BINAMU WEWE UNGEWEZA? SEHEMU 08
ENDELEA.......
Nilimueleza mama kila kitu wala sikumficha.
"Wewe huyu mpaka Sony anakupiga kwaajili ya Manka. Aiseee sikuwai kujua kama unaishi na nyoka ndani mwako. Pole binti yangu" mama aliongea kwa masikitiko.
Hakutaka mambo yaishe juu juu alihitisha kikao, wazazi wa Sony waliitwa na mtoto wapo, Manka pia alitlitwa. Taarifa zilimfikia baba nje ya nchi chapu. Alimpigia simu dada yake kumshtakia aliyofanya mwanae ila mama Manka ndo kwanza alifurahi na kusema kwamba mimi kuwa na Sony huenda haikupangwa aliyepangiwa ni Manka.
Saa mbili usiku wote walikuwa wamefika.
Mama aliwaeleza yanayoendelea kati yangu na Sony na chanzo ni Manka.
"Sony ni kweli?" Mama yake alimuuliza.
Sony bila kupepesa macho alikubali kuwa ni kweli.
"Kwanini sasa umefanya hivi, huoni kuwa ni mambo ya aibu na yanaweza kujiludia katika kizazi chako?.
" halikuwa jambo nililolikusudia naombeni mniradhi wazazi wangu".
"Kwaiyo una mpango gani na Nice mpaka sasa"
"Nice nilishaongea nae kwaiyo hakuna kilichobadilika"
"Mbwa wewe. Unataka kuendesha mambo ki lahisi tu ilhali umefanya kosa kubwa, mtoto mshe....nzi sana wewe , ningejua kama nazaa mtoto mji.....nga kama wewe ningekubana kichwa hicho siku na kuzaa ili uzaliwe na kichwa kirefu kama treni" Mama Sony alichafukwa kweli kweli. Maneno aliyokuwa anaongea yalichekesha sema hakuna aliyecheka kutokana na jambo hili kuwa serious sana.
"Achana na huyu binti haraka iwezekanavyo sio ombi ni lazima" baba wa Sony aliongea hayo akimtaaka mwanae aachane na Manka.
"Tena mama Nice huyu mwehu aludishwe kijijini kwao hata kesho mapema tu"
"Mbona mnakosa utu na ikiwa mimi huyu naenda kuwapa furaha mtoto wenu kwa kuitwa baba. Nyinyi hamtaki mjukuu?, yaani kwaajili ya huyu mgumba mnataka kunifanyia roho mbaya mimi niliyebeba kiumbe chenu tumboni kwangu"
Baada ya manka kuniita mimi mgumba mimi na mama tulitazamana alafu.
"Sony achana na huyu mpuuzi haraka iwezekananyo na tambua kuwa hatumtambui yeye wala huyo mtoto" mama yake aliongea kwa hasira.
"Muacheni achakue mwenyewe anataka kubaki na nani kwanini mnataka kuingilia maamuzi yake. Sony chagua ni kati yangu na Nice unabaki na nani na kama utamchagua Nice silazi damu naenda kutoa hii mimba" Manka aliongea hayo.
"Chagua sasa mbona unakaa kimya" Mama Sony alimwambia mwanae.
"Sony chagua mmoja kama unataka kubaki na Nice sema nikatoe mimba mimi" Manka aliongea kwa makasiriko.
Baada ya ukimya wa muda mrefu Sony alichagua.
"Nitabaki na Manka" nyie moyo wangu ulipasuka pasuka. Mwili uliishiwa nguvu kabisa.
"Huyu ndo mwanamke unayempenda?" Baba yake alimuuliza.
"Ndiyo kwa sasa nampenda Manka na sio Nice, huyu ndo mama watoto wangu" Sony alimmwagia sifa Manka. Manka mwenyewe sasa anachekelea meno 32 nje.
Mie nilikuwa natabasamu tu huku nasilitika
"Nice haina haja ya kuzungumza chochote kwakuwa kamchagua Manka acha awe nae lakini siku zote MUNGU ni wa mwenye haki. Haki yako ipo binti yangu"
"Jamani sina la kusema zaidi ya kusema Asante. Mnaweza mkaondoka sasa" Mama aliongea hayo kwa unyonge. Wazazi wa Sony hawakuwa na namna walimuomba mama msamaha na baada ya hapo waliondoka.
"Nisamehe Nice siwezi kuiacha damu yangu iteketee" Sony aliongea hayo kabda ya kuondoka.
"Washenzi nyie. Nafumba na kufumbua nisawaone hapa, na wewe Manka kamwe usije ukajitokeza tena kwenye familia yangu kwa hili ulilomfanyia Nice utalilipa tu kwa namna yoyote ile.
Mwanangu alikutoa kijijini ameishi na wewe kwa upendo wote mpaka umeng'aa leo hii unajiona mjanja. Umesahau kama hii ni dunia eeeeeh!.
"Kila mtu ashinde mechi yake. Kabda ya kunilahumu mimi muulize kwanza mwanao kizazi kakipeleka wapi mpaka leo hii ashindwa kumzalia Sony au anadunga misindano ya uzazi wa mpanga?" Manka aliongea hayo kwa dharau.........ITAENDELEA..........
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi
Maoni