MUME WANGU ALIVYONIOLEA MKE WA PILI SEHEMU YA : 13 KWa mwendo wa taratibu nikamsogelea sabra na kWa sauti ya chini na yenye u serious
“Katika vitu ambavyo sitaki utani kabisa Basi ni watoto wangu, sabra Kaa mbali na mambo ya watoto wangu”
Wala sikutaka kupoteza muda kisha huyo nikaondoka na kurudi zangu kazini, kabla sijaanza kufanya chochote kile, ujumbe mfupi wa simu ukaingia kwenye simu yangu na ulitoka kwa sabra na ulisomeka hivi.
“Mimi ndio naweza kukusaidia wewe kupata watoto wako hivyo kama utaitaji msaada Nipo kukusaidia Wifi yangu kipenzi nakupenda “
Aaah kuna watu jamani aibu hawana kabisa, Yaani huyu sabra ni Mmoja kati ya watu ambao wamechochea sana ndoa yangu Kuwa ya moto, kuna kitu sikuwai kuwaambia, sabra huyu Niliishi nae pale Nyumbani kwangu kwa mwaka mmoja eeeh cha moto nilikiona, sabra alihakikisha Kuwa kila siku nalia, alihakikisha Kuwa amani kwangu ni kitu cha ajabu sana, halafu Leo hii anataka kujifanya Kuwa yeye ni msaada kwangu.
Nikiwa nimeshikilia simu yangu gafla muda huo huo alikuja mtu na kunishika begani Walahi nilishtuka sana na kujikuta nikitupa simu chini.
“Uko Sawa kweli ??”
Max aliniuliza, Yaani boss wangu.
“Yaaah, yeah Niko Sawa “
Nilijibu kWa sauti ya wasiwasi sana.
“Njoo upumzike uku “
Alizungumza boss wangu kisha akanishika mkono na moja kwa moja akanipeleka ofisini kwake na kunipatia maji ya kunywa.
“Pumzika kwanza “
Alizungumza max kisha akatoka nje.
Kiukweli siku yangu ilikuwa ngumu sana, nilijikuta nikiwawazia sana watoto wangu, kuna Namna nilitamani ata kwenda kuwaona lakini sikuruhusiwa kwani kesi ndio kwanza ipo mahakamani.
Majila ya Kama saa 2 usiku hivi, muda ambao nilikuwa najiandaa kwenda Nyumbani, max alikuja na kuomba kunirudisha Nyumbani, kwa wakati huo Mimi na max tulikuwa tumezoeana sana hivyo sikuweza kukataa haraka nikakubali na safari ya kwenda Nyumbani kwetu ikaanza.
Kwakuwa nilikuwa na mawazo sana ata sikuwa naangalia gari ilikuwa inaenda wapi gafla tu nikajikuta nikiwa nje ya Jumba la sinema.
“Uku wapi ??”
Nilimuuliza Max.
“Hauko sawa Shamsa hivyo Basi Nafikili hapa pataibua mood yako nzuri “
“Max bwnaa usingejichosha ningeenda tu Nyumbani kupumzika”
“Usijali wewe ni mtu wangu wa Karibu sana Sawa, so relax and let’s go babe girl”
Ila nyie huyu kama anajua kucheza na akili yangu, Mwenyewe nikajikuta nikitabasamu na kwa pamoja tukaingia kwenye jumba la sinema.
Eeeeh nilitaka kusahau Bwana ata Kama Mimi ni mtu mzima lakini Nyumbani kwetu Nyumbani kuingia Ndani mwisho ni saa 3 usiku 😂🙌 Yaani ikipita muda huo tafuta pa kulala tu maana eeeh cha moto utakiona, Basi nikachukua simu yangu na kumwambia mama Kuwa nitalala kwa Neha kwani mama yangu anamjua Neha.
Mimi na max tukaangalia movie pale na movie ikaja kuisha saa 7 kasoro usiku.
“Neha Apokei simu “
Nilimwambia max uku Nikiwa natamani ata kulia 😂🙌 Yaani Mimi nilipanga nikitoka hapo niende kulala kWa Neha, Picha linaanza Neha Apokei simu.
Nilijitaidi kupiga simu mfululizo mwisho Neha akatokea.
“We nawe ata ujaniambia mapema, me Nipo uku ukweni shoga Angu, shemeji yangu Mdogo anamvisha mchumba wake Pete”
😂😂🙌 kweli nguo ya kuazima aistiliiii……….. malizieni waenga 😂 Yaani Leo ndio nitajua Sijui kabisa.
“Twende kwangu “
Alizungumza max.
Niligeuka na kumuangalia sana mwisho Nikacheka.
“Unacheka nini sasa na Mimi nakuambia ukweli Kama utaki kwangu Twende kwenu tukamgongee baba yako “
“Acha bwna “
Mpaka nilipofikia jamani Sina changuo hapa ni kwenda kulala kwa max tu.
Basi safari ikaanza pale moja kwa moja kuelekea Nyumbani kWa max.
Mkaka wa watu akiwa bize na kuendesha gari, Mimi nilikuwa bize kuangalia uzuri wake tu, nisiwe Muongo nimemtamani huyu kaka sio kidogo 😂🙌 majilani mnisiadie kumwambia ikiwezekana awe wangu tu au amtaki shemeji jamani 😂🙌.
Hatimaye tulifika Nyumbani kwa Max nyieeeh macho yalinitoka na kubaki nikishangaa huo mjumba ulivyokuwa mkubwa.
Baada ya muda geti lilifunguliwa na max akaingiza gari Ndani.
“Karibu sana Shamsa”
“Weeeh kwanza subili ulikuwa unajenga Nyumba au Ikulu ??”
Max akaniangalia kwa muda kisha akacheka sana na kuniambia.
“We mjinga sana ujue sasa Ikulu iko wapi hapa 😂 Binti Ebu shuka Twende uko “
“Max “
Nilimuita kwa sauti ya utulivu sana, max akageuka na kuniangalia tu nakubaki akinisikiliza.
“Hivi uku ata ukiniteka napigaje Kelele Mimi 🥹 hivi kuna mtu anaweza akanisikia kweli 😂”
Max alijikuta akicheka sana maana hakutalajia kabisa Kama nikamwambia kitu Kama iko.
“Shamsa acha Basi Ebu Twende ona mama anavyotuangalia”
Hapo kwanza nikashtuka sana na kuangalia mbele ambapo nikamuona mwanamke mtu mzima akiwa Amesimama kwenye mlango mkubwa wa kuingilia Ndani.
“Wewe kumbe upo na mama yako ??”
Niliuliza nikiwa na wasiwasi wa hali ya juu Wala sikutalajia Kama kutakuwa na watu wengine hapo kwake.
Kwa pamoja tukashuka, haraka max akanisogelea na kunishika mkono maana aliona Kuwa Nina woga Fulani hivi.
“Shikamoo mama “
Nilimsalimia mwanamama huyo uku nikikunja goti kidogo.
“Marahaba mkwe yangu Karibu sana “
Alijibu mama huyo Tena kWa kuniita mkwe, haraka nikamgeukia max na akanikonyeza tu akimaanisha nitulie.
Basi nilibaki nikijichekesha tu, mama huyo akanikaribisha kwa furaha sana na bashasha ya hali ya juu akiamini Kuwa Mimi ni mkwe wake.
“Wewe hiki ndio chumba cha wageni au ??”
Nilimuuliza Max baada ya kunieleka kwenye chumba ambacho kilikuwa na Picha zake nyingi sana.
“Hapana hiki ni chumba changu “
Alijibu max na kusogea kitandani kisha akakaa na kuning’iniza miguu yake.
“Karibu ukae”
Alizungumza max na kushika mkono wangu akitaka nikae Karibu yake.
“Max ungenipeleka kwenye chumba cha wageni tu chumbani kwako sio Sawa kabisa”
“Naelewa lakini Tulia kwanza aaah mama yangu Ana shida ya akili kidogo na hapo amekufananisha na mke wangu “
Nyieeeeh kumbe Ana mke huyu 🥹 Yaani kitendo cha kusema mke wangu Ka moyo kangu kakafanya paaaah, na sio tu kufanya paaaah nilijikuta nikiumia sana, huyu kaka sijamtamani tu lakini nimependa kabisa na nazani kwakuwa ananijali sana 🥹🥹.
Kwa mshtuko wa hali ya juu nikamuuliza.
“Mke ?? “
ITAENDELEA….
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi



Maoni