VYOTE NDANI GONGA94
MPISHI ANA UTAMU WAKE 9 na 10
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
SEHEMU YA 9
Wacha nitoe macho moyo ukitaka kunitoka kila nikitazama namna panga lilivyo kali kupitiliza.
" Ni nimemaanisha unavutia mtukufu malkia " nikaona nijitetee sikutaka mambo mengi.
" Mpe uhuru malkia wangu, nahitaji kuonja chakula chake siku ya leo " alizungumza mfalme huku akinitazama, sikukawia niliinama chini kuomba rehema.
Namna bahati ilikuwa upande wangu, ombi la mfalme lilitimizwa.
" Nifuate nahitaji kukupeleka jikoni haraka " alizungumza malkia huyo, ni binti wa rika langu si ajabu nimemzidi urembo ni vile tu sina matunzo, sikuacha kujisemea kila jicho langu la kushoto lilipomtazama malkia huyo, nilipohisi atanigundua niliagaza pembeni na kuinamisha uso chini.
" Zama ndani "
" Sawa mtukufu "
" Ni jiko huru na la kisasa la ajabu, lina kila kitu utakachokihitaji kupikia, kuna tanuru na kila kitu anza kazi " alizungumza malkia huyo huku akikaa pembeni na kunitazama.
" Siamini kama makaa ya mawe ni jiko la kisasa, sioni oven wala microwave sidhani kama kuna umeme mahala hapa " nilisema kichinichini.
Nilipokumbuka nipo chini ya uangalizi nikaongeza umakini kisha nikaanza kazi.
" Wali nyama,nitaandaa " nilizungumza huku nikianz kupika.
Ilichukua saa tu kumaliza mapishi hayo.
Japo sikumuita, malkia alinyanyuka kuja kuangalia chakula changu.
Sikuelewa ni dharau au nini, binti huyo mrembo kiasi alionekana kusikitika.
" Beba nifuate " kwa haraka nilibeba msosi na kunfuata.
Tulipofika chumbani kwa mfalme niliomba rehema ya kumuangalia usoni, aliponiruhusu nilinyanyuka na kuingia sambamba na malkia.
" Mmmmh makubwa mbona haya " nilijikuta nikizungumza.
Nyie sawa ni mapenzi, siamini kama wawili hawa wanaweza kunyanduana mbele yangu ilihali nimeleta chakula mahala hapa.
Basi nikaanza kujikoholesha lengo wakumbuke uwepo wangu.
" Ni kitamu hatari sijawahi onja pishi hili " alizungumza malkia... mfalme mpuuzi alibaki akitikisa kichwa tu bila kusema neno lolote.
haikuchukua muda, lango la mfalme liligongwa.
“Mtukufu malkia, mama mfalme anaomba kukuona " alizungumza kijakazi huyo.
Huenda malkia huyo anaogopwa, kwa namna malkia huyu alivyokurupuka punde alipisikia jina hilo lilinifanya nicheke, japo nilijikaza nisitambulike.
" Chakula chako ni kitamu mno japo hakijafikia utamu wako " alinena mfalme punde malkia alipoondoka.
Sikuwa na jibu nilibaki nikiduwaa.
Endelea kufuatilia.
SEHEMU YA 10
Waweza kunieleza nini uliiweka kwenye nunu yako ewe mlimbwende ? Aliuliza mfalme huyo mpuuzi.
Huwa namuita hivyo kwani siamini kama anastahili cheo hiko kabisa, ni kama mvulana asiyejielewa wala nini anaendeshwa na mihemko tu.
" nNona una yako unayoniwazia, usihofu nitakuwa na wewe usiku wa leo " nikiwa naduwaa sauti ya mfalme ilisikika.
Upande wa malkia na mama wa mfalme sauti ya kufoka inasikika.
" Ina maana nimekosea kukuchagua sio ? Ni binti gani usiyeweza kumshawishi mwanaume kwa kiasi hiki ? Si ajabu umeshindwa kumvuta akulale kwenye siku za hatari ni salama tu " alizungumza malkia huyo mama wa mfalme aliyejulikana kama Dorica.
" Nisamehe mama nitajitahidi " alijibu malkia.
" Si mara ya kwanza kuomba hilo, hakuna mabadiliko ya maombi yako, usiku wa leo ni nafasi yako ya mwisho kumtega mfalme, nimezungumza na mganga mkuu wa ikulu kanieleza leo upo kwenye siku ya hatari, ni rahisi kunasa mimba usiku wa leo hivyo usiniangushe " alizungumza malkia huyo...ni mzuri sana wa sura ila mgumu wa roho kama vandame.
" Sawa mama " malkia huyo aliitikia kisha akaondoka.
" Waita wewe ! !! " Aliita malkia docas.
" Abee mama "
" Usiniangushe sawa ? "
" Sawa mama " akajibu waita kisha akaondoka mahala hapo.
Sasa sijui itakuwaje wajameni..... huyu mfalme huyu sijui atajigawaje aiseee.....aje kwangu aninyandue au alale kwa mkewe..... mimi na wewe hatujui wadau wangu.
Endelea nakuja
Umesoma kwa utulivu · dakika chache tu Asante Endelea kusoma chagua hapo chini
Umependezwa ?? Asante Soma Zaidi mpishi-ana-utamu-wake

