FATE TO LOVE YOU π1 1--2 Lina alikuwa binti wa miaka 20, mrembo mwenye haiba ya upole, macho makubwa yenye mashiko , yenye mvuto mfano wa mbaramwezi na tabasamu lililofanya uso wake ingawa kama nuru.
Lina alikuwa anaishi na shangazi yake mjini tangia alipokuwa maliza elimu yake ya msingi.
Kwakuwa alikuwa yatima shangazi yake alibeba jukumu la kumchukua kijijini na kuja kumsomesha .
Shangazi yake hakuwa na kazi ya maana alikuwa mfanyakazi wa ndani katika familia moja ya kitajiri ya bwana mmoja aliyetambulika kwa kina la Maxwell, tajiri aliemiliki jumba la kifahari lenye walinzi, bustani na magari ya kifahari.
Yeye na mke wake Maurine alikuwa na watoto wawili wa kiume, mkubwa alikuwa anaitwa Amor ambae alikuwa kazini na Stephen kijana wa mwisho aliyekuwa na umri kama wa Lina na ndio kwanza alikuwa amemaliza chuo na kurudi nyumbani kwao.
Stephen alikuwa kijana mtanashati, mwenye haiba ya kujiamini na macho ya kuvutia , mwili wa mkakamavu wa mazoezi.
Kila mwanamke aliemuona alivutiwa nae .
Sifa za Stephen zilifanya apendwe na wasichana na wengine walikuwa wazazi kwake na kumueleza hisia zako kuwa wanampenda.
Huyo ilisababisha Stephen kutembea na wasichana wengi sana na kuwaacha.
Baada ya Stephen kurudi chuo akakutana na Lina, safari hii lina alikuwa amenawiri sana .
Stephen alipomuona alianza akuvutiwa nae na kutamani kukutana nae sehemu iliyotumia ili kumuelezea hisia zake lakini haikuwa rahisi sababu kila alipokuwa lina na shangazi yake alikuwepo.
Siku moja Mida ya usiku Lina alikuwa jikoni akisafisha viombo, Stephen alitembea kwa kunyata na kwenda kusimama nyuma yake na mkono yake akazungusha kiunoni kwa Lina.
Lina alishituka na kugeuka haraka kuangalia ni nani aliemshika .
" Stephen unafanya nini?
" Nimekukumbatia , najisikia amani sana kufanya hivi.
" Hapana , ondoka bwana , niache tusije tukakuta.
" Ni nani atakuja huku saizi?
" Hiyo tabia yako mimi sipendi.
Aliongea lina huku akiwa na hofu na moyo wake ulikuwa unadunda kwa nguvu .
" Lina usijifanye mtoto hujui kile ninachomaanisha .
" Unamaanisha nini?
" Upendo , nakupenda Lina.
" Wewe ni boss wangu.
" Kwani Boss hana moyo wa kupenda?
Lina hakuwa na jibu la kumpa walikuwa wakiangaliana usoni huku akili zao zikiwa mbali, kila mtu aliwaza lake kichwani mwake . Lakini ghafla walishituka baada ya kusikia mtu akikohowa.
Waligeuka kuangalia mlangoni wakakutana macho kwa macho na bi Eliza shangazi yake Lina.
Lina akijisigeza nyuma haraka, Stephen alienda kuchukua chupa ya maji kwenye friji na kuondoka.
Bi Eliza alimsogelea Lina.
" Wewe nini kinaendelea hapa?
" Hakuna kitu shangazi.
" Hakuna kitu wakati nimeona ulikuwa umesogeleana na Stephen na akili zenu zilikuwa zimefika mbali sana . Vipi kama angewakuta mama yake au baba yake?
" Nisamehe shangazi.
" Huo mchezo sitaki kukuona upo hapa kwaajili ya kazi na sio kuja kutembea na watoto wa boss .
" Lakini sina uhusiano nae na ni yeye amenishitukiza akanishika.
" Akakushika wapi?
" Huku kiunoni lakini sikutaka nilikuwa namwambia aniachie .
" Wewe usije ukaniletea matatizo hapa.
" Sawa shangazi haitajirudia.
Stephen hakukoma mara kwa mara alikuwa akimfuatilia Lina, Lina alikuwa anamkwepa sana na kuna muda alikuwa akimuona karibu yake moyo wake ulikuwa uunadunda kwa kasi sana.
Siku moja Shangazi yake Lina alikuwa safarini kijijini. Usiku Lina alikuwa kwenye nyumba yao amekaa kitandani kwaajili ya kujiandaa kulala.
Ilipofika saa tano za usiku, akiwa amelala usingizi alihisi kama anaguswa miguuni kwake Alishtuka, akawasha taa haraka. Alikutana uso kwa uso wa Stephen akimuangalia huku akiwa anatabasamu.
βStephen!? Umeingiaje hapa?βaliuliza kwa mshangao na hofu kubwa maana alikuwa amefunga mlango wa sebleni.
Stephen alitabasamu kwa upole.
βNilipita dirishani, nilijua uko peke yako. Lina nimeshindwa kuzuia hisia zangu tena.
" Nataka kujua umeingiaje hapa ndani.
" Nimepita dirishani, dirisha la sebleni lipo wazi.
βLakini si sawa sijapenda ujue . alisema kwa sauti ya kujiamini japo mwili wake ulikuwa ukitetemeka.
Stephen alinyoosha mkono wake na kushika kiganja cha Lina
βNaelewa Sikutaka kukutisha ila hii ndio nafasi nzuri kwangu kuzungumza na wewe Lina , Nimekuja kusema ukweli wangu . Lina nimekupenda tangu zamani. Sio kwa kutamani bali kwa mapenzi yangu ya dhati kutoka moyoni mwangu.
Lina alimuangalia kwa tahadhali kisha akasema
βStephen moyo wangu haujajua bado unachotaka, mimi ni mwanamke ambae najiheshimu sana na sitaki mtu avunje heshima yangu.
βNitaheshimu hilo.
" Ninaamini vipi?
" Nitakuonyeaha kila dalili ya kuonyesha naoundena na kukuthamini.
Lakini kabla sijaondoka, naomba kitu kimoja.
Lina hakuwa na jibu alikuwa akimuangalia tu usoni.
"siyo kwa nguvu ni ombi tu.β
βKitu gani?β
βDakika moja ya kukaa kimya tukitazamana bila kusema neno. Ili nijue kama kweli moyo wangu hauko peke yake.
Lina aliangalia chini kwa aibu, Stephen alimnyanyua kidevu kwa kidole fumba chake.
Wakawa wanaangaliana.
Kulikuwa na ukimya wa hali ya juu Lina alijikaza sana kumuangalia sababu Stephen hakuna nafasi ya kuangalia pembeni.
Baada ya dakika tano Stephen alitabasamu, akapumua kwa nguvu na kusema
βAsante hiyo imetosha kuna kitu nimekiona kwako, nitakupa muda wa kufikiria na wala sita kulazimisha. Alisogea karibu na kumbusu Lina kwenye shavu.
" Uwe na usiku mwema malkia ukae nga'a mfano wa mbaramwezi
Baada ya hapo alinyanyuka akatokea dirishani alikoingilia kimya kimya akarudi kwenye jumba lake kubwa la kifahari, akimuacha Lina akifikiria usiku mzima juu ya kile kilichotokea.
FATE TO LOVE YOU π 2
MTUNZI UHURU MEDIA
Siku zilienda Lina akaanza kumuweka Stephen moyoni mwakle , hatimae penzi lilianza kukuwa taratibu.kila mara nyakati za usiku walikuwa wakikutana kwa siri sana. Hata kuna wakati walikuwa wakikutana nje ya nyumbani badae kila mmoja alirudi nyumbani kwa wakati wake.
Siku moja walikuwa wamesimama chini ya mti, kulikuwa na mwanga hafifu ambapo sio rahisi mtu kuwaona.
" Huwa napenda sana nipate muda mwingi wa kukaa na wewe mpenzi.
" Najua lakini si unajua nabanwa sana na kazi na mama yako alivyo mkali sasa.
" Usijali kadili siku zinavyoenda kila kitu kitakaa sawa. Na mama yangu atakuchukulia kama mkwe.
" Sio rahisi.
" Mimi ndio nimependa kwanini wao wa iingilie kwenye mapenzi yangu?
Maongezi yaliwanogea na kujisahau kabisa.
Mara lilisikika gari likiwa limesimama getini na mlinzi alifungua geti na gari iliwasha taa full na kukamilika pale walipokuwa wamesimama . Mama na baba yake Stephen waliwaona Lina akataka kukimbia lakini Stephen akamzuia.
" Stephen acha niende.
" Uende wapi?
" Wazazi wako wakinikuta hapa italetaa shida.
" Kila kitu niachie mimi nitamaliza .
Lina alisimama lakini alikuwa anaogopa sana.
Gari ilipoingia na kwenda kuegeshwa kwenye maegesho mama yake Stephen alishuka kwenye gari na kuwafuata.
" Mnafanya nini huku kwenye giza usiku huu?
" Tunapunga upepo.
" Upepo? Kwani ndani hakuna Ac? Wewe Lina kwenye nyumba yenu hakuna feni?
" Ipo madam.
" Mama sio kila siku feni, sijui AC hata huu upepo wa Mungu unafaa sana tu.
" Stephen hakujua vizuri sana , unamtongoza lina."Mama....
" Sitaki kusikia mama , sijui nini. Lina kaa mbali na Stephen sitaki kabisa uanzishe mahusiano nae maana likitokea la kutokea wala siwezi kupokea kama mkwe . Hiyo ni tahadhali nakupa.
Maneno ya mama Stephen yalikuwa kama mwiba iliochoka kwenye moyo wa Lina.
" Mama maneno gani hayo ya kumwambia mtu.
" Sitaki kuongea zaidi Lina ondoka nenda ndani kwenu.
Lina aliondoka haraka bila kugeuka nyuma , huku nyuma Stephen alikuwa akilalamika kwa kupeperushwa ndege wake.
" Stephen kina sio mwanamke wa hadhi yako kumbuka wewe ni msomi na unatoka kwenye familia inayoheshimika.
" Sasa hapo inaingilia aje na mahusiano?
" Siwezi kumkubali Lina kama mwanamke wako hilo liwekwe hapo akilini kwako.
Alisema na Stephen kisha akaondoka.
Kesho yake kulipokucha kitu cha kwanza mama Stephen alimfuata shangazi yake Lina.
" Eliza ongea na mtoto wako , mkanye akaembali na kijana wangu , akae mbali na Stephen.
" Kwani kuna nini madam?
" Wale watoto wapo kwenye mahusiano na mimi sitaki kusikia wala kuona Lina na Stephen wakiwa na uhusiano.
" Sawa madam, nitaongea nae.
" Kama hatakuwa muelewa unajua nini nitafanya.
" Naelewa madam.
Baada ya hapo mama Stephen aliondoka na
Eliza akimtafuta lina na alijaribu kumkanya sana na kumkumbusha baadhi ya matukio yaliyotokea kipindi cha nyuma.
" Lina nilikwambia acha kuwa na ukaribu na Stephen hukusikia ona sasa mama yake amekuja kunilalamikia. Unakumbuka kilichomkuta Mishely?
" Ndio.
" Basi jiandae na wewe, na ikitokea umefukuzwa utarudi kijijini.
Eliza alimkanya sana Lina lakini ilikuwa kazi bure mapenzi yake na Stephen na lina yalikuwa yakishamiri kwa siri sana.
Siku moja Stephen alimuomba lina waende kwenye sherehe ya kuzaliwa ya rafiki yake wa karibu .
Lina alikubali na kumuaga shangazi yake kuwa ataenda kumtembelea Mishely . ( Mishely alikuwa mfanyakazi mwenzao lakini aliishia kufukuzwa baada ya kugundulika ana mahusiano na Amor kaka yake Stephen)
Shangazi yake alimkubalia .
Jioni Lina alitangulia kutoka na kwenda kumsubiri Stephen huko mbele.
Baada ya muda Stephen alifika na gari yake akamchukua wakaenda kwenye nyumba moja ya ghorofa, waliingia kwenye lift mpaka walipofika ghorofa ya sita walielekea kwenye nyumba ya sherehe huku mambo yalikuwa ni moto , muziki mkubwa, watu waliingua na zawadi . Kulikuwa na vinywaji vya kila aina.
Stephen alimtambulisha Lina kwa marafiki zakekana mpenzi wake wapo waliomuangalia kwa dharau kutokana na jinsi alivyo vaa mavazi yake hayakuwa ya bei ghali kwa kiasi fulani walimuona kama mtu wa hali ya chini.
Stephen alimchukua akampeleka kukaa sehemu, alimtelekeza hapo na kuwa Bize na wenzake. Lina alikuwa kajikunyata huku akishangaa shangaa wadada ambao walikuwa wakijipitisha huku wakiwa wamevalia vinguo vifupi.
Kuna muda Stephen alimfuata Lina.
" Mpenzi naomba unisubiri hapa kuna mtu naenda kumuangalia hapo chini.
" Unaniacha hapa?
" Usiogope hii ni sehemu salama na sita Chelewa kurudi.
" Sawa.
Lina alikaa pale huku akiendelea kushangaa jinsi watu walivyokuwa wanasherekea na wengine walifanya vituko kwa ulevi.
Kuna muda Lina alihitaji kwenda chooni , alimfuata dada mmoja akamuuliza yule dada akamuelekeza.
Lina alienda chooni na kumaliza haja zake, wakati anarudi alishitukia kavutwa na kwenda kutulia kwenye kifua cha mwanaume ambae hakuwa anamfahamu.
" Wewe vipi mbona umenivuta?
Lina aliuliza lakini yule mwanaume hakujibu, ghafla alisogeza midomo yake na kumbusu Lina.
Lina alimsukuma na kujitoa kwake.
" Kichaa wewe. Alisema lina kwa hasira kisha akaondoka , yule mwanaume alikuwa kasimama akimuangalia mpaka alivyopotelea.
Lina alirudi kukaa huku akiwa anamsubiri Stephen. Alianza kuhisi upweke na kujisikia vibaya alihisi Stephen kamtelekeza pale. Alipoangalia pembeni alikutana macho na yule mwanaume alimvuta na kumbusu.
" Huyu mjinga anakuja kukaa huku na ananiangalia bila aibu.
Wakati huo Stephen alikuwa ametoka na mwanamke wake mwingine ambae wanaendana kiuchumi na ni mwanamke wa muda tangia walipokuwa chuo. Walikuwa kwenye moja ya hotel ya karibu wakifanya yao.
"Tasha wewe ndio mwanamke pekee ambae unafikisha moyo wangu yani hata nikiwa usingizini ukipiga simu na kunihitaji lazima nitakuja.
" Mmmh...
" Sasa mbona unaguna mpenzi?
" Sikuamini Stephen ulinitesa sana chuo kila siku nilikuwa na gombana na wasichana wenzangu sababu yako.
"Stephen wa sasa sio yule mvulana wa chuo. Sasa mimi ni mwanaume ninaejielewa.
Full 1000
Whatsp 0784468229
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi