VYOTE NDANI GONGA94
FORGIVE ME, MOM ππ NISAMEHE MAMA SEHEMU YA: 14
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
SONGA NAYO...............
Kila mtu alistuka baada ya kuona jeneza likishushwa, watu walianza kulia bila kujua lilikuwa jeneza la nini au limembeba nana wakati huo nilikuwa nimemshika mwanangu nikijiambia tuliza akili hakuna kibaya kimetokea tulia, nikiwa naendelea kujipa moyo baba mkwe alinisogelea na kumchukua mtoto kisha kuniambia pole sana, nilihisi kuchaganyikiwa yaani kweli Benny leo analetwa akiwa kwenye jeneza, nilishazoea aje nimpokee acheze na mtoto wake.
Sikumbuki ilikuwaje nilikuja kuamka nikiwa kitandani kwangu pembeni alikuwako wifi yangu vero akiwa amevalia mavazi meusi na Mimi nilikuwa nimevikwa mavazi meupe,
"Bella Yuko wapi ...??"
Nilimuuliza Vero
"Yupo na mama kule nje unajisikiaje....??"
" Kidogo afadhali, Benny Yuko wapi ajarudi tuuu ??"
Wifi Vero aliinuka na kunikumbatia Vero alilia Sana hapo nikakumbuka Mara ya mwisho mwili wa Benny ulikuwa umeingizwa ndani akiwa kwenye jeneza na ulikuwa umeharibika Sana baada ya kugongwa na gari kubwa ambalo lilivamia duka letu la nafaka, nilipoteza mume na duka ambalo lilikua likiendesha maisha yangu ya mume wangu pamoja na Bella wetu.
Nikamuomba wifi atoke nje na aniache peke yangu , nilikwa ndani siku hiyo sio kawaida nilikuwa nasali muda wote na kuomba msamaha, kwa niliyoyatenda nyuma niliona kabisa naadhibiwa kwa unyama ambao nilikuwa nimeutenda kipindi kirefu kilichopita, baada ya muda bellah aliletwa ndani na mama mkwe, niliona mama mkwe anamaumivu makali Sana akutaka hata kuniangalia akaondoka baada ya kumuweka bellah kitandani nilimuita
" Mama....."
" Ishia hapo hapo eti mama kama uliweza kumuita mama yako shangazi unawezaje kuniita Mimi mama mtoto nuksi wewe nilikuwa nakusubili kwa hamu Sana , nuksi zako umemletea mwanangu uoni aibu wewe eeeh "
Aliongea kwa hasira Sana Kisha akanitupia daftari langu ambalo nilikuwa nimeandika historia yangu niliogopa Sana nilijiuliza maswali mengi Nini hatima yangu baada ya mama kujua haya juu yangu je nitaendelea kuishi hapa au ndio nitafukuzwa kama mbwa ? Nililia uku nikimuangalia bellah wangu ambaye alikuwa aelewi chochote
Majila ya saa kumi tulielekea makaburini kwaajili ya kumpumzisha Benny nyie sio Siri nilikuwa nalia na kuzimia mda wote, uwepo wa Benny kwangu ndio ulikuwa kila kitu kwa kipindi hiko, baada yamazishi tulirudi nyumbani nikajifungia ndani na bellah wangu mda wote naangalia picha za Benny anaangalia video ambazo nilikuwa nikijirekodi na Benny nilitamani iwe ndoto na niamke pembeni nimkute Benny akiwa amelala lakini haikuwa hivyo π Nina makosa sawa lakini kwani sistahili msamaha ?? Kwani ukiwa mkosefu ndio utakiwa kuwa na furaha jamani ? Kwani ukiwa una makosa ndio watu wakutenge mbona Benny alinipenda sana , kwani Benny sio binadamu Kama binadamu wengine jamani.
Baada ya wiki mbili kupita nikiwa nje nafua alikuja Amina nilimsalimia Kama kawaida lakini aliishia kunisukuma tu mpaka nikaanguka chini,
"Una Nini Amina we shida yako Nini niache Basi siko sawa "
" Unaanzaje kuwa sawa muuwaji mkubwa wewe Benny wangu angenisikiliza mpaka Leo angakuwa anaishi "
Nilipata hasira hizo nikasema huyu Sasa tunazidi kuzoeana na anavuka mipaka, nikamrukia nilimpiga siku hiyo nilimpiga yaani nilikumbuka mateso yote ninayopitia hasira zikaishia kwake, kwakuwa watu wa nyumbani walikuwepo walikuja na kuamua ugomvi
"Mmmmh huyu ndo mfiwa huyu ndo mke ambaye tunaamini kuwa na maumivu juu ya kifo Cha mume wake SI ndio , nimesema huyu mwanamke simtaki umu ndani "
Alizungumza mama mkwe akiwa analia, yaani aliona Mimi ndio mkosaji hakutaka kuulia Nini kilitokea nilio a Sasa Ni too much wacha niondoke tu Sina namna Sina jinsi Bora nikatafute maisha Kama Mungu amepanga niteseke Basi Ni sawa tu kuliko kubaki umo ndani ambapo nilikuwa naambiwa kuwa nimemuuwa benny, yaani tangu kifo Cha Benny baba mkwe na Vero tu ndio walikuwa wakinielewa lakini wengine wote walikuwa maadui kwangu hata wifi yangu mkubwa ambaye alitoka mwanza na kuja kwaajili ya mazishi alinichukiw ingawa hakuwai kukaa na Mimi , niliingia ndani na kupaki mabegi yangu , nilichukua Simu na kumpigia dereva ambaye tulikuwa tukimtumia kubeba nafaka kupeleka dukani.
Baba mkwe akaingia chumbani kwangu na kuzungumza na Mimi
" Mwanangu hala ya Sasa naona Hapa mtaumizana kabisa na uvumilivu unanishinda Mimi yaani nimetoka kumzika mwanangu lakini madrama kila siku nachoka kweli, Sasa naomba ukakae mijini kule Kuna mtu utakutana nae atakupigia atakupeleka sehemu nzuri naomba ubebe kila kitu kilichomo umu, maana ulileta wewe ukiwa na Benny sawa "
Nilimuelewa Sana baba na kukubali, yeye na wifi Vero wakanisaidia kutoa viti nje ingawa bado ilileta maneno kwanini niondoke na vitu vya Benny lakini baba mkwe alinitetea kwa kusema Ni kwaajili ya kusaidia malezi ya Bella, kwakuwa hata mama mkwe alikuwa akimpenda Bella alikubali ingawa sikujua ni kweli au shingo upande.
Gari ilifika na nikaiaga familia ile na kuondoka, nilikuwa nikilia mwanzo was Safari mpaka nilipofika kwenye nyumba ambayo baba alinielekeza, kulikuwa Ni mjini lakini Ni uswazi Sana kwanza hiyo nyumba yenyewe nilikuta wasichana Kama nane wamekaa nje wanapiga umbea.
Nilishusha vitu na kuanza kupanga bila kupumzika, uku Bella nikiwa nimembeba mgongoni, mmoja Kati ya wale wasichana aliinuka na kuja kunipokea Bella nilimshukuru sana.
Siku mbili zilipita nilianza hata kuwa mwenyeji ingawa nilikuwa mtu mwenye mawazo Sana, kumbukumbu kuhusu Benny azikuweza kufutika kichwani mwangu.
Nilikuwa na pesa kiasi nilibaki nazo nikaona hizi nikikaa hivi hivi zitaisha na sitakuwa na kitu Cha kufanya kilichokuwepo Bora nianzeshe biashara, nikafungua genge kwani nilikuwa na uzoefu nao, katika wasichana wote nilizoeana na mmoja tu ambaye alionekana simple Sana kuliko wengine na ndio alikuwa ata akinisaidia kumbeba Bella
"Dada saada mama alikuwa amekaa na bellah amesema umepeleke hospital maana joto lake sio la kawaida "
Sikutaka kusubili niliogopa Sana maana Bella ndio familia pekee niliyokuwa nayo karibu, nikajiandaa na Moja kwa Moja tukaenda hospital alipimwa na kuonekana kuwa anahoma Kali Sana na nimonia ilikuwa ikimshika polepole, hivyo tukapewa kitanda kwaajili ya uangalizi zaidi, Mambo yalizidi kuwa magumu nilitumia pesa nyingi Sana kumuuguza bellah uku nyumbani biashara ya genge ilisimama kabisa nilihisi kuvurugwa yaani
Baada ya wiki mbili niliruhusiwa kurudi nyumbani hapo Sina hata Mia mkononi, maana hata kurudi kutoka hospital nilitembea mpaka nyumbani, kipindi chote nilichokuwa hospital hakuna ahata mmoja kutoka katika familia ya Benny ambaye alikuja ingawa niliwapa taarifa za ugonjwa, niliporud pia nilimtafuta baba lakini haupatikana , nilipompigia wifi Vero alikata Kisha kuzima simu kabisa
" Sasa Ni Mimi na Bella tu Mungu tusimamie "
Niliona kabisa ndio tushatelekezwa, nishukuru Kodi nililipa ya miezi sita lakini niliwaza ikiisha je ? Ukiachana Kodi nitakula Nini na Bella atanyonyaje Kama Mimi sili kichwa kilikuwa kinapata moto tu, hapo nilikumbuka mama alivyokuwa akiangaika kwaajili yetu lakini niliona afanyi kitu.
Maisha yalibadilikq yakawa ya shida, ili kupata hela ya kula nikaanza kuuza vitu vyangu vya ndani na kununua chakula na kuweka ndani niliuza kabati la nguo na dressing table, hapo kidogo nilikuwa na chakula Cha kutosha , ingawa Bella alikuwa ajafikisha miezi sita niliamua kumuanzishia uji tu niliona kuwa maziwa yangu ayamtoshi.
Nakumbuka siku Moja nilikuwa nimekaa kibalazani peke yangu mda huo Bella alikuwa ameondoka na fatuma lilikuja gari zuri la kifahari na kupaki pale nje, nilistuka kwani nililipita honi.
Akashuka mbaba wa makamo, akiwa amembeba Bella nilishtuka inakuwaje Bella Yuko na huyu ikiwa aliondoka na fatuma
"Habari......"
Alinisalimia baba huyo ndipo nikatoka kwenye butwaa na kumjibu
" Salama , eeeh baba namuomba mwanangu kwanza "
"Tulia kwanza kwahiyo wewe ndio saada SI ndio au wewe ndio mama bellah??"
" Ndio Ni mimi, Nini kimetokea fatuma yuko wapi....?"
"Funga mdomo wako uko unakuwa Kama ujielewi we mwanamke wa aina gani eeeh unamtumia mdogo wako na mtoto wako kuomba omba ili mpate hela ukiwa wewe umelala......."
Nilistuka hatari......
ITAENDELEA.....
FORGIVE ME, MOM ππ
Kila mtu alistuka baada ya kuona jeneza likishushwa, watu walianza kulia bila kujua lilikuwa jeneza la nini au limembeba nana wakati huo nilikuwa nimemshika mwanangu nikijiambia tuliza akili hakuna kibaya kimetokea tulia, nikiwa naendelea kujipa moyo baba mkwe alinisogelea na kumchukua mtoto kisha kuniambia pole sana, nilihisi kuchaganyikiwa yaani kweli Benny leo analetwa akiwa kwenye jeneza, nilishazoea aje nimpokee acheze na mtoto wake.
Sikumbuki ilikuwaje nilikuja kuamka nikiwa kitandani kwangu pembeni alikuwako wifi yangu vero akiwa amevalia mavazi meusi na Mimi nilikuwa nimevikwa mavazi meupe,
"Bella Yuko wapi ...??"
Nilimuuliza Vero
"Yupo na mama kule nje unajisikiaje....??"
" Kidogo afadhali, Benny Yuko wapi ajarudi tuuu ??"
Wifi Vero aliinuka na kunikumbatia Vero alilia Sana hapo nikakumbuka Mara ya mwisho mwili wa Benny ulikuwa umeingizwa ndani akiwa kwenye jeneza na ulikuwa umeharibika Sana baada ya kugongwa na gari kubwa ambalo lilivamia duka letu la nafaka, nilipoteza mume na duka ambalo lilikua likiendesha maisha yangu ya mume wangu pamoja na Bella wetu.
Nikamuomba wifi atoke nje na aniache peke yangu , nilikwa ndani siku hiyo sio kawaida nilikuwa nasali muda wote na kuomba msamaha, kwa niliyoyatenda nyuma niliona kabisa naadhibiwa kwa unyama ambao nilikuwa nimeutenda kipindi kirefu kilichopita, baada ya muda bellah aliletwa ndani na mama mkwe, niliona mama mkwe anamaumivu makali Sana akutaka hata kuniangalia akaondoka baada ya kumuweka bellah kitandani nilimuita
" Mama....."
" Ishia hapo hapo eti mama kama uliweza kumuita mama yako shangazi unawezaje kuniita Mimi mama mtoto nuksi wewe nilikuwa nakusubili kwa hamu Sana , nuksi zako umemletea mwanangu uoni aibu wewe eeeh "
Aliongea kwa hasira Sana Kisha akanitupia daftari langu ambalo nilikuwa nimeandika historia yangu niliogopa Sana nilijiuliza maswali mengi Nini hatima yangu baada ya mama kujua haya juu yangu je nitaendelea kuishi hapa au ndio nitafukuzwa kama mbwa ? Nililia uku nikimuangalia bellah wangu ambaye alikuwa aelewi chochote
Majila ya saa kumi tulielekea makaburini kwaajili ya kumpumzisha Benny nyie sio Siri nilikuwa nalia na kuzimia mda wote, uwepo wa Benny kwangu ndio ulikuwa kila kitu kwa kipindi hiko, baada yamazishi tulirudi nyumbani nikajifungia ndani na bellah wangu mda wote naangalia picha za Benny anaangalia video ambazo nilikuwa nikijirekodi na Benny nilitamani iwe ndoto na niamke pembeni nimkute Benny akiwa amelala lakini haikuwa hivyo π Nina makosa sawa lakini kwani sistahili msamaha ?? Kwani ukiwa mkosefu ndio utakiwa kuwa na furaha jamani ? Kwani ukiwa una makosa ndio watu wakutenge mbona Benny alinipenda sana , kwani Benny sio binadamu Kama binadamu wengine jamani.
Baada ya wiki mbili kupita nikiwa nje nafua alikuja Amina nilimsalimia Kama kawaida lakini aliishia kunisukuma tu mpaka nikaanguka chini,
"Una Nini Amina we shida yako Nini niache Basi siko sawa "
" Unaanzaje kuwa sawa muuwaji mkubwa wewe Benny wangu angenisikiliza mpaka Leo angakuwa anaishi "
Nilipata hasira hizo nikasema huyu Sasa tunazidi kuzoeana na anavuka mipaka, nikamrukia nilimpiga siku hiyo nilimpiga yaani nilikumbuka mateso yote ninayopitia hasira zikaishia kwake, kwakuwa watu wa nyumbani walikuwepo walikuja na kuamua ugomvi
"Mmmmh huyu ndo mfiwa huyu ndo mke ambaye tunaamini kuwa na maumivu juu ya kifo Cha mume wake SI ndio , nimesema huyu mwanamke simtaki umu ndani "
Alizungumza mama mkwe akiwa analia, yaani aliona Mimi ndio mkosaji hakutaka kuulia Nini kilitokea nilio a Sasa Ni too much wacha niondoke tu Sina namna Sina jinsi Bora nikatafute maisha Kama Mungu amepanga niteseke Basi Ni sawa tu kuliko kubaki umo ndani ambapo nilikuwa naambiwa kuwa nimemuuwa benny, yaani tangu kifo Cha Benny baba mkwe na Vero tu ndio walikuwa wakinielewa lakini wengine wote walikuwa maadui kwangu hata wifi yangu mkubwa ambaye alitoka mwanza na kuja kwaajili ya mazishi alinichukiw ingawa hakuwai kukaa na Mimi , niliingia ndani na kupaki mabegi yangu , nilichukua Simu na kumpigia dereva ambaye tulikuwa tukimtumia kubeba nafaka kupeleka dukani.
Baba mkwe akaingia chumbani kwangu na kuzungumza na Mimi
" Mwanangu hala ya Sasa naona Hapa mtaumizana kabisa na uvumilivu unanishinda Mimi yaani nimetoka kumzika mwanangu lakini madrama kila siku nachoka kweli, Sasa naomba ukakae mijini kule Kuna mtu utakutana nae atakupigia atakupeleka sehemu nzuri naomba ubebe kila kitu kilichomo umu, maana ulileta wewe ukiwa na Benny sawa "
Nilimuelewa Sana baba na kukubali, yeye na wifi Vero wakanisaidia kutoa viti nje ingawa bado ilileta maneno kwanini niondoke na vitu vya Benny lakini baba mkwe alinitetea kwa kusema Ni kwaajili ya kusaidia malezi ya Bella, kwakuwa hata mama mkwe alikuwa akimpenda Bella alikubali ingawa sikujua ni kweli au shingo upande.
Gari ilifika na nikaiaga familia ile na kuondoka, nilikuwa nikilia mwanzo was Safari mpaka nilipofika kwenye nyumba ambayo baba alinielekeza, kulikuwa Ni mjini lakini Ni uswazi Sana kwanza hiyo nyumba yenyewe nilikuta wasichana Kama nane wamekaa nje wanapiga umbea.
Nilishusha vitu na kuanza kupanga bila kupumzika, uku Bella nikiwa nimembeba mgongoni, mmoja Kati ya wale wasichana aliinuka na kuja kunipokea Bella nilimshukuru sana.
Siku mbili zilipita nilianza hata kuwa mwenyeji ingawa nilikuwa mtu mwenye mawazo Sana, kumbukumbu kuhusu Benny azikuweza kufutika kichwani mwangu.
Nilikuwa na pesa kiasi nilibaki nazo nikaona hizi nikikaa hivi hivi zitaisha na sitakuwa na kitu Cha kufanya kilichokuwepo Bora nianzeshe biashara, nikafungua genge kwani nilikuwa na uzoefu nao, katika wasichana wote nilizoeana na mmoja tu ambaye alionekana simple Sana kuliko wengine na ndio alikuwa ata akinisaidia kumbeba Bella
"Dada saada mama alikuwa amekaa na bellah amesema umepeleke hospital maana joto lake sio la kawaida "
Sikutaka kusubili niliogopa Sana maana Bella ndio familia pekee niliyokuwa nayo karibu, nikajiandaa na Moja kwa Moja tukaenda hospital alipimwa na kuonekana kuwa anahoma Kali Sana na nimonia ilikuwa ikimshika polepole, hivyo tukapewa kitanda kwaajili ya uangalizi zaidi, Mambo yalizidi kuwa magumu nilitumia pesa nyingi Sana kumuuguza bellah uku nyumbani biashara ya genge ilisimama kabisa nilihisi kuvurugwa yaani
Baada ya wiki mbili niliruhusiwa kurudi nyumbani hapo Sina hata Mia mkononi, maana hata kurudi kutoka hospital nilitembea mpaka nyumbani, kipindi chote nilichokuwa hospital hakuna ahata mmoja kutoka katika familia ya Benny ambaye alikuja ingawa niliwapa taarifa za ugonjwa, niliporud pia nilimtafuta baba lakini haupatikana , nilipompigia wifi Vero alikata Kisha kuzima simu kabisa
" Sasa Ni Mimi na Bella tu Mungu tusimamie "
Niliona kabisa ndio tushatelekezwa, nishukuru Kodi nililipa ya miezi sita lakini niliwaza ikiisha je ? Ukiachana Kodi nitakula Nini na Bella atanyonyaje Kama Mimi sili kichwa kilikuwa kinapata moto tu, hapo nilikumbuka mama alivyokuwa akiangaika kwaajili yetu lakini niliona afanyi kitu.
Maisha yalibadilikq yakawa ya shida, ili kupata hela ya kula nikaanza kuuza vitu vyangu vya ndani na kununua chakula na kuweka ndani niliuza kabati la nguo na dressing table, hapo kidogo nilikuwa na chakula Cha kutosha , ingawa Bella alikuwa ajafikisha miezi sita niliamua kumuanzishia uji tu niliona kuwa maziwa yangu ayamtoshi.
Nakumbuka siku Moja nilikuwa nimekaa kibalazani peke yangu mda huo Bella alikuwa ameondoka na fatuma lilikuja gari zuri la kifahari na kupaki pale nje, nilistuka kwani nililipita honi.
Akashuka mbaba wa makamo, akiwa amembeba Bella nilishtuka inakuwaje Bella Yuko na huyu ikiwa aliondoka na fatuma
"Habari......"
Alinisalimia baba huyo ndipo nikatoka kwenye butwaa na kumjibu
" Salama , eeeh baba namuomba mwanangu kwanza "
"Tulia kwanza kwahiyo wewe ndio saada SI ndio au wewe ndio mama bellah??"
" Ndio Ni mimi, Nini kimetokea fatuma yuko wapi....?"
"Funga mdomo wako uko unakuwa Kama ujielewi we mwanamke wa aina gani eeeh unamtumia mdogo wako na mtoto wako kuomba omba ili mpate hela ukiwa wewe umelala......."
Nilistuka hatari......
ITAENDELEA.....
FORGIVE ME, MOM ππ
Umesoma kwa utulivu Β· dakika chache tu Asante Endelea kusoma chagua hapo chini
Umependezwa ?? Asante Soma Zaidi forgive-me-mom-nisamehe-mama-sehemu-ya