VYOTE NDANI GONGA94
FORGIVE ME, MOM ๐ญ๐ญ NISAMEHE MAMA SEHEMU YA: 08
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
SONGA NAYO...........
Nifurahi Sana kujua kuwa Julius amepiga na alikuwa akitaka kujua naendeleaje
"Naweza nikaongea nae....??"
Niliuliza lakini muda huo huo Julius alikata simu na kutuma sms
"Kama Kuna bill zitakuwa zimeongezeka utaniambia lakini pia usimuamini huyo mwanamke "
Alituma ujumbe huo kwa Ness , Ness aliishia kunitizama tu Kisha akaondoka nililia Sana niliona ni dunia chungu kiasi gani pale watu ambao unategemea upendo kwao wanakuwa wa kwanza kukutenga.
Baada ya wiki moja nilipona kabisa na niliruhusiwa nilikuwa na mawazo Sana kuwa nitaenda wapi Mimi nitaishije, muonekano mbaya angu mzuri ulishaanza kupotea niliogopa hata kukutana na marafiki zangu ambao nilikuwa nawavimbia, nilianza kuzulula huku na huku nikitafuta ajila ambayo kwa namna Moja au nyingine ingenisaidia kuendesha maisha yangu, nikiwa nimekaa kwenye kituo Cha daladala jua lote lilikuwa likinipiga Mimi , ilipack gari nzuri ya kisasa gari yenye muonekano mzuri sana Kisha kioo kikashushwa mwanamama aliyekuwa kwenye gari akaniita
" Binti....."
Niliinuka na kumfata
"Habari yako,"
"Salama shikamoo"
"Marahaba, unafanya Nini hapa nimepita kama Mara tatu nakuona umekaa tu hapa upandi gari uendi kokote au Kuna mgeni unamsubili....??"
Niliangalia chini na machozi kuanza kunitoka, Kisha nikajibu
" Sina pa kwenda Sina familia Sina chochote Ni Mimi tu "
Mama yule alishuka kwenye gari na kunifata Kisha akanikumbatia kwa kunipa moyo
"Nitakusaidia ongozana na Mimi panda kwenye gari"
Akanifungulia mlango wa nyuma nikapanda Kisha Safari ikaanza, Gari lilitembea Sana mwisho tulifika kwenye nyumb kubwa ya kifahari, ilikuwa nyumba nzuri yenye kila kitu swimming pool yaani ilikuwa nyumba ya luxury Sana, nilikuta mabinti Kama watatu wakiwa wanaogelea Moja kwa moja nilijua kuwa watakuwa Ni watoto wake, maana mama huyo alionekana kuwa umri umeenda Seema pesa Zina mbeba, binti mmoja alitoka kwenye maji na kumfuata lakini haraka akasema
"Noooh unaweza kuendelea kuoga "
Basi binti yule akarudi kwenye maji, nilifurahi sana kuyaona maisha hayo maana nilikuwa nayapenda sana, nilikaribishwa ndani, kulikuwa Kuna seble kubwa Sana yaani sijui niseme Kama kwa wahindi, pia sebleni nilikutana na wasichana wawili na mvulana mmoja, nikajisemea kimoyo moyo
" Huyu mama anawatoto wazuri na wote amewapa maisha mazuri "
Maana walikuwa wamependeza Sana na ukiangalia simu zao Ni za Bei Sana nilifika na kuwasalimia, waliitika kwa furaha sana, nikatabasamu
Moja kwa moja nikapelekwa kwenye chumba kizuri kilikuwa na kila kitu yaani nguo sijui vipodozi yaani kila kitu Ni full.
" Umesema unaitwa Nani binti...??"
"Oooh naitwa saada mama "
" Oooh jina zuri lakini usiniite mama niite madam Grace nitafurahi Zaidi "
"Sawa"
"Utaoga Kisha utachagua nguo hapo utavaa ukimaliza utashuka chini ukapate chakula nitawaambia wakuandalie chakula "
"Shukran madam Grace Mungu akubariki"
Nilimshukuru sana, mwisho aliondoka na kuniacha mwenyewe nikaanza kuangalia nguo aiseee Ni mavazi yangu Yale niyapendayo, lakini kwakuwa nilikuwa mgeni niliogopa kuyavaa nikachukua gauni ambalo lilikua Ni refu nikavaa.
Majila ya usiku niliitwa sebleni kwaajili ya utambulisho, nilistuka kukuta wasichana wapatao Kama 20 na kitu hivi na wavulana kidogo nilibaki nikijiuliza maswali mengi
"Saada mbona unaogopa BINTI yangu eeeh njoo karibu yangu "
Alizungumza madam Grace nikakaa karibu yake
" Hello guys najua mmeshinda poa kabisa weekend imeenda vizuri SI ndio....??"
Wote wakaitika kwa pamoja nilibaki nikiangalia
"Meet saada she's our new girl atakuwa na sisi hapa kuanzia Leo na kuendelea, naomba tumpokee na kushirikiana nae, kauli mbiu yetu Ni ile ile upendo kwetu sote,"
Akanigeukia Mimi Kisha akasema
" Saada hii ndo familia yako mpya watakupenda na utaishi kwa amani Sana sawa..."
"Sawa madamu nashukuru kuwafahamu "
"Kila mtu utamjua kidogo kidogo kwa majina na Mambo mengine, Betty utakuwa karibu na saada utamfundisha kila kitu Cha hapa na utalalane chumba kimoja "
"Sawa madam"
Kila mtu akaondoka na kuendelea na harakati zao nilitamani Sana kujua inawezekanaje mtu kuwa na watoto wengi vile na awamuiti mama wote Ni maadam.
Asubuhi namapema niliamka kila mtu alikuwa bize na kazi zake, Betty akanifuata na kuniambia
" Leo kazi yetu Ni jikoni utakuwa unafanya ninachofanya Mimi sawa...??"
"Sawa..."
Tukaelekea jikoni na kuanza kusafisha, lakini Bado nilitaka kujua undani wa nyumba hiyo nikauliza
"Hivi kwanini Kuna watu wengi Sana hapa ??"
"Muda sahihi ukifika utajua focus na kazi acha umbea"
Betty alionekana kuwa serious Sana na alikuwa akiaminiwa Sana na madam grace, baada ya muda niliona gari ikiingia ndani umo ilikuwa ya kifahari Sana alishuka mkaka mzuri Sana nikajisemea kimoyo moyo
"Umu ndani Kuna wakaka wazuri mno wataniua Mimi jamani "
Muda huo huo madam alikuja na kumuita Betty nilitamani sana kujua wanaongea Nini lakini sikuweza.
Baada ya lisaa limoja nilikuwa nimemaliza kila kitu nilitoka jikoni na kutaka kuelekea chumbani nikakutana na mkaka yule mtanashati aliyeingia na gari ya kifahari akiwa na madam
"Madam grace aisee Hawa mabinti wako wako vizuri huyu wa leo akenifurahisha huduma nzuri Sana "
Alizungumza hivyo lakini nilibaki njia panda Wala sikuelewa wanaongea kuhusu Nini niliwasalimia na kuanza kuondoka
"Woooooow madam Grace huyu mpya Nini ...??"
Nilisikia mkaka yule akiuliza
",Ndio amekuja Jana tu hapa Nampa wiki mbili za kumuweka sawa wiki ya tatu anaanza kazi "
"Mbona hapo tu anamuonekano mzuri tu, jamani nasi me na booking kabisa niwe wa kwanza"
"Sawa mtu na pesa zako."
Nilisikia maongezi hayo nikawa na vitu kibao vya kufikilia kichwani lakini sikuwa na majibu, nikiwa naingia chumbani alikuja makaka na kunisalimia
"Hi saada, am Benny "
Alijitambulisha, nikatabasamu na kumpa mkono
"Kama hautakuwa na kazi unaweza kunipa kampani maana Sina Cha kufanya naenda nje kupunga upepo"
Alizungumza
"Oooh sawa ngoja nioge nijiweke sawa nitakuja "
Kisha nikaingia ndani nikaoga na kuanza kuchagua nguo
"Aaaah bhana weh nimechoka kuziangalia hizi nguo me navaa mapigo yangu yale, maana daah nimeyakumbuka "
Nikavaa kapensi keupe na cloptop ya njano ambayo iliacha kitovu nje ukizingatia nilikuwa na flat tammynq rangi yangu ya ngozi ukiipaka mafuta inakuwa na shukurani, nikapaka na make up simple nikajiangalia kwenye kioo nikasema
"Bingooo, huyu ndo saada Sasa"
Nikatoka nje kwa mwendo wa madaa nikaacha kuigiza kama mtu mshamba nikaona ngoja niwaoneshe Mimi Ni nani.
Wa kwanza kukutana nae nje alikuwa Ni madam Grace all shangaa Sana alibaki akiniangalia akiwa ameachia mdomo, niliachia bonge la tabasamu hakuwa na neno kabisa, kwakuwa tulishasalimiana nikampita shaaaaa yaani Kama tumezoeana Sana alibaki akinishangaa akuamini kabisa, nilipokotoka mlango mkubwa kila mtu alikuwa akiniangalia na asiamini Kama Ni Mimi ule mwendo tabasamu shape langu ambalo nilikuwa najua kulitumia kila mtu alibaki mdomo wazi, nikaita
"Benny........."
ITAENDELEA........
Umesoma kwa utulivu ยท dakika chache tu Asante Endelea kusoma chagua hapo chini
Umependezwa ?? Asante Soma Zaidi forgive-me-mom-nisamehe-mama-sehemu-ya