BETWEEN SISTERS AND SECRET 8-9 Chapter 8 "Sweetheart, hapa ni kituo cha watoto yatima. Kila mwaka huwa tunakuja kupata nao chakula,
kucheza nao..."
Mira alimkatisha Gael. "Kwahiyo hii ndo sehemu nzuri uliyoniambia?"
"Ndiyo sweetie, hapa kuna furaha ya kweli.
Twende ndani, ukajionee mwenyewe."
Gael alimfungulia Mira mlango, akashuka.
Waliingia kwenye geti dogo.
"Gael, mbona umechelewa sana leo?" Mr.
Maximilian alimuuliza Gael.
"Nilikuwa na kazi nyingi sana baba, lakini kwa bahati nimewahi kidogo kufika."
"Na huyu amefuata nini hapa?" Bi Helen alimuuliza Gael.
"Mama, huyu ni mpenzi wangu. Ana haki ya
kuwa hapa, na nina haki ya kwenda naye popote ninapotaka, alijibu Gael bila uoga huku ameushika mkono wa Mira.
"Unamjibu vipi hivyo mama yako!" Mr.
Maximilian alikasirika sana.
"Mume wangu, acha yapite. Hapa kuna
wafanyakazi na watoto, tusiwape watu faida. Tufanye kilichotuleta," Bi Helen alimtuliza mumewe.
"Mira, twende huku," Gael alimshika mkono, wakaelekea upande mwingine.
"Gael, mimi siwezi kukaa hapa. Mazingira ya hapa si mazuri hata kidogo, na sipendi kelele," Mira aliwaangalia watoto kama ameona kitu cha
ajabu.
"Basi kaa hapa unisubiri. Sasa hivi narudi then tunaondoka."
"Okay babe, usichukue muda mrefu," Mira alimkiss Gael shavuni.
Upande wa bustanini, Mia alikuwa akicheza na
watoto, na walionekana kumpenda sana.
"Hahaha, subirini kwanza! Kwanini kila mara
mimi ndo nashindwa? Nyie mtakuwa mnanichezea mchezo nyie!" Mia aliongea huku
anatabasamu. "Aunt Mia, wewe hujui kucheza huu mchezo, ndomana kila mara unashindwa, alisema
Jasmine.
"Kweli eeh? Basi inabidi mnifundishe," alisema Mia.
"Sawa Aunt Mia, wewe ni mzuri sana. Tunatamani uje hapa kila siku!"
"Msijali watoto wazuri, kila mara nikipata muda nitakuja hapa kujumuika nanyi."
"Kweli?" watoto walimuuliza kwa furaha.
"Ndiyo, hii ni ahadi," Mia alijibu kwa tabasamu.
Gael alimuangalia Mia akitabasamu.
"Uncle Gael!" watoto walimkimbilia Gael.
"Niliwamiss sana," alisema Gael, wakakumbatiana.
"Natataka kuondoka hapa sasa hivi, sitaki hata kumsalimia, Mia alitaka kuondoka, Gael akamzuia.
"Unaenda wapi?"
"Aaah, naenda kuwasaidia watoto wadogo kuoga na kuvaa, wanatakiwa kwenda kula sasa,"
Mia alitafuta sababu ya kumtoroka Gael.
"Basi tunaweza kwenda pamoja."
"Hapana boss, unaweza ukachafuka. Acha mimi nitafanya hiyo kazi, naimudu mwenyewe. Na
kuna watu wengine wapo hapa. Furaha, si tutaenda pamoja?" Mia alimuuliza Furaha.
"Utanisamehe kwa leo shoga yangu, nimeshafanya kazi nyingi sana. Acha nipumzike, Furaha alikataa na kukaa kwenye kiti.
"Naweza kwenda kusaidia, acha ubishi, Gael alitangulia.
Mia alimfuata nyuma. Waliwaogesha watoto kwa pamoja.
Gael alijikuta anamuangalia sana Mia Jinsi anavyowajali watoto na kucheza nao kwa upendo.
"Acheni kuchezea maji, ni muda wa kuvaa sasa," alisema Gael baada ya kumuona Mia akicheka. "Sawa Uncle Gael!" watoto waliitikia kwa
pamoja.
Alibaki Gael na Mia.
"Samahani kwa kilichotokea jana," Gael alimwambia Mia.
"Kilichotokea jana? Kipi hicho?" aliuliza Mia.
"Niliondoka haraka kwa sababu ya kikao, ila najua sikufanya vizuri," Gael alidanganya,
hakutaka kusema sababu iliyomfanya aondoke. "Aaah, hata usijali boss. Hata hivyo lazima uwe
busy kusimamia kampuni na mambo mengine ya muhimu."
"Wewe pia ni mtu muhimu, nimegundua hilo leo." "Unamaanisha nini?" aliuliza Mia. "Sikuwahi kuona mtu akiwajali hawa watoto
kama unavyofanya wewe. Wewe ni mrembo sana, na una roho nzuri kama sura yako,"
aliongea Gael huku anatabasamu.
"Asante sana boss kwa maneno yako, nitaenda kuwaangalia watoto, Mia alitabasamu kisha akaondoka.
Chapter 9
"Asante sana boss kwa neno yako, nitaenda kuwaangalia watoto. Mia alitabasamu kisha akaondoka.
"Mmmh, ni kweli yeye ni wa tofauti sana. Gael alijiongelea mwenyewe huku anamsindikiza Mia kwa macho..
Mia alijitahidi kumkwepa Gael, lakini kila alipoenda, Gael alikuwa pembeni yake.
"Huyu mbona kama amekuwa mlinzi wangu sasa, kila ninapoenda yupo," Mia alijiongelea mwenyewe.
"Nimerudi mpenzi," Gael alimkumbatia Mira.
"Umekaa sana huko, nimekusubiri kwa muda mrefu na unajua sipendi kusubiri, Mira aliongea
huku amenuna.. "Nisamehe mpenzi wangu, halitojirudia tena.
Tunaweza kuondoka sasa, Gael alimshika
mkono Mira wakaondoka.
Siku hiyo ilikuwa ni siku ya furaha kwa watoto
wa kituo cha Tumaini Jipya. Asubuhi Mia aliwahi sana kwenda kazini, cha ajabu alimkuta Gael nje ya duka.
"Boss Gael, kuna kitu unataka au umegizwa na Mama G?" Mia alimuuliza.
"Hapana, hayo yote sio majibu... nimekuja hapa kukuona. Hii ni kwa ajili yako, Gael alimkabidhi
Mia kibox cha zawadi.
"Ni nini hiki?" aliuliza Mia.
"Ni zawadi ndogo kwa ajili yako," aliongea Gael huku anatabasamu.
"Kwanini unipe zawadi, boss Gael? Mia aliuliza huku anaangalia huku na huku, hakutaka mtu
yoyote amuone.
"Nimeona jinsi unavyowajali watoto na upendo wako kwao ni wa kweli. Hii imenifanya nitamani
kuwa karibu na wewe ili nikujue zaidi, na tunaweza kuwa marafiki, aliongea Gael huku anatabasamu.
"Hapana boss wangu, siwezi kupokea hii zawadi, Mia alimrudishia kibox.
"Ukiikataa hii zawadi utanifanya nijisikie vibaya.... ipokee tafadhali," Gael aliongea kwa
kubembeleza.
Mia alimuangalia kwa wasiwasi.
"Sawa, nitaipokea kwa sababu umesisitiza niipokee, Mia alichukua kile kibox akakificha
kwenye begi lake
"Mbona una wasiwasi kama vile unafanya kitu
kibaya?" Gael alimuuliza.
"Mbona nipo sawa tu, Mia alijilazimisha kutabasamu.
"Okay, kwa kuwa umepokea zawadi yangu, kuanzia leo sisi ni marafiki."
"Eeeh, kama ni hivyo chukua zawadi yako," Mia
alitaka kuitoa kwenye begi. "Hata ukiitoa sitoipokea... hii hapa utanitafuta
muda wowote," Gael aliweka business card yake kwenye meza ya Mia kisha akaondoka.
"Wewe... namaanisha boss Gael, Mia aliita, lakini Gael aliondoka huku anatabasamu.
Judith, Dora na Furaha walikuwa ndio wanafika dukani. Furaha aliona kila kitu ila akazuga.
"Kuna nini kati yako na Gael?" Furaha alimtumia Mia meseji.
"Hakuna kitu chochote, alijibu Mia.
"Mbona kama amekupa zawadi na mliongea
kwa muda mrefu?"
"Anataka tuwe marafiki, sijui itakuwaje. Naogopa Mira akijua."
"Tutaongea vizuri baadaye, nimepata mteja," Furaha aliendelea kuhudumia.
Jioni, baada ya kufunga duka, Furaha alimvuta Mia pembeni.
"Mmmh, niambie."
"Nikwambie nini?" Mia aliuliza. "Nawe kama umesahau vile, si kuhusu boss
Gael.
"Anataka tuwe marafiki, lakini mimi sitaki. Naogopa Mira akijua atanihisi vibaya kama kwa Joel."
"Acha uoga, yani uache kuwa na ukaribu na mtu kwa sababu ya Mira?"
"Furaha, unajua kabisa Mira alivyo. Sitaki kugombana naye kwa mara nyingine."
"Acha ujinga, kwa jema lipi ambalo ulimfanyia Mira akaliona? Kila unachomfanyia anaona
umemkosea. "Kwahiyo unanishauri vipi?"
"Kubali tu, si urafiki wa kawaida. Acha kumuogopa mtu."
Mia aliamua kusikiliza maneno ya Furaha.
Kwa upande wa Gael na Mira, walienda club
maarufu Blue Haven.
"Babe, leo nimefurahi sana. Umenipa muda wako mwingi kuliko siku zote, Mira aliongea kwa kudeka huku amelalia bega la Gael.
"Natamani kila siku tuwe pamoja kama hivi. Ni kazi tu zinanibana, ila nitajitahidi kutenga muda
kwa ajili yako, mpenzi, Gael alimkiss Mira kwenye paji la uso.
"Babe, afu familia yako hata hawanipendi ujue."
"Nalijua hilo, ila usiwe na wasiwasi. Hakuna. anayeweza kututenganisha, na soon tutafunga
ndoa."
"Kweli babe?" Mira aliuliza kwa kupayuka. "Yeah, ni kweli kabisa. Nataka tuanzishe familial
haraka sana,"
"Nimefurahi sana babe, lakini nataka tufurahie ndoa yetu kwanza. Sitaki kuzaa mapema."
"Kwanini?" aliuliza Gael huku anamuangalia Mira
kwa makini.
"Huoni kama nikizaa nitajiharibu shape yangu,
na usichana wangu ndio utakuwa umeishia hapo. Kila kitu kitabadilika, sio mwili tu, hata kazi
na starehe, Mira aliongea bila wasiwasi wowote,
"Oh, kwahiyo unataka tupate watoto baada ya
muda gani?" aliuliza Gael swali la mtego.
"Mmmh, hata miaka sita hivi baada ya ndoa.
Tutakuwa tumesha enjoy vya kutosha, Mira aliongea bila wasiwasi, hakujua kama Gael
alimuangalia huku akijiuliza maswali mengi
kichwani kwake.
"Okay, ni uamuzi wako, Gael alinyanyua glass
yake akanywa pombe yote kwa mkupuo.
"Babe, naenda toilet mara moja," Mira aliondoka.
Wakati anatoka chooni, alivutwa kwenye giza na
Full 1000
Whatsp 0784468229
Makala nyingine zinazocheza na ladha yako
Mapendekezo haya yanatokana na kile unachosoma sasa + Endelea kugundua zaidi

Maoni