha yangu . Ujeuri wako umejenga kitu kwenye moyo wangu nakupenda sana Jasmine.
" Nakupenda pia leon.
Ndani ya ofisi kulikuwa na ukimya wa mapenzi, moyo wa Leon na Jasmine ukigongana kwa mapigo ya aina moja. Safari ya kimapenzi ilianza rasmi, na safari hii Leon hakuwa tena “Mr. Arrogant” pekee alikuwa mwanaume aliyekubali moyo wake kutekwa na binti kiburi asiyekuwa na uwoga nae hata kidogo.
Siku hiyo ilikuwa ni mwanzo mzuri wa penzi lao jipya lililochipuka. Na mapenzi yao yalikuwa ya siri sana hakuna ambae alijua pale kazini .
Siku zilienda penzi lilipamba moto kuna wakati Leon alikuwa alitamani kumuona Jasmine alimpigia simu na kumuita ofisini kwake.
Jasmine alienda akamkuta akiwa kasimama mbele ya meza yake huku akiwa kuegemea meza na mikono yake ilikuwa kwenye mifuko ya Suruali. Jasmine aliingia akiwa na tabasamu.
" Nimefika Boss wangu. Aliongea huku akiwa anamuangalia Leon usoni.
Leon alimkagza kuanzia juu mpaka chini .
" Leo umependeza sana.
" Asante. Alijibu Jasmine huku akiangalia chini kwa aibu. Leon alitoa mikono mfukoni akapiga hatua mbili kumsogelea . Alimshika kiuno na kumvutia kwake.
" Sikujua kama na wewe huwa una aibu. Jasmine alicheka
" Umeanza uchokozi wako.
" Ni kweli tangia nimekufahamu sijawahi kuona ukiunganisha nacho chini kwa aibu.
" Basi hata mimi sikuwa nikiamini kama unaweza kuwa romantic hivi.
Leon akimvuta na kumkumbatia vizuri.
" Nimemiss busu lako.
" Leon hapa ni kazini na haya mambo tukisema mwisho pale getini.
" Ni kweli lakini nimeshindwa kujizuia na wala kazi haziendi. Please nipe busu kidogo.
Jasmine alijifanya anaona aibu kukubali lamba midomo yake. Hisia zilizidi kupanda Leon, aliinamisha kichwa chake na kukutanisha midomo yao leon akiinyonya ulimi wa Jasmine kwa ufundi mkubwa Jasmine alikuwa akitoa mifumo ya mbali.
Ghafla mlango ulifunguliwa na paul akataka ndani na kushuhudia kila kitu.
Full 1000
Whatsp 0784468229
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi










Maoni