FATE TO LOVE YOU π 17 MTUNZI: UHURU MEDIA Maneno ya Jerry ni kama yalikuwa
Usiku uwe wa aina yake. Kila kitu kilionekana kuwa kimetulia, upepo ukipuliza kupitia madirisha makubwa ya chumba yaliyokuwa yameachwa wazi , baridi tamu iliyokuwa ikipenya ndani ya chumba cha Jerry.
Ndani mapenzi yalikuwa yamewaka moto. Jerry na Lina walikuwa wamechoka, lakini mioyo yao ilikuwa na furaha na hisia mpya ambazo hakuna mmoja kati yao aliyetaka zifutike.
Baada ya kimya kifupi, Lina alikuwa amejilaza kwenye kifua cha Jerry huku akipapasa kifua chake
βJerryβ¦aliita kwa sauti ya taratibu
βNdiyo mpenzi.
βNinaogopaβ¦
Jerry alishtuka kidogo, βKuogopa nini tena, baby?β
Lina alinyamaza sekunde chache, kisha akavuta pumzi ndefu.
βNajua unapenda, najua unanithaminiβ¦ ila kuna wakati nahisi labda hii ni ndoto na sio kweli.
" Kwanini baby uhusi hivyo?
" Hali yangu tofauti na yako labda ndugu zako, wazazi wanaweza kunikataa kutokana na mimi sijatoka kwenye familia yenye uwezo.
" πππ Jerry akicheka huku akikaa vizuri, Lina akinyanyua pale kifuani na kumuangalia usoni.
" Unacheka wakati mimi nipo serious.
Jerry alimshika uso kwa mikono yote miwili, akamuangalia kwa upendo wa dhati kabisa kutoka moyoni.
βLina, futa kabisa hayo mawazo potovu, Mimi siwezi kuondoka kwenye maisha yako , Nilikuona ukiwa kwenye giza, nikaamua kuwa nuru yako. Hata dunia ikinigeukia, ssitabadilisha chochote kutoka kwako. Na kuhusu familia yangu wanaelewa uwepo wako kwenye haya maisha yangu na wanatamani sana nikukutanishe nao ila mambo yangu yanabana sana , ila siku sio nyingi nitakufundisha na familia yangu uwafahamu nao wakufahamu vizuri
Lina alitabasamu huku akiona aibu, βUnanifanya nijisikie kama nipo kwenye filamu moja kali ya mapenzi.
βLabda kweli tupo kwenye filamu, ila tofauti ni kwamba hii ni ya kweli.Jerry alijibu huku akimbusu paji la uso.
Siku ziliendelea kupita...
Mahusiano yao yakazidi kuwa imara, lakini kama kawaida ya dunia furaha yao ilianza kuingiliwa na walimwengu wanye roho za kwanini.
Siku moja Lina alitoka kwenda kufanya manunuzi yake binafsi. Aliingia kwenye Mall moja kulikuwa na duka kubwa la nguo za bei ya gharama na zenye viwango vya hali ya juu huko walienda watu wenye pesa zao.
Akiwa anaendelea kuangalia Cheni mara alitokea mama yake Stephen na kusimama pembeni yake. Lina hakuwa amemziba akili yake ilikuwa kwenye zile Cheni.
" Samahani dada nitolee hii yenye kifani che kundu.
" Hiyo ni almasi nyekundu bei yake ipo juu sana sijui kama unaweza kumudu bei.
Ilikuwa sauti kutoka kwa mama Stephen, Lina aligeuka kumuangalia kisha akaachia tabasamu .
" Oooh msr Maxwell kumbe na wewe upo hapa?
" Ni kawaida yangu mimi kuja hapa sijui wewe mwenzangu ambae ndio kwanza umeanza na sijui kama unaelewa hapa hawajui mabati ila ni madini ya bei ghali.
" Najua , naelewa sana ndio maana nipo hapa nikiwa nimejipanga na ninaelewa kilichonileta . Alijibu Lina kwa kujiamini .
" Hivi napata wapi jeuri ya kujibishana na mimi?
" Kuna mtu mmoja muhimu sana ananipa kiburi na kujiamini.
" Unazungumzia Jerry si ndio?
" Jibu hilo piga mstari.
" Umewezaje kumraghai kijana wa watu mpaka ukajiweka kwake?
" Ni kama ilivyokuwa kwa mwanao Stephen
" Mfyuuuuuu mchawi mkubwa.
" Ni kweli nina uchawi wa kuwaumbua vijana wa kitajiri ili nichukue mali zao , kwako ilikuwa bahati uliwahi la sivyo ningekuwa wamiliki hati ya kile kijumba chenu.
" Kijumba?
" Mmmmm kijumba cha kawaida sana , yani haiingii kabisa kwenye lile kasri la mubaba wangu Jerry.
" Unajidanganya sana binti, kesho na kesho kutwa nitakupa barabarani ukiuza mboga mboga na matunda kwenye beseni.
" Duwa la kuku hilo mrs Maxwell. Kwa sasa tegemea kuona maendeleo yangu yani kila utakapoingia na mimi nipo kama hivi yani unafaa dhahabu na mimi na vaa, unavaa almasi na mimi mimi. Yani jino kwa jino.
Mama Stephen alimuangalia Lina kwa hasira huku akiwa kang'ata neno.
" Binti usijisahau haya maisha unayoishi ni ya muda mfupi tu siku sio nyingi utarudi ilikotoka.
" Umechelewa sana alafu teke ulilonioiga ndio limeniglfikisha hapa nilipo so hulaumu mwenyewe kwa roho mbaya yako.
" Sawa Lina tutaona.
" Na ikipania sana safari hii nitahakikisha unaumia vibaya mno yani zaidi ya hapa sababu nitahamia kwa mume wako Maxwell.
Mama Stephen alishikwa na hasira akataka kumvamia Lina alimuwahi akamsukuma mpaka akaanguka chini.
Mama Stephen alianza kulia kuwa kuamia mguu.
Walinzi na wafanyakazi pamoja na wateja wengine waliwazunguka.
" Huyu binti anataka kumuuwa jamani.
Watu waliokuwa karibu walitetea Lina na kusema mama Stephen ndio alianza ukorofi.
Lina akiacha hata kufanya manunuzi aliondoka pale dukani na kwenda kazini kwa Jerry.
" Vipi baby mbona ghafla bila taarifa, ulikuja kufumania? Jerry aliongea kama utani lakini Lina hakumzingatia alikaa kwenye kiti huku simu na pochi yake ndogo akiweka mezani.
" Vipi mpenzi upo sawa ?
Kabla Lina hajanyanyua mdomo kuongea simu yake iliita . Namba iliyoonekana kwenye kioo cha simu haikuwa na kina lakini Lina alikuwa ameshaanza ni namba ya Stephen. Lina aliangalia ilivyokuwa inaita.
" Baby pokea simu.jerry alisema
" Achana nae.
" Kwani ni nani?
" Stephen.
Jerry alimuangalia Lina huku akiwa amekunja uso kisha akachukua ile simu na kuipokea
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi