Ingia

Sema Jambo 2025

Unsplashb
750+ Trending Pictures | Download Free Images on gonga94
  gonga94 official track

๐ฟ๐‘œ๐‘ฃ๐‘’๐‘†๐‘ก๐‘œ๐‘Ÿ๐‘ฆ.....: ๐‹๐€๐’๐“ ๐๐Ž๐‘๐ ๐๐€ ๐๐ˆ๐Š๐ˆ๐‘๐€ ๐˜๐€ ๐‡๐Ž๐”๐’๐„ ๐†๐ˆ๐‘๐‹ (๐™Ž๐™๐™–๐™ฃ๐™œ๐™– ๐™†๐™ž๐™ช๐™ฃ๐™ค๐™ฃ๐™ž) ๐‘ฉ๐’–๐’“๐’–๐’…๐’‚๐’ ๐‘บ๐’Š๐’Ž๐’–๐’๐’Š๐’›๐’Š SEHEMU YA 07

27th Aug, 2025 Views 73


Kiukweli kwa hali halisi ya maisha ni kwamba watu ambao maisha yao ni duni wanaogopaga sana kutoka na watu ambao wana maisha mazuri, hii ni kwa sababu ya kushindwa kulinganisha hadhi, hivyo basi Nasma alivyokuwa anawaza kuhusu kija Raymond aliona kama vile anapoteza muda wake.

Ray alimaliza kupiga mswaki akaenda chumbani na kuchukua taulo halafu akazama bafuni akioga โ€œMh yaani Rose atahisi nimesusa jamani wakati ninampenda sanaโ€ aliwaza akiwa bafuni anajipaka sabuni taratibu. Maana tangu jana usiku alikuwa hajamtakia hali mpenzi wake wa jijini Dar aitwaye Rose.

Ray alioga haraka haraka na kuweza kurudi chumbani, muda huo bado mama yake alikuwa amelala, ila mzee alikuwa akichunga mbuzi wake mitaa ya jirani kidogo kutoka pale nyumbani.

Ray alitoka nje akiwa ananukia, hasa, halafu akasimama mlangoni na kumuangalia binti aliyekuwa anamalizia kufagia uwanja โ€œHeeeh kakaโ€ Nasma alianza mazoea

โ€œNiniโ€ aliuliza Ray

โ€œUnaoga kila saa?โ€ alimuuliza

โ€œKawaida, nimezoea, kule Dar kulivyo na joto lazima mtu uoge mara 3 mpaka 4 kwa sikuโ€

โ€œMungu wangu ni nyingi sanaโ€ alisema Nasma

โ€œVipi wewe umeoga kweli tangu jana, maana nguo zilikuwa hizo hizoโ€ Ray aliuliza

โ€œHamna, nimeoga, sema tu, nguo mimi ninazo mbili tu, hii ya kufanyia kazi, ila nikishaoga navaa hiyo nyingine nzuri nzuriโ€

โ€œMungu wangu, nguo mbili? Unalipwaga mshahara?โ€ alimuuliza

โ€œNalipwa, ila hivyo nyumbani kuna maisha magumu, mimi ndo mtoto ninayetegemewa na wazazi mshahara wangu huwa unatumwa kwao woteโ€

โ€œpole sanaโ€ alisema Ray binti akatikisa kichwa na kuinama kuendelea kufagia uwanja wake โ€œUtaratibu wa chai vipi?โ€ aliuliza Ray

โ€œngoja namalizia usafi halafu nitatengenezaโ€ alisema binti

โ€œvitafunwa je?โ€ aliuliza

โ€œKuna kiporo cha makandeโ€

โ€œHahahaaaโ€ฆ..kwa huu mjengo nilijua maisha yamebadilika lakini kumbe wapi, embu niacheni kidogo bwana mimi ngoja nikalete vitafunwa nje huko.โ€ Alisema Ray na kurudi ndani akachukua pochi pamoja na simu yake akatoka nayo mpaka njiani.

Alitembea tembea, kutafuta sehemu yakununulia chapati au vitafunwa vingine vitramu vitramu, akaona kama vile pale kijijini hakuna, ndipo akaanza kuelekea katika duka moja kununua mkate. Kabla hajafika akasikia sauti

โ€œWe, Raymondโ€ ilitokea sauti nyuma yake, akatazama, ni Elinami pamoja na Doto walikuwa na mizigo ya majani wanapeleka nyumbani.

โ€œNaaamโ€ aliitika na kusimama kuwasubiri mpaka wakafika pale

โ€œHeh, ni wewe unanukia barabara nzima jamani?โ€ Elinami alianza kumpamba lakini Ray alimtazama kwa aibu kidogo

โ€œkawaida mbona?โ€ alisema Ray na kumgeukia Doto aliyekuwa pembeni mwa Elinami

โ€œShikamooโ€ alisema Doto huku akimkagua kuanzia juu mpaka chini

โ€œMarahaba wewe ni yupi tena?โ€ aliuliza

โ€œDotoโ€ alisema binti

โ€œDoto yupiโ€ฆ.wale niliwaacha vidonchi juzi juzi wa kwa mama Saumu?โ€ aliuliza

โ€œndioโ€

โ€œDuuuh mnakuwa sanaโ€ alisema na kumgeukia Elinami โ€œVipi natafuta sehemu wanayouza chapati chapati ntapata kweli humu kijijini?โ€ aliuliza

โ€œDah, ni mbali, karibia na sokoni muleโ€ฆ.ina maana umeshasahau mitaa hii miaka michache tu mhโ€ alimuuliza binti

โ€œHamna, maisha yamebadilika, mimi kipindi natoka huku kulikuwa hamna maendeleo hivi, nyumba kama hizi hapa, zote hazikuwepoโ€ alisema akizungusha mikono angani kuonyesha nyumba zilizokuwa zimejaa maeneo yale

โ€œNdo hivyo lakini, wewe nyoosha na hii barabara, utapaona kumechangamka kidogo kuna kabango kameandika Rukia Foodโ€ alisema Elinami

โ€œOk powa asanteโ€ Ray alisema, ndipo Elinami akamkonyeza kwa style fulani kwamba watawasiliana kwenye simu, halafu jamaa aliondoka zake akiwa anatabasamu.

Alimtext Rose, Good morning babeโ€ alitum text kwa furaha lakini kwa bahati mbaya Rose hakujibu kabisa ile message akajua labda yuko bize na kazi yeye akaendelea na mishe zake

Kweli alifikia maeneo fulani akaona bango dogo limeandikwa Rukia Food, akatazama, akamuona mama mmoja mweusi mweusi akisukuma chapati

โ€œShikamooโ€ alisilimia ikabidi yule mama atabasamu bila kuitikia salamu yake โ€œVipi mbona unatabasamuโ€ aliuliza

โ€œHahaaaโ€ฆ..hivi Ray, wewe ni wa kunipa shikamoo mimi?โ€ mama yule alimfahamu

โ€œmhโ€ฆ..mbona sijaelewa hapo kumbe najulikanaโ€

โ€œEmbu kwenda bwana,โ€ฆ.yani mkishatoka mjini ndo zenu, mnasalimia hadi wadogo zenu, au kisa tumezeeshwa na maisha sisi?โ€ aliuliza

โ€œMmmmh hapana, sister sorry sijakujua fulani hiviโ€

โ€œHumkumbuki dada mkuu wako ee?โ€ aliuliza huku akimkazia macho, ndipo Ray akakumbuka na kucheka

โ€œHahahaaaaaaโ€ฆโ€ฆSawa bana, jina la Rukia likanichanganya kumbe Mwanaidiโ€ฆok sorry sana nimezeeka mpaka kumbukumbu zimeenda mbali

โ€œAchana na mimiโ€ alisema huyo dada kwa jeuri, halafu akainuka โ€œEmbu nipe zawadi yangu kutoka huko mjini, au ndo umemletea mama yako peke yakeโ€ alisema mwanamke yule

โ€œHamna cha zawadi wala nini, sikia, nifungie chapati 3 mara 4, nikale raha mimiโ€ alisema Ray

โ€œMh yaani chapati kumi na mbili?โ€ aliuliza mwanaidi

โ€œYaaapโ€ Ray alisema na kutoa noti ya 5000 kwenye pochi akamkabidhi, na yule dada alifanya hivyo โ€œShilingi ngapi inakuwaโ€ aliuliza

โ€œ3600โ€ alisema huyo dada maana chapati moja ilikuwa sh 300 tu

โ€œOk iliyobaki kunywa sodaโ€

โ€œHayo ndo maneno, lakini kabla ya yote uoeeโ€ alisema mama huyo

Wote walibaki wakicheka huku akizidi kumuwekea chapati kwenye gazet. Akiwa anasubiri chapati pale ziwekwe vizuri, Doto alitokea akikimbia na kusimama pale, akamtazama Ray na kumuongelesha kwa sauti ndogo โ€œUnisubiriโ€ alisema hivyo ili muuzaji asielewe kinachoendelea

Hata hivyo mwanamke huyo alimaliza akamuwekea vizuri na kumkabidhi Ray, wakaagana Ray aliondoka kwa mwendo wa taratibu huku akimsubiri Doto taratibu alikuwa anataka asikie kwamba ataambiwa nini

โ€œDoto leo umekujua huku?โ€aliuliza

โ€œNdio,naomba unipe chapati mbili haraka ninawahiโ€ alisema Doto

โ€œsasa mbona kuna moja tu imebaki hizo zingine ni za kusubiriโ€ alisema mwanaidi

โ€œBasi nipe hiyo hiyo, inatoshaโ€ aliongea kama vile ni mtu anawahi sana, kumbe alichokuwa anawahi ni kwenda kuongea na Ray.

๐ฟ๐‘œ๐‘ฃ๐‘’๐‘†๐‘ก๐‘œ๐‘Ÿ๐‘ฆ.....: ๐‹๐€๐’๐“ ๐๐Ž๐‘๐ ๐๐€ ๐๐ˆ๐Š๐ˆ๐‘๐€ ๐˜๐€ ๐‡๐Ž๐”๐’๐„ ๐†๐ˆ๐‘๐‹
(๐™Ž๐™๐™–๐™ฃ๐™œ๐™– ๐™†๐™ž๐™ช๐™ฃ๐™ค๐™ฃ๐™ž)
๐‘ฉ๐’–๐’“๐’–๐’…๐’‚๐’ ๐‘บ๐’Š๐’Ž๐’–๐’๐’Š๐’›๐’Š
SEHEMU YA 08

Alipatiwa chapati moja na kuondoka akikimbia akamuwahi Ray, huku akicheka na kuhema sana

โ€œWe kaka, shikamooโ€ alimuamkia

โ€œKila saa??โ€ Ray aliuliza

โ€œHamna jamaniโ€ฆsi lazima nikuamkie kila saa kukuheshimu au hupendi?โ€ aliuliza

โ€œOk marahaba, shule vipi?โ€ Ray alijifanya kukaza asijeonekana mrahisi

โ€œShule nzuri, naona umeamua kuja kututembelea huku kijijiniโ€ alisema

โ€œHahaaโ€ฆ.nimekimbia maisha magumu Dar weweโ€ alisema Ray
โ€œMmmh muongo, maisha magumu upendeze hivi?โ€ aliuliza dotto

Ray alicheka kisha akamuambia โ€œBy the way sitakaa sana, nitaondoka siku sio nyingiโ€

โ€œUnawahi nini? Au ndo wifi? Eeh naona, ila sawa kweli hawezi kuwa wifiโ€ alisema mtoto huyo aliyekuwa na uchangamfu uliozidi kipimo

โ€œKwanini asiwe wifi?โ€ Ray aliuliza

โ€œHahaa.. wanaume wa Dar hizo mambo mh, kwani mnakuwaga nazo?โ€ alimuuliza ikabidi Ray asimame na kumshangaa kidogo

โ€œHiv wewe ni Doto au nakufananisha, mbona unaongea sana?โ€ alimuuliza โ€œMtoto wa juzi una maneno mengi hivi, kwanza wewe una miaka mingapi?โ€ aliuliza

โ€œkumi na sabaโ€

โ€œKumi na saba ndo uongee hivyo?โ€ embu acha mambo yako, nambie kwanza mambo mazuri mazuri

โ€œMazuri ni yapi kaka? Embu kwanza, kwani hayo niliyoongea sio mazuri? Mbona jamani watu wanayangโ€™angโ€™ania wanasema ni matramuโ€

โ€œShitโ€ฆโ€ฆโ€ฆ. Dotoโ€ฆ.kimbia uende nyumbaniโ€ alisema Rayโ€

โ€œHaya sawa, basi nipe namba yako kakaโ€

โ€œElinami anayo kamuombeโ€ alisema Ray

โ€œPoa byeโ€
Binti alianza kukimbia mpaka akaenda nyumbani kwa Elinami huku akiwa ameificha chapati ili Elinami asishtuke kwamba alimfukuzia Raymond kule kibandani.

โ€œEliiiโ€ alimuita mwenzake

โ€œNini dogo?โ€ alimwambia kwa kejeli

โ€œUna message unisaidie nimtumie mtu?โ€ aliuliza binti

Elinami alitoka na simu mkononi kisha akampatia binti mkononi โ€œzipo chacheโ€ alisema na kuingia ndani kwake alikuwa anafanya fanya usafi kidogo

Kumbe ili ilikuwa ni gia ya binti kuiba namba ya Ray alitaka anagalao aibe namba ya Ray kwenye simu ya Elinami, hata hivyo bahati kama bahati ni kwamba Elinami alikuwa amesevu namba ya Ray hivyo hivyo kwa jina la Ray hivyo basi haikumpa taabu kuipata na kuiiba akaweka kwenye kisimu chake kidogo lakini kalikuwa ka-smartphone ka Samsung ambako ni version ya zamani halafu akamuita Elinami

โ€œShogaaaโ€ alimuita โ€œMi naenda kufua simu yako niweke hapa?โ€ alimuambia

โ€œNyooo, uweke simu yangu hapo? Je wakiibaโ€ alisema mtoto wa kike huku akitoka ndani na kuipokea simu yake

โ€œAsante eeโ€ alisema Doto halafu akakimbia kuelekea nyumbani alipofika nyumbani hivi alikunywa kwanza chai na ile chapati yake

*
Upande wa Ray yeye muda huo alikuwa yuko mezani anakunywa chai na mama yake baba bado alikuwa anachungua mbuzi na kondoo wake, Ray alikula chapati mbili halafu akawa hoi na kuachana nazo halafu akatoka nje ya nyumba akamkuta Nasma akiwa ameketi kwenye ndoo akabaki anamshangaa

โ€œHivi wewe mbona hauna raha muda wote?โ€ alimuuliza

โ€œSamahani kaka, ndo hivi nilivyo mimi nina raha sanaโ€

โ€œHaya kale chapati huko ndani halafu leo kwani una kazi ngumu sana?โ€ alimuuliza

โ€œhapana ninafua nguo za baba na mama, halafu nitapikaโ€ alimuambia

โ€œOk basi, wewe nenda kanywe chai pale kuna chapati, ukishamaliza oga vizuri nikuone na nguo nyingine hiyo ni chafu sanaโ€ aliongea akimnyooshea kidole maana alijua uchafu tu ndo kilichokuwa kinamponza mpaka wazazi wakawa wanamdharau

โ€œSawa kakaโ€ฆ.nilikuwa na mpango huo piaโ€ alijitetea baada ya kuhisi amedharaulika.

โ€œSio kwamba nimesema hauogagi lakini nimekuambia uvae nyingine, wewe mbona mzuri ukiwa kila saa msafi basi utavutia saaanaaโ€ฆhujioni ulivyo mweupe?โ€ alimuuliza, Nasma alitabasamu kwa furaha kwani mwanamke anapenda kusifiwa sana

Alitazama chini kichwa mwake wakiwa anawaza kwamba mh kanipenda au? Lakini ni kwamba jamaa alikuwa anamsaidia tu kimawazo, sio mapenzi.

Hata hivyo baada ya maneno hayo, Ray aliondoka akaenda mpaka pale baba yake alipokuwa anachunga mbuzi โ€œMzee umeamkaje?โ€ alimsalimia

โ€œsalama umeamkaje wewe?โ€ alimuuliza

โ€œsijambo, emb niachie mbuzi hapa ukanywe chai kidogoโ€ alisema Ray na kusogea kwenye jiwe akaketi

โ€œHuh, kuna chai na nini viporo mimi sili bwanaโ€ alisema

โ€œHahaha, mzee unaringaโ€ฆ kule nimeleta chapati za kutoshaโ€ alisema kijana huyo

โ€œHapo sawaโ€ mzee alisema akitabasamu na kuanza kuondoka kuelekea nyumbani.

Sasa alipomuacha Ray pale na mbuzi Ray alipata muda wa kupiga selfie za kutosha, halafu aliwatumia marafiki zake aliokuwa akifanya nao kazi huko jijini Dar.

Lakini pia alimtumia Rose na kuweka captions โ€œUkwen kuko hivi utakuja kweli wewe mtoto mayai?โ€ alisema na kumtumia, akaona imefika na kusomwa tayari, lakini haikujibiwa ikabidi ampigie simu aelewe labda ni ubize ama

โ€œhallow Roseโ€ aliongea baada ya binti kupokea simu

โ€œUsiniite tafadhali niache na maisha yanguโ€ Rose aliongea kwa hasira na kukata simu

Hilo suala lilimpa taabu sana Ray maana alimpenda yule mwanamke japo alikuwa akimsaliti mara kwa mara. Alimpigia simu tena na binti hakupokea simu kabisa ikabidi jamaa abaki akicheka maana hakuelewa kosa lake liko wapi โ€œni hasira kisa sijamtafuta asubuhi atakuwa powa tuโ€ alijisemea Ray na kuchukua jiwe akamrushia kondoo aliyetaka kuondoka eneo lile.

Baada ya kumrushia jiwe, alisikia ujumbe umetumwa akaufungua ni namba mpya
โ€œHello, uko pouwa?โ€

โ€œNiko powa, nani?โ€ alimuuliza

โ€œMi Doto, ingia WhatsApp kuna kitu nimekutumiaโ€ alisema Doto

โ€œOkโ€ Ray alijibu na kuingia WhatsApp moja kwa moja, alipongia hivi aliona ametumiwa ujumbe na Doto, akaingia kwenye msururu, alichokiona kutoka kwa Doto wala hakuaminiโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆ..JE KAONA NINI?
Soma muendelezo kwa sh 1000
Njoo WhatsApp 0743433005.
   

X
SHARE TO SOCIAL MEDIA

๐ฟ๐‘œ๐‘ฃ๐‘’๐‘†๐‘ก๐‘œ๐‘Ÿ๐‘ฆ.....: ๐‹๐€๐’๐“ ๐๐Ž๐‘๐ ๐๐€ ๐๐ˆ๐Š๐ˆ๐‘๐€ ๐˜๐€ ๐‡๐Ž๐”๐’๐„ ๐†๐ˆ๐‘๐‹ (๐™Ž๐™๐™–๐™ฃ๐™œ๐™– ๐™†๐™ž๐™ช๐™ฃ๐™ค๐™ฃ๐™ž) ๐‘ฉ๐’–๐’“๐’–๐’…๐’‚๐’ ๐‘บ๐’Š๐’Ž๐’–๐’๐’Š๐’›๐’Š SEHEMU YA 07  >>> https://gonga94.com/semajambo/lovestory-last-born-na-bikira-ya-house-girl-shanga-kiunoni-burudan-simulizi-sehemu-ya-07

#Nk #gonga94 #trending #instagood #explore #viral #challenge #simulizi #hadithi #israel #iran #war 

Share on Facebook
Share on Twitter
Share on LinkedIn
Share on Pinterest
 

Maoni

You're not logged in
Click here to login and comments
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
gonga94 official track
ZETU
SIMULIZI NA SAUTI ZETU
gonga94ads - The Best Popunder Adnetwork
Kama wewe hujatimiza miaka 18+ usije nasema usije kabisa ni wakubwa tu
Kama wewe hujatimiza miaka 18+ usije nasema usije kabisa ni wakubwa tu

RATIBA YA SIMULI ZETU

Hakuna ratiba iliyopangwa kwa sasa.


Home Login Signup
Top 20 Popular Contact us
Terms & Conditions About us Latest