FATE TO LOVE YOU π 14 MTUNZI UHURU MEDIA Kelsho yake muda ya saa nne asubuhi Jerry alikuwa amesimama kwenye dirisha la chumbani
" Kweli nampenda sioni haja ya kuficha hisia zangu .
Aliamua kutoka nje akamkuta Lina bado anatafuta mauwa.
Alitembea taratibu na kusimama nyuma yake wakati huo lina alikuwa akitaka kuchuma uwa la waridi, alikuwa na tahadhari sana asije akachomwa na mwiba.
" Naweza kukusaidia? Jerry aliuliza, lina akaacha kuchuma na kugeuka kumuangalia. Walipoangalia na usoni Jerry aliduwaa baada ya kuona Lina akiwa kajiremba kwa makeup, alikuwa amependeza sana kuliko siku zote ambazo amewahi kumuona . Lina aliona aibu .
" Nilikuwa najaribu tu.
" Haukuwa unajaribu bali umeweza, Umependeza sana . Lina alitoa tabasamu dogo lililobeba aibu.
" Nilijua umeenda kazini.
" Hapana leo nipo nyumbani ila badae nitatoka na nisingependa kutoka mwenyewe ningependa tutoke pamoja.
" Sawa.
" Tunaenda kwenye sherehe.
" Sherehe ya nini?
" Ni kupongezana tu, huko tutakutana wafanya biashara na familia zao sasa mimi sina wakaenda nae nikaona sio vibaya nikienda na wewe mrembo.
" Hahahaha....
" Mbona unacheka?
" Na kucheka wewe sababu unanipa sifa ambazo sistahili.
" Sikiliza Lina , wewe ni mwanamke mzuri sana . Kuanzia sura , muonekano nikimaanisha umbo na tabia. Imekamilika kila idara.
" Basi acha niseme asante kwa Mungu alienitunukia hivyo vyote.
Jerry akitabasamu na kuendelea kumuangalia.
Hatimae ilifika muda ya saa kumi jioni Lina alipelekwa saloon na dereva kwaajili ya kutengeneza nywele zake na kujiandaa kwaajili ya kuhudhuria hiyo sherehe.
Lina alihakikisha siku hiyo anapendeza sana , alikuwa ana mambo mawili ya kumfanya apendeze.
Kwanza ni kwaajili ya kumvutia sana Jerry ili zaidi kuchanganyikiwa juu yake na pili hakutaka kumuangusha alitaka aendane nae
Alipo maliza kujiandaa alisimama kwenye kioo kujikaza kama yupo sawa.
Wakati huo Jerry alikuwa amesimama sebleni akiangalia saa yake ya mkononi.
Mara akasikia visigino vya viatu , alinyanyua macho yake kuangalia , alimuona Lina akishika ngazi akiwa amevalia gauni lake la usiku, alikuwa amependeza mno. Jerry alikuwa kamtolea macho huku kila sekunde tabasamu likichanua usoni kwake.
Lina alifika karibu yake na kusimama mbele yake.
" Umependeza sana. Alisema Jerry huku akimuangalia usoni.
" Pia wewe umependeza.
" Aaaaaaa.... Kuna kitu Jeetu alitaka kuongea lakini mdomo ulikuwa mzito .
" Kuna tatizo?
"Hapana twende zetu.
Walitembea hatua zilizolingana kuelekea kwenye gari. Dereva alifungua mlango mlango wa mbele lakini Jerry alikataa kupanda huko.
" Nitakaa nyuma. Alisema Jerry kisha akamgeukia Lina
" Panda. Lina alipanda huku Jerry akimsaidia kushika gauni lake refu na kumuwekea vizuri kisha nae akapanda , dereva akafunga mlango na kupanda kwenye siti yake na kuwasha gari.
Walifika kwenye hoteli moja ya kifahari huko yalikuwa yakiongozwa na magari ya kifahari na watu wa hadhi ya juu, wafanya biashara wakubwa na familia zao.
Jerry alikutana na Nabir akiwa na mke wake.
" Niambie simba dume.
" Safi kama unavyoona.
" Kweli jambo safi. Alijibu Nabir huku akimuangalia Lina.
" Bila shaka huyu ndio Lina.
" Haujakosea. Lina huyu ni rafiki yangu kipenzi, urafiki wetu imezifanya tumekuwa kama ndugu anaitwa Nabir na huyu ni Nayna ni mke wake.
" Asante nimefurahi kuwafahamu.
" Poa sisi karibu sana.
" Asante.
Walienda kukaa sehemu , kumbe wakati wanapita walipishana na mama yake Stephen.
Mama Stephen hakuamini alichokiona .
" Haiwezekani . Aliangaza macho akamuona Stephen akiwa kasimama na vijana wenzie. Alimfuata na kumshika begani.
" Mama ...
" Hebu njoo. Walisomea pembeni kidogo.
" Nimemuona mtu kama Lina.
Stephen alishituka
" Lina yupo kwenye hii sherehe?
" Itakuwa ni yeye jamani , hebu twende ukamuangalie .
Walienda mpaka sehemu walipokuwa wamekaa wakina Lina Stephen aliangalia alihisi ni Lina lakini hakuwa na uhakika asilimia zote. Alizidi kumuangalia kwa makini alipomuona anatabasamu mashavuni alikuwa anabonyea moja kwa moja aliamini kuwa aliyekuwepo pale ni Lina. Mara akamuona Jerry akisogea na kumpa grass ya kinywaji.
Stephen alikunja uso wake kwa hasira.
" Vipi ni yeye? Mama yake aliuliza.
" Ndio ni yeye kwani una shida nae?
" Hapana nilikuwa nataka kujua kama ni yeye na kwanini yupo hapa.
" Ni mwanamke wa Jerry. Stephen alijibu kisha akaondoka na kumuacha mama yake kwenye mshangao.
" Inawezekana vipi kwani walikutana wapi na Jerry?
Mama Stephen alimuuliza mtoto wake lakini Stephen hakumjibu aliondoka na kumuacha mama yake alimuangalia Lina jinsi alivyo mawili na kupendeza .
Full 1000
Whatsp 0784468229
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi