*MMMM DADDY NIKIKUPA UTANIOWA KWELI?!* *SEASON TWO* *SEHEMU YA 28* Siku hiyo Kingston alioga akajiandaa akaondoka pale nyumbani aliniachia pesa kiasi fulani kwa ajili ya matumizi..
Aliniambia pia nijitahidi kutafuta Dada niishi naye pale😞😞kilichokuwa kinanitesa ni vile haongei chochote kuhusu mimi na yeye..
Kwani ananichukuliaje huyu chalii😂😂😂subiri nitamkomesha..
Nilitoka nikaulizia kwa majirani soko lilipo nikaelekezwa ni mbali🙌unatembea lisaa lizima bado uko njiani😰😰na vile mie mgeni lol
Kwa bahati nzuri wakati bado natembea kwenda sokoni nilipata lift🥰🥰
Ilikuja gari fulani hivi nikashangaa inasimama..
Kwenye gari alikuwemo mkaka naye alikuwa mgeni mitaa ile ndo alikuwa amehamia🥳🥳tulisalimiana then akaniuliza soko lilipo..
Nilimwambia namimi ni mgeni ila nimeelekezwa soko liko mbele mbele hapo nazani siyo mbali sana kutoka hapa...
Oh kwa hiyo na wewe unaelekea sokoni???. Nikamwambia yes naenda sokoni😩😩oh panda basi twende wote🤗🤗
Kwa jinsi nilivyokuwa nimechoka😂😂😂nilipanda tu kwenye gari sikuwa na namna..
Nilipewa lift mpaka sokoni tukahemea zetu na muda wa kurudi pia nikapewa lift mpaka nyumbani🥰🥰...
Yule mkaka alikuwa ni mkarimu sana🥰🥰tulipiga story mbili tatu siku hiyo tukabadilishana na namba ya simu🤩🤩..
Tuliendelea kufahamiana zaidi kwenye simu tukazoeana mpaka nikamuomba anisaidie kutafuta msichana wa kazi🥰🥰🥰hatukuwa tunaishi mbali ni jirani tu ng'ambo ya pili..
Yule mkaka alikubali kunitafutia msichana huko kwaoo..
Mimi na Tristian ambaye ndo huyo mkaka jirani yangu tulizoeana sana kiasi kwamba akawa akitoka kazini jioni lazima aniletee kakitu😂😂😂🙌
Wakati huo Kingston alikuwa amenizuia kumpigia pigia simu alidai anakaribia kufanya mitihani so hataki kugasiwa...
Mawasiliano yetu yalikuwa ya tabu sana na mimi ndo nilikuwa namtafuta yeye aaa🙌🙌🙌..
Nilifanikiwa kupata binti wa kazi mstaarabu sana nikaanza kuishi naye..
Siku zilisonga ile pesa ya matumizi niloachiwa na Kingston ikaisha na wakati huo hata kwenye simu alikuwa hapatikani😺
Kile chakula cha ziada kilichokuwemo ndani kiliisha chote wacha njaa itutandike😂😂🙌
Niliendelea kupiga simu ya Kingston kila siku haipatikani tulikuwa tunashinda njaa jioni Tristan akiniletea chochote kitu ndo tunakigawana na mdada wa kazi tunakula tunalala..
Maisha yaliendelea hivo my wenu nikaanza kukonda😩😩 nikiwaza kumwambia Tristan naogopa kwanza nitaanzaje😂😂🙌
Mkaka wa watu si ataniona chuma ulete😂😂😂hapa cha kufanya niwapigie simu wazazi wa Kingston niwape mkasa mzima ili wanisaidie kabla sijafia hapa makao mapya😂😂😂
Basi bwana siku hiyo nimeamka zangu asubuhi sina hata mia😂😂😂 nikamtuma Dada akaniombee buku kwa Tristan ninunue vocha niwapigie wazazi wa Kingston...
Dada akaenda nikabaki nawaza sijui Tristan atanichukuliaje Mungu wangu lol shida hizi😂😂 na that time mama yangu alikuwa hajui kinachoendelea...
nilikuwa namdanganya kila mwezi kuwa Boss ana matatizo hajanilipa na nikamuahidi akinilipa nitatuma pesa tuendeleze ujenzi🤭🤭🤭
Mama yeye alijua niko kazini na namshukuru Mungu mama hakuwa na namba za wazazi wa Kingston wala wazazi wa Kingston hawakuwa na namba za mama...
Hapo ishapita miezi mitatu tangu nitoke nyumbani🤭🤭na muda huo ujauzito ushafika miezi mitano..
Basi bwana nimekaa kaa hapo Dada akarudi na rundo la pesa kalishikilia mkononi😳😳
nikashangaa wewe mbona pesa nyingi hivi mi si nimekwambia uombe buku peke yake😳😳
Nini kitafuata???...
Full 1000
WhatsApp 0742133100
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi