FATE TO LOVE YOU π 7--8 7 MTUNZI UHURU MEDIA Lina alitoka nje akaenda kuchukua usafiri na kuelekea nyumbani kwa Mishely. " Wewe mbona umerudi mapema na mr Jovin anasema haujafika? Lina alikaa kwanza kwenye kochi.
" Ni kweli sijafika kuna mambo yaliingiliana.
Mishely alikunja uso wake.
" Unamaana gani kunijibu hivyo? Kwahiyo hayo mambo yako yaliyoingiliana yalikuwa muhimu sana kuliko hilo lililokupeleka?
" Mishely sijui nikwambiaje ili unielewe maana mimi mwenyewe hapa nilipo ni kama nimechanganyikiwa.
Nilienda mpaka kwenye chumba cha mr Jovin wakati nataka kugonga mlango alikuja mwanaume mwingine na kunipeleka kwenye chumba cha Jerryson yule billionea kijana ambae alipata tuzo mwezi uliopita na kuonyeshwa sana kwenye TV.
Mishely alikuwa ana muelewa vizuri sana Jerryson alitoa macho kwa mshangao.
" Unasemaje Lina? Unamaanisha ulienda kuonana na Double J?
" Ndio Nilichukulia nikaenda kuonana na Jerry....
" Mama weeeee.... Lina una bahati ndugu yangu yule jamaa ni mtu adhimu sana na kila msichana alie bahatika kuwa nae basi huyo anakuwana pesa ya kutosha. Niambie shoga yangu umepata kiasi gani.
"Sijafanya nae chochote.
" Unasemaje?
" Mishely nimeshindwa kabisa kufanya kazi uliyonipa , Jerry amenipa kiasi cha pesa pia ameniambia kama nataka kazi basi niseme atanipa. Na sio kufanya kazi ya kuburudisha wanaume ovyo.
" Sasa yule ni baba yako mpaka alipangiwa nini cha kufanya? Wewe angalia maisha yako yeye pale alipo ana pesa ya kutosha na bado anatafuta.
" Anataka nitafute kazi ya kufanya na inaonekana yupo tayari kunisaidia.
" Usiniambie kama umeamua kuchagua kufanya kazi kwa mtu.
" Naona bora nifanye kazi kuliko hii kazi ya kwenda kuhangaika na wanaume ambao siwajui.
Mishely alitingisha kichwa kama vile anansikitikia .
" Lina huwezi kufanikiwa kwa kufanya kazi za kuosha viombo na kumtumikia mtu kijinga . Chimbo nililokuonyesha ndio Chimbo la mafanikio ya haraka, kama unataka kuwa kama mimi basi sehemu ya kazi ni ile na mimi nitakupa connection za kuonana na watu wazito wasiokuwa na longolongo. sasa kazi kwako kuchagua mshahara wa mwisho wa mwezi tena kwa kulisotea au kuchagua kuingiza pesa kila siku tena ukiwa unapata starehe.
Alisema Mishely kisha akaondoka na kumuacha Lina alimuangalia.
Kesho yake asubuhi Lina aliamka mapema sana akakaa kitandani akiwa anatafakari jinsi atakavyotoboa kwenye haya maisha magumu yanayozunguka.
Akiwa katikati ya mawazo simu yake iliita , aliekuwa anapiga alikuwa shangazi yake.
" Asubuhi hii shangazi anapiga atakuwa ana shida gani? Aliuliza huku akiwa na wasiwasi.
Alipokea ile simu ilikujua.
" Hallow shangazi.
" Lina mwanangu upo salama kweli?
" Ndio shangazi , usiwe na wasiwasi na mimi bado sijakata tamaa natafuta kazi.
" Lina naomba turudi kijijini kwani hata mimi nimechoshwa na mambo ya hapa .
" Kivipi shangazi?
" Umri wangu umeenda , siwezi tena kuendelea kufanya kazi ya kupika bila uwepo wako. Wewe Ulikuwa msaada mkubwa sana kwangu
" Ni hilo tu shangazi yangu?
" Ndio kipenzi.
Lina hakuamini sababu ya shangazi yake alihisi huenda kuna jambo linaendelea kwenye familia ya Maxwell.
" Subiri kwanza shangazi nitakupigia simu badae kidogo.
" Sawa.
Lina alikata simu kisha akanyanyuka pale kitandani na kumfuata Mishely chumbani kwake.
" Mishely kuna jambo naomba tuongee.
" Kuna tatizo lingine?
" Mishely , shangazi amenipigia simu anataka kuacha kazi na kuondoka kwenye jumba la Maxwell .
" Mmmmh kumekucha tena , sasa unataka shangazi yako nae aje hapa nyumbani kwangu?
Lina alimuangalia Mishely usoni kwake akawa amegundua Mishely hataki mizigo nyumbani kwake hivyo anatakiwa kujiongeza .
" Sikiliza Lina hapa ni mjini , maisha ni magumu sana mimi sitaweza kuwalea wewe na shangazi vyako.
" Naelewa ila nilikuwa nahitaji ushauri wako tu.
" Nitakushauri nini wakati wewe mwenyewe hutaki kazi ya pesa ya haraka unachofikiria wewe ni kutumikishwa ovyo kama punda
Lina alinyanyuka taratibu na kutoka nje ya chumba cha Mishely, alienda kukaa kwenye chumba chake ,alijiinamia na kufikiria nini cha kufanya.
" Shangazi yangu atakuwa anapitia wakati mgumu lazima nikamtoe kwenye ile nyumba.
Lina alinyanyuka na kwenda kuoga, alipomaliza alivaa nguo zake na kutoka .
Alienda mpaka kwenye jumba la kifahari la Maxwell . Alipoingia ndani ya geti mbele alimuona Stephen akiwa anafungua mlango wa gari lake , lakini alipomuona Lina alisimama na kuvua miwani yake myeusi aliyokuwa ameivaa na kumuangalia vizuri.
Lina alitaka kumpita kama vile hajamuona Stephen akamuita.
" Lina....
Lina aligeuka kumuangalia , Stephen alipiga hatua kumfuata.
" Wewe si uliondoka sasa umefuata nini nyumbani kwetu?
" Ni kweli niliondoka lakini kuna mtu wangu wa karibu nilimuacha hapa.
" Kwanini usimchukue huyo shangazi yako ukaondoka nae ili tujue una maamuzi magumu?
Lina alimuangalia kisha akatabasamu kidogo.
" Tafadhali niache sina mood ya kirumbana na wewe. Lina alitaka kuondoka , Stephen alimshika mkono na kumvutia kwake.
" Niachie ... Lina alimwambia huku wakiwa wanaangaliana usoni.
" Sikuachi mpaka uniambie ulikuwa wapi?
" Unaniuliza kama nani?
" Mwanaume wa kwanza wa maisha yako, niliekutoa ushamba na kumuonyesha mapenzi ni nini.
Lina alijikuta kwa nguvu kisha akafyonza na kuondoka. Alimfuata shangazi yake ndani akamkuta anafuta makabati ya jikoni.
" Shikamoo shangazi
" Lina, marahaba ...
" Shangazi naomba ujiandae tuondoke.
" Mbona ghafla sana , ungenipigia simu ili niweze kuaga.
" Unataka kumuaga nani hawa watu wenyewe hawana shukurani, wanarithi mbaya zisizokuwa na chembe ya utu hata kidogo.
Kumbe wakati Lina anaongea mama yake Stephen aliwasikia .
" Mtoto huna adabu wewe , yani unatusema vibaya ndani ya nyumba yetu wenyewe. Kwanza nini kimekurudisha hapa wakati uliondoka bila kuaga?
" Nimekuja kumchukua shangazi yangu.
" Afadhali mchukue uondoke nae tumeshawa choka na hekaheka kwanza mtu mwenyewe kashajizeekea .
" Kumbuka mlikuwa mnategemea kwenye kuwapikia.
" Sisi tunapenda binti tunaweza kuagiza chakula hotelini au tukaajili mfanyakazi mwingine tena akiwasomea maswala ya mapishi.
" Hiyo ndio shukurani yenu baada ya kuwatumikia kwa muda wote wa miaka 17?
" Kwani alikuwa halipewi, alikuwa anafanya kazi ya msaada?
" Huna haya wewe mwanamke. Lina aliongea kwa hasira , mama Stephen akampiga kibao cha shavuni.
FATE TO LOVE YOU π 8
MTUNZI UHURU MEDIA
Lina alishuka shavu lake na kumuangalia kwa hasira .
" Maurine chunga mipaka yako mara nyingine sitaweza kuvumilia .
" Lina acha , twende tuondoke. Alisema shangazi yake Lina ili kuepusha mzozo.
" Nilikuwa sahihi sana kukataa kuwa karibu na kijana wangu huna adabu hata kidogo ndani ya nyumba yangu mwenyewe unanitisha na kuniita jina langu kwa dharau. Kumbuka naweza kufanya chochote na usifanye chochote mjinga mmoja wewe. Ulitoka kijijini ukiwa unanuka vumbi na harufu ya moshi nikakupa sabuni nzuri na marashi sasa umekuwa na jeuri ya kunijibu na kuita jina langu kama tunalingana.
Shangazi yake Lina alipoona hali inazidi kuwa mbaya alimshika lina mkono na kutoka nae nje.
" Lina mlasani shetani tuondoke hapa kwa usalama .
" Shangazi kachukue nguo zako haraka tuondoke.
Walifika kwenye ili nyumba aliyokuwa akiishi shangazi yake Lina na kuanza kukusanya kila kitu chako.
" Tukitoka hapa tunaenda kwa Mishely?
" Hapana tunaenda hotelini kwanza baada ya hapo tutajua .
" Muda bado unaruhusu kwanini i tusirudi kijijini?
" Siwezi tena maisha ya kijijini nitapambana hapa hapa mjini.
Waliendelea kukusanya vitu vyao na kuweka kwenye mabegi .
Wakati wanatoka walimkuta Stephen kasimama mbele ya mlango. Lina alimuangalia alafu akataka kuondoka.
" Lina nataka kuongea na wewe.
" Sina muda tafadhali.
Alijibu lina kisha akapiga hatua kuondoka , Stephen alimfuata na kumshika mkono.
" Bado sijamaliza na na wewe. Alisema Stephen kwa sauti ya ukali kidogo.
" Stephen nakuomba niachie lina usije ukasababisha maneno yasiyo na lazima. Aliongea shangazi yake Lina kwa upole.
" Eliza wewe tangulia nina maongezi kidogo na Lina , atakuja muda sio mrefu.
Eliza alimuangalia Lina usoni.
" Naomba dakika chache shangazi.
" Usikawie .
" Sawa
Baada ya shangazi yake kufika mbele kidogo Lina alimgeukia Stephen.
" Unataka nini?
" Kwanini uliondoka bila kuaga? Nakupigia simu hupokei?
" Kwani kuna kitu ambacho haujamaliza kwangu? Unataka uendelee kunitumia huku ukiwa na malengo na mwanamke mwingine?
" Lina kuna mambo ambayo wewe hujui ....
" Na wala sitaki kuyajua , ni bora uendelee na huyo mwanamke wa hadhi yako ambae ilimtambulisha kwa mama yako.
" Upo ndani ya moyo wangu.
Lina alifyonza kisha akaanza kuondoka.
Stephen alimvuta bado alikuwa anataka waongee.
Mara mama yake Stephen akatoka ndani na kuwaona.
" Wewe binti mjinga bado upo ? Ondoka nyumbani kwangu.
" Stephen sitaki kugombana na mama yako hebu niachie.
Stephen bado alimng'ang'ania, wakivutana mpaka kiatu cha Lina kukatika.
Katika kujitetea lina alivua kiatu chake na kumpiga Stephen kwenye paji la uso.
Stephen alipasuka kwenye paji la uso na damu zikaanza kutoka.
Lina alishituka kuona damu, Stephen aliushika kwenye jeraha lake wakati huo mama yake alikuwa amepaniki.
" Umemuumiza mtoto wangu. Stephen nilikwambia kaa mbali na huyu mjinga ona sasa kakutoa damu.
" Ni bahati mbaya Stephen sikutarajia kufanya hivi. Lina alijaribu kujitetea lakini mama Stephen hakumuelewa aliingia ndani na kupiga simu polisi , alitoa taarifa ya kuvamiwa na mwanae kujeruhiwa
Shangazi yake Lina alikuwa na wasiwasi sana alimuomba sana mama Stephen asifanye hivyo.
" Nakuomba madam usifanye hivyo nipo tayari kufanya chochote lakini kitu chochote kisimpate Lina wangu.
" Huyu binti ni jeuri sana sasa ngoja aione nguvu yangu akakae ndani akitoka huko awe na heshima tena aogope hata kunisogelea.
" Watu wanataka heshima na sio kuogopewa Maurine.
" Madam sikuwa na nia ya kumuumiza ilikuwa bahati mbaya.
Lina na shangazi yake waliomba sana msamaha lakini hawakusikilizwa.
Mama Stephen alimchukua Stephen akamuingiza ndani . Huku akiwa ametoa maagizo geti lisifunguliwe.
"Nilikwambia Lina ona sasa kinachotukuta .
" Shangazi unajua sikuwa na nia mbaya .
" Nilikuwa hasira kukuacha uongee nae tungeondoka haya yasingetokea.
Lina aliona hata wakilaumiana na kulia haitasaidia aneshsingia matatizoni. Alifungua pochi yake na kutoa zile pesa alizopewa na Jerry.
" Shangazi shika hizi pesa uondoke ukasnze maisha huko kijijini.
" Siwezi kuondoka bila wewe.
" Hakuna njia ya kuepuka hili labda Mungu aingilie kati . Kama nikimaliza kifungo changu nitakuja kijijini.
Wakiwa bado wanaongea mara geti likifunguliwa wakaingia polisi wawili , wakike na wakiume.
" Lina.... Shangazi aliita .
Lina akafutwa machozi kwa ujasiri.
" Ondoka shangazi hili nizmtakabiliaba nalo mwenyewe.
Mama Stephen alitoka ndani na kumwambia polisi.
" Huyu binti kunifanyia fujo sana na kumjeruhi kijana wangu.
Polisi walimchukua lina bila kuongea chochote na kumpeleka kituoni.
Shangazi yake aliondoka na kwenda kutafuta gesti za mtaani za bei poa ili kufuatilia hatma ya Lina japokuwa hakuwa na matumaini kama wanaweza kushinda kutokana na umaarufu wa familia ya Stephen.
Lina alikuwa rumande akiwa amejikunyata huku akilia. Alijitoa mno kuingia kwenye mahusiano na Stephen .
" Sijui akili yangu ilifungwa na nini laiti ningejua ningemsikiliza shangazi haya yote yasingetokea.
Lina alikaa rumande masaa mawili . Baada ya hapo alikuja askari wa kike na kufungua mlango.
" Lina nifuate.
Lina alinyanyuka na kuanza kumfuata yule askari mpaka kaunta , alimkuta mwanaume mmoja aliekuwa kavalia nadhifu sana.
" Habari Lina!
" Salama.
" Naitwa Angelo ni mwanasheria nipo hapa kwaajili yako na utatoka kwa dhamana.
Lina alimuangalia mara mbili mbili huyo mwanasheria alitamani kuuliza maswali lakini akaona achukue kwanza vitu vyake watoke pale ndani ya kituo.
Baada ya kupatiwa kila kitu chake alitoka nje .
" Pole sana.
" Asante. Samahani wewe ni nani na umeanza je kuja kunitoa hapa ikiwa mimi sikufahamu?
Full 1000
Whatsp 0784468229
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi