FATE TO LOVE YOU π 12 MTUNZI UHURU MEDIA Stephen alisimama huku akitetemeka kwa hasira, macho yake yakiwaangaoia Jerry na Lina kwa chuki.
βJerryson, pesa zako hazitafanya umchukue Lina wangu. Nampenda, huyo ni mwanamke wangu! Stephen alijikuta akiongea kwa sauti ya ukali na kumfanya washirika na kuvunja kumbatio.
Jerry alikuwa amesimama kwa utulivu akimuangalia jinsi alivyo kuwa amepaniki , na Lina alikuwa akimuangalia kwa hasira.
βStephen sitaki fujo nyumbani kwangu.
" Jerry nilikuwa najiheshimu sana lakini hapa ulipofikia nimekushasha thamani.
" Haidhuru wewe kushusha thamani yangu . Alafu hizo kelele zinazopigwa ni kazi bure unakumbuka vizuri
wewe ndiye uliyepoteza nafasi kwa Lina, Ulimdhulumu na kumuumiza.
" Mambo yangu na Lina wala hayakuhusu.
" Yanamuhusu sana tu sababu maisha yangu kwa sasa yapo mikononi mwake.
Alisema lina kwa hasira .
Stephen aliangua kicheko cha dharau.
" Yani haumjui vizuri huyo ulie mkabidhi maisha yako , atakupa maumivu zaidi ya niliyokupa mimi.
Osca alipoona Stephen ameenda kufanya fujo alianza kumvuta ili waondoke.
" Kwahiyo ulitaka tumechukua ili uje kufanya fujo?
" Osca tulia hujui kile ninachopitia.
" Acha mambo yako bwana , naomba tuondoke.
" Miondoko hapa mpaka niongee na Lina.
Jerry alipiga hatua mbele kuwasogelea kisha akasema
βWewe huna akili kabisa. Endelea tu kubweka hapo kama mbwa koko ukichoka njia nyeupe utaondoka.
Jerry alimgeukia Lina na kumwambia.
Nenda chumbani kwako ukapumzike .
Jerry alimshika mkono wakapandisha pamoja kuelekea chumbani kwa lina.
" Stephen kumbuka huyu ni baba yangu mdogo. Haupaswi kujibishana nae hivyo. Alisema Osca
Stephen alimgeukia Osca kwa hasira na kumwambia
βUsiniingilie wewe Osca, hii kesi haikuhusi kabisa.
βStephen, naongea kwa mara ya mwisho. Ondoka kwa amani kabla Jerry hajatoka huko ndani.
Stephen aliondoka kwa hasira huku alimuacha Osca.
" Huyu jamaa chizi kweli yani nataka kuja hapa ili agombanie demu .
Lina alikaa kitandani huku akiwa kajiinamia, kwa kiasi flan alijihisi kuumia. na Jerry alikuwa kasimama pembeni yake.
" Lina hutakiwi kuumia kwaajili yake, hakuwa mwanaume sahihi kwako.
Lina alinyanyua uso wake kumuangalia.
" Najua kwao hawanitaki .
" Sio kwao tu hata yeye bado hajui msimamo wake uko wapi.
" Ni kweli
" Inawezekana ni kweli anakupenda lakini hastahili kuwa na mtu kama wewe.
Lina alimuangalia kwa jicho lenye maswali , ni kama alikuwa anahitaji maelezo zaidi.
" Unajua nini kuhusu Stephen?
Jerry aliona sio busara kusema mambo ya Stephen.
" Sikiliza Lina , wewe ndio mwenye maamuzi kwa sasa, kama utaanza kumpa moyo wako Stephen au kuachana nae na kusimama kwenye masomo ili kufikia malengo yako .
" Kusoma ndio swala la muhimu kwangu.
Jerry alipomaliza kuongea na ona alitoka chumbani .
Stephen walifika nyumbani kwao akiwa na hasira , kila aliemuongeleza aliishia kujibiwa vibaya kisha akaenda kujifungia chumbani kwake.
" Inawezekanaje Lina akaniumiza roho yangu kiasi hiki? Sikujua kama nampenda kiasi hiki .
Alichukua simu yake na kupiga namba ya lina.
Simu iliita , wakati huo Lina alikuwa akiangalia mwishowe aliamua kupokea ile simu.
" Unataka nini Stephen?
" Lina hivi ni kweli umeamua kuwa na mahusiano na Jerry?
" Kwani unaumia?
" Nipe jibu la swali langu.
" Acha kuteseka kijana , endelea na maisha yako sababu mimi nilishakusahau na wala sikumbuki kama tulikuwa na uhusiano mwingine tofauti ya mtoto wa boss wangu wa zamani.
" Lina unajua unauumiumza sana moyo wangu.....
" Acha utumie sababu huu ndio wakati wako wa kuumia kama mlivyoniumiza mimi.
" Nahisi kukupenda lina.
Lina aliangua kicheko kikubwa .
" Unasema unanipenda wakati wewe na familia yako mliniweka ndani?
" Alikuwa ni mama , hata hivyo kesho yake nilikuja polisi sikukukuta.
"Sikiliza Stephen nikwambie kitu kimoja muhimu sana kwako.
" Mimi siwezi kuwa na wewe wala Jerry sio mwanaume wangu ila ni mwanaume anayejua umuhimu wangu na kunipa thamani kubwa ambayo sikuwahi kupata hata kwa ndugu zangu wa karibu. Basi naomba usimsumbue kaka wa watu.
" Usijidanganye niliwakuta mmekumbatiana kama wapenzi.
" Sina muda wa kutaka kukuaminisha hicho ninachokwambia . Uwe na maisha mema.
Lina alimaliza kuongea kisha akakata simu.
Lakini kwa kiasi fulani Lina walikuwa anaumia sababu ni kweli alikuwa anampenda Stephen na ni mwanaume wake wa kwanza lakini hakuwa na jinsi ilimbidi akae mbali nae ili kuepusha matatizo. Pale pale alifuta namba za Stephen na kila kumbukumbu aliyokuwa nayo alijaribu kuipoteza. Alichukua baadhi ya vitu alivyopewa na Stephen na kwenda kutupa kwenye takataka.
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi