*AFANDE NILEGEZEE KAMBA ππ«π«* Chapter 9 Elton alikuja jikoni pale nilipokuwa nimekaa, Akanikamata mkono wangu kwa nguvu, akaniambia kwa hasira
"We unataka kunius?"
Nikamuuliza "Kwani unamaanisha nini?"
"Hivi chakula gani kile ulichopika? Unataka tule tufe? Una akili kweli wewe?'
Nikajibu kwa upole, "Lakini nilijaribu kadri ya uwezo wangu. Ukweli... Sijui kupika"
Elton akashangaa "nini? We hujui kupika? Msichana mzima. kama wewe? Kazi yako ni kutapeli watu na
kuongea ovyo, lakini hata chakula rahisi hujui kupika? Kwanza uliniharibia nguo zangu, pili ukaharibu kahawa yangu, tatu ukaharibu chakula chetu, then umenivunjia wine yangu ya bel Unadhani nitaendelea kuvumilia mpaka lini?"
Alipiga meza kwa hasira kidogo akaendelea
kusema, "Mimi nimechoka. Nitakurudisha selo. Sitaki tena kukulipia hilo deni lako. Mkataba wote tuliokuwa nao, umeisha, Leo nakurudisha kituo cha polisi
Weeeh Niliposikia hivyo nusu nizimie
Nikagundua nimeharibu kweli. Nikaanza kumuomba msamaha, nikipiga magoti kabisa, lakini hakuongea kitu. Alichukua furiguo za gari, akamchukua Elijah wakatoka wote wawili
Walikwenda kula nje kwa sababu chakula nilichopika hakifai kuliwa. Walifika kwenye mgahawa mmoja, wakaagiza chakula. Elton bado alikuwa na hasira hakutulia kabisa. Elijah akamuuliza
"Bro, sasa niambie ukweli. Kuna nini kati yako na yule demu?"
Elton akaanza kumueleza kila kitu kuanzia siku tulivyokutana mpaka yote yaliyotokea. Alipomaliza, Elijah alianza kucheka vibaya mpaka Elton akammaindi
"unacheka? Hii si kitu ya kucheka"
"Yaani bro, demu alikuambia una kibamia eeh! Aiseee amekua na ujasiri wa kukwambia hivyo? Kawaida watu wote wanakuogopa
"Muulize nilichomfanya! Nilimikuna mpaka akaomba majiΕ Yani kila nikimuona lle kauli yake. ya kusema nina kibamia inanicheza kichwani.
Lengo langu ni kumyoosha mpaka anyooke lla kwa sasa nimechoka, bora nimrudishe nilipomtos
"Aaah bro, achana nayo bwana. Msamehe tu Unaona kabisa hajui hata mambo ya kawaida kama kupika. Sidhani kama anajua chochote yulee
"Kama hajui kupika nifanyeje? Unataka mimi nile nje kila siku? Hapana. Wakati mwingine nataka chakula cha nyumbani alilalamika Elton
"Basi urnfundishe"
Elton akacheka kidogo, "Sina muda wa kufundisha mtu. Kila siku niko kazini. Nikirudi
nyumbani nataka nipate chakula nishibe niende. kulala. Ndo sababu nyingine iliyo fanya nimchukue kama house girl"
"Acha uongo bwana. Hukumchukua kwa ajili ya kazi ya nyumbani peke yake. Ulitaka kumkomoa tu kwa maneno allyokuambia"
Elton akakubali, "Ndio, nilitaka kumlipiza kisasi -na nimeshafanya hivyo
"Basi kama umemlipizia, mpe nafasi nyingine. Na mimi nadhani huyo demu siyo tapeli. Angalia
mavazi yake, yanaonekana ya bel. Pia vile anavyoongea, ana sauti ya mtu aliyelelewa vizuri. Sidhani kama anatoka familia duni
"Usidanganywe na sura yake. Wanaigiza mpaka
unaamini Kama kweli anatoka familia nzuri, unadhani kwanini walimuacha selo bila kumtoa?
Alisema hana mtu wa kumlipia dhamana, ndiyo nikamsaidia. Bro usiruhusu akuingie kichwani
Elijah akasema "Sawa bro"
Wakati huo huo waiter akawaletea chakula. Wakala na kubaki huko hadi jioni.
Upande wangu mimi, nilikuwa nangoja warudi Nilihitaji kumuomba Elton asinirudishe selo. Nyumba yake ilikuwa bora mara elfu kuliko selo yenye mbu, sakafu chafu na harufu mbaya. Sikutaka kurudi kabisa.
Niliendelea kusubiri, hadi usiku wa manane niliposikia honi ya gari. Mlinzi akafungua geti,
Elton akaingia na gari lake. Kabla hata hajashuka nilikuwa kwenye mlango, nikapiga magoti, nikiomba msamaha. Lakini hakusema kitu, Alishuka kimya kimya, akaingia ndani
Elijah akaniangalia akasema kwa upole, "Haupaswi kupiga magoti. Hujafanya kubwa mbona
"Lazima nimwombe msamaha asinirudishe kituo cha polisi
Elijah akatabasamu kidogo, "Sidhani kama atakurudisha. We jitahidi tu kufanya mambo
vizuri Usijali
"Najaribu lakini kila nikifanya kitu naishia kuharibu tu. Na pia Sijui mambo mengi
"Usijali, nitakusaidia. Cha muhimu sasa, nenda ulale. Kesho anza upya"
"Asante sana"
"Ginah
Akauliza "Jina lako nani maana Elton anakuita tapeli?"
"Mimi ni Elijah. So Tutaonana kesho, byeee" Akaingia zake ndani na Nilirudi kwenye store nikalala Kabla sijalala, nikaweka alarm asubuhi niamke mapema.
Asubuhi sasa Nikaamka nikaaanza kusafisha nyumba. Wakati niko jikoni nikianza kuandaa kahawa ya Elton, Elijah alikuja
"Good morning Gina
Nikajibu "morning Elijah"
"Unapika nini?"
"Ninatengeneza black coffee ya Elton. Hawezi kuanza siku bila kunywa kahawa
"Lakini unajua kuipika vizuri?"
Nikashusha macho nikasema "Hapana, sijui"
"Sawa, siyo vibaya. Nitakufundisha
Nikashangaa, "Kweli?"
"Ndio"
Kwell Akanifundisha hatua kwa hatua. Nikafuata maelekezo yake. Mwishoni kahawa ikatoka bomba sanal Nilifurahi mpaka nikatamani kulla
"Sasa chukua hil kahawa, mpelekee Elton. Hapo
ndipo njia pekee ya kumuomba msamaha. Labda atakusamehe okay?" Alinammbia
Nikasema "Sawa"
Nikapeleka kahawa mezani nikisubiri Elton aje
kunywa. Baada ya mda Elton akaja, akaiona kahawa lakini hakuonyesha kama ana nia ya kunywa. Nikamwambia kwa upole
"Nimetengeneza kahawa yako"
"Naiona. Umeweka sukari tena? Au umeweka sumu ili ikolee vizuri??"
"Hapana, leo nimejitahidi kweli. Please jaribu
Elton alinyamaza kwa muda, akaangalia kile kikombe, akakinyanyua, akanywa kidogo. nikaona macho yake yamebadilikal Kahawal ilikuwa perfect kabisa
Akanitazama kisha akasema "Good job" Kisha akaondoka zake.
Kwa mara ya kwanza tangu tumefahamiana, Elton aliniambia neno zuri. Nilifurahi vibaya mno mpaka nika blush wapendwa
Je nini kitaendelea?
Nakuja
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi