*MMMM DADDY NIKIKUPA UTANIOWA KWELI?!* *SEASON TWO* *SEHEMU YA 40* Mipango niliyokuwa nayo ni kumuondoa Kingston mikononi mwa lulu aje tulee watoto..
Nilitamani siku moja mimi nayeye tufunge ndoa awe mme wangu hayo ndo malengo yangu kwake..
Siku tuliyopanga Kingston aje kuwaona watoto iliwadia na kweli asubuhi mida ya saa nne the Boy aliwasili akiwa na zawadi kadhaa za watoto na za kwangu mama watoto🤗
Nilimpokea kwa shangwe na vigelegele🥳🥳🥳na muda huo nilikuwa nimesha muita yule kijana aje kunichukulia mapicha ya kutosha🥳🥳
Huyo kijana ni mfanyakazi wangu wa kwenye restaurant nilimuona ni kijana msitaarabu sana mpole na mwenye nidhamu sana thas why nilimtumia kwenye hii mipango yangu..
Swala la picha lilianzia kule mgahawani siku ya kwanza Kingston anakuja kuniona kuna picha kadhaa pia nilimwambia huyo kijana anipige nikiwa na Kingston..
Kingston alifurahi sana alipowaona watoto wake.... Damu yangu hii🥹🥹🥹alijisemea huku akinikumbatia na kuniambia asante sana kwa kuwa mwanamke jasiri na mama bora kwa watoto wangu🥹🥹🥹
Yote hayo wakati yanaendelea tayari camera ya siri ilikuwa inarecord kila kitu🥰🥰🥰...
Siku hiyo tulikula tukanywa tukafurahi ilipofika jioni Kingston aliondoka lakini aliniomba sana nimruhusu aweze kuwa karibu na watoto wake..
Nilimwambia it's okay hilo halina kipingamizi... nilizidisha ukaribu kwa Kingston kiasi kwamba asubuhi mchana mpaka usiku alikuwa anakuja kula pale mgawahani kwangu...
na kila weekend tukawa tunatoka wote kwenda kuenjoy na twins wetu🥳 ukaribu ule ulimfanya Kingston aanze kunionea wivu sana😩😩
Muda wote akawa anataka kujua niko wapi nafanya nini na kibaya zaidi kilichozidi kumchanganya ni vile nilivokuwa simfuatilii wala kumuuliza chochote juu ya mahusiano yake yeye na lulu🤣🤣🤣...
Kutokumfuatilia kwangu Kingston kulimfanya aamini kuwa mimi nina mwanaume na ndo maana sina shida naye🤣🤣🤣..
Sikuwa na mwanaume ila ni mbinu tu niliamua kuitumia ili ajilete mwenyewe🤣🤣 unajua hao nao ukiwafuatilia wanajiona sana cake😂😂😂...
Jamaa alizidisha wivu mpaka akaanza kuwa analala kwangu😴😴mdogo mdogo tukajikuta kwenye huba zito mapenzi ndindindi💋💋
Baada ya kuhakikisha kuwa Kingston sasa hawezi kuchomoka mikononi kwangu....
Kuna mchezo niliamua kuucheza😴😴😴 kama mnakumbuka niliwaambia kuna picha zilipigwa kwa siri bila Kingston kujua..
Zile picha nilienda kuziweka kwenye picha mbao alafu siku moja mchana kweupeee nikamtuma mtu azipeleke kule ofisini kwa Kingston..
Zilipelekwa picha tatu moja nikiwa mimi na yeye tunakiss🤗🤗🤗picha ya pili akiwa amewabebelea twins wake🤪🤪na picha ya tatu tuko wote mimi yeye na watoto🥳
Zile picha zilikuwa kubwa kama unavyojua picha mbao huwezi kuificha mfukoni😂😂😂inamaana kila mfanyakazi lazima angeziona tu🥳🥳🥳
Nyieeee nyieeeè picha linaanza siku picha zinapelekwa zilipokelewa na lulu maana yeye ndo receptionist wa hapo ofisini kwao🥳🥳🥳...
Alipoziona picha baraaa likaanza watu wakadundana humo humo ofisini wakatoleana matusi mpaka ya nguoni wakaachania hapohapo🤪 vita ya panzi furaha ya kunguru😂😂😂kunguru ndo mimi hapa zarina🤗
Baada ya hilo varangati mwanaume akaenda akachukua mabegi yake akahamia mjengoni💃🏼💃🏼 nikajichukulia Dodo bila hata kutumia nguvu😂
Lulu na Kingston walikuwa wapenzi tu bado walikuwa hawajaoana wala kuchumbiana🤣🤣🤣hata mtoto tu alikuwa hajamzalia🤣🤣🤣
Baada ya kumchukua Kingston kutoka kwa lulu tulianza kuishi wote kwa miezi kadhaa nikamwambia baba la baba sa sikia nikupe mchongo🥳🥳
Twenzetu Arusha kwa wazazi wako ukawaombe radhi muweke mambo sawa🤗🤗🤗
baada ya hapo nitambulishe kwenu nikutambulishe kwetu tufunge ndoa tulee watoto hakuna muda wa kupoteza😴😂😂😂...aku chelewa chelewa nitakuja kunyang'anywa tena🤣
Mshikaji wala hakupinga tulikwea pipa mpaka Arushani pale kwa wakwe tukiwa full family hatujali wala nene🥳🥳🥳
Mama mkwe alipotuona akataka kuleta za kuleta tukamwambia oya maza sikiliza😴😴😴sisi hapa ndo tushapendana upende usipende ndo tunaenda kuoana🥳🥳🥳🥳
Mama ilibidi aachilie kinyongo chake akaanza kucheza pale na wajukuu akaniomba na msamaha siku ile alinikataa akanifukuza na badae akaanza kunizushia namchukua mzee wake mie nilimsamehe kwa yote..
Baada ya hapo tukaenda kwetu💃🏼💃🏼💃🏼💃🏼nikatolewa posa mahari ikaletwa...
baada ya hapo ikaandaliwa harusi fulani hivi ya kishua... moja ya marafiki niliowaalika kwenye harusi yangu ni Tristan jamaa alishawahi kunisaidia sana nisingeweza kumsahau kirahisi hivo..
Tristan alifurahi sana kuniona nikiwa mshindi🥳🥳alinipongeza nikamshukuru kwa wema aliowahi kunitendea basi bwana mimi na Kingston tukafunga ndoa takatifu..
Wanasemaga mshindi ni yule anayetangazwa kanisani my wenu mimi ndo niliibuka mshindi katika kinyang'anyiro cha kumnga'ang'ania Kingston🤣🤣🤣wenzangu Mary na lulu walizubaa mie nikajichukulia kombe...
Bwana ninaye na ninatamba naye🥳🥳🥳Na mpaka leo hii tuko wote tunapendana sana🥰🥰
kwa sasa tuna watoto watatu wa kike mmoja wa kiume wawili hatuna mpango wa kuongeza kwa sasa ni kukulana tu na kuenjoy maisha🙈🙈...byeeeeeeeee...
*mwisho*
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi