VYOTE NDANI GONGA94
BINAMU WEWE UNGEWEZA? SEHENU 07
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
ENDELEA.......
"Mbona unaongea ni kama vile umefanya jambo la kawaida na wala hujutii makosa yako. Vipi unafikilia nini kuhusu familia na ukoo wetu? Huoni kama umetusababishia laana?"
"Ni jambo la bahati mbaya"
"Mbona kama ni bahati mbaya unajali sana kuhusu yeye. Imefikia hatua unanipiga na wala haunisikilizi kwa chochote wala kujali kuhusu mimi"
"Ni kwaajili ya mtoto tu ila tambua wewe ndiyo mwanamke wa maisha yangu"
"Ni Upuuzi mtupu" niliongea hayo kwa hasira niliinuka nikataka kuondoka ila Sony alinidaka mkono wangu. Muda huo huo Manka alifika eneo hilo.
Taratibu Sony aliniachia mkono ndipo nikajua kwa sasa Manka ndiye udhaifu wake. Sikutaka kuendelea kubaki eneo hilo nilitoka mpaka nje ya hotel kwanza nilitafuta sehemu ya kulilia mpaka nitosheke ndipo niludi kazini. Niliingia kwenye bustani iliyopo hapo Hotelini nilianza kulia.
Mala gafla nilishangaa nanyooshewa mkono wenye leso, sikujua mtu huyo ni nani. Niliipokea ile lesho nilifuta machozi mpaka makamasi alafu niligeuka kumtazama mtu aliyenipa leso ni nani.
Ni kijana handsome sanaaaaa na anavutia machoni pa kila mwanamke na zaidi ni mtanashati nikoumaaa!. Sura yake wala haikuwa ngeni machoni pangu.
"Asante kwa kujali" Nilimshukuru kijana yule wala hakunijibu aliachia tabasamu bomba usoni mwake, uzuri wake uliongezeka zaidi kutokana na Dimpozi alizokuwa nazo mashavuni mwake.
"Naitwa Iron nadhani sio mgeni sana machoni pako"
"Nakumbuka nilikuona hivi karibuni kazini kwetu. Nafurahi kufahamiana na wewe. Naitwa Nice"
"Waooooh! My lady. Una jina nzuri kama uzuri wa sura na umbo lako, bila shaka una moyo safiii! Pia"
Niliachia tu tabasamu. Kuongea kidogo tu Iron maumivu ya moyo yalipoa kwa kiasi chake.
"Sitegemei kukuona unalia tena mrembo wangu. Usilie nipo kwaajili yako" Iron aliyasema hayo nikajisemea huyu bwana vipi mbona gafla sana nae si ndo mafataki vijana wenyewe hawa.
"Niliagana Na Iron nililudi kazini yeye nilimuacha bustanini.
Jioni baada ya kutoka kazini nilipitia nyumbani kwetu.
" ujio wako wa leo unaonekana kabisa haupo sawa. Usinifiche niambia nini tatizo" Mama aliomgea hayo kabda ya kuanza kumuambia ukatili walionifanyia Manka na Sony nilianza kulia.
"Usiniambie Sony amekataa mimba?. Hofu ya mama alijua labda Sony ameikataa mimba yangu.
"Mpaka sasa hajui kama mimi ni mjamzito, mama napata wapi kungu ya kumwambia Sony kama nina mimba ilhali yeye na manka pia wanatarajia kupata mtoto siku za usoni. Mama hii aibu sijui hata pakuifichia" niliongea hayo huku nalia.
Mshtuko alioupata mama nilihisi presha inampanda muda si mrefu, haraka nilienda kumletea maji nikampa anywe kwanza. Baada ya mama kunywa maji alikaa kimya kama dakika kumi hivi.
Joleen aliludi kutoka chuo alitukuta na simanzi.
"Sijui ni nini kinaendelea kati shemeji na dada Manka. Huwezi amini nimekutana nao Super market tena wanabebishana balaaa na hata waliponiona Dada Manka hakuonyesha kujali wala kuogopa ndo kwanza alizidisha mbwembwe. Eti dada kuna nini?" Joleen aliongea.
"Hivi ni kweli kumbe oooih! MUNGU wangu ni nini hiki kinataka kumtokea binti yangu. Muhurumie BABA". Mama alimlilia MUNGU kwanza kabda hajaendelea kuongea zaidi........ITAENDELEA...........
Umesoma kwa utulivu ยท dakika chache tu Asante Endelea kusoma chagua hapo chini
Umependezwa ?? Asante Soma Zaidi binamu-wewe-ungeweza-sehenu