VYOTE NDANI GONGA94
MPISHI ANA UTAMU WAKE 13&14
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
SEHEMU YA 13
" Amka buana, haifai wewe kulala kwenye chumba cha kijakazi kama mimi " nilizungumza huku nikimtikisa mfalme aamke.
Nilipoona haamki nilihitaji kutumia njia ya ziada kumtoa mahala hapa.
" Mama Dorcas nimekuletea habari njema sana siku ya leo" alizungumza mtabiri mkuu wa ikulu akiwa mbele ya malkia mkuu.
Kwa namna wanavyoongea waweza sema wana mazoea ya muda mrefu sana, si kawaida kwa kijakazi wa kifalme kunyanyua uso pale anapoongea na malkia.
Upande mwingine za ndani, malkia Dorcas mara kwa mara huonekana usiku kwenye kasri la mtabiri mkuu si haba wanakulana siri kwa siri.
" Ni zipi hizo, masikio yangu yana tamani kuzisikia " alijibu malkia Dorcas.
" Ni siku za usoni mfalme atapata mrithi wa kiti chake .. " alizungumza mtabiri kisha akaweka pause.
Wacha malkia Dorcas afurahie, ni muda sana alikuwa anataka mjukuu japo waita hakufanikiwa kumpatia hilo.
Furaha yake ilienda mbali, akajikuta akimkumbatia mtabiri mkuu kinyume na makubaliano yao.
" Sijamaliza mtukufu malkia kuna habari zishangazazo "
" Ni zipi hizo "
" Ni kwamba mwanamke huyo si malkia waita.... "
" Nini enheee jingine ? "
" Ni kwamba mimba yake itahatibika siku ya leo kama hatutazuia vurunguti hilo " akamaliza mtabiri mkuu kunena.
Malkia forcas si mzembe kama anavyoonekana, mgongo wa mtabiri mkuu ulikuwa ngazi zake, alimpita kama hewa.
Kituo cha safari yake ilikuwa ni chumbani kwa binti Amara.
Upande mwingine anaonekana malkia waita akitembea kwa jazba kuelekea chumbani kwa binti Amara.
Haijulikani nini kitajiri zaidi endelea kufuatilia mdau wangu.
SEHEMU YA 14
Nikiwa chumbani kwangu, nikihangaika kumuamsha mfalme sina hili wala lile .
" Ananikera sana huyu mpuuzi, kwanza siamini kama ananila kirahisi namna hii ni mara ya pili sasa sielewi ni wapi ananishika mpaka nalainika namna hii, sawa ni mfalme ila sipaswi kumpa mwili wangu kizembe namna hii ukizingatia sifahamu ni wapi nimetokea, wazazi wangu ama familia yangu katika nchi hii, vipi kama akinisababishia matatizo mtu huyu ? " Nilijikuta nikianza kulalamika.
Nikiwa nawaza yangu huku macho yangu yakimtazama mfalme aliye jiachia sana juu ya kitanda nipumzi chasho mwili wangu ghafla nikasikia mlango ukifunguliwa.
" Ni nini tena ? " Nikajiuliza.
Nikajikuta nikiruka kitandani mithili ya spiderman, mikoni yangu ikatua kwenye sakafu za mbao huku kichwa changu kikielekea chini.
" Naomba rehema yako malkia wangu sikudhamiria kufanya hili " nilizungumza.
" Ingekuwa busara sana kama ungemsitiri kwanza mwanangu, nafahamu kuwa unampa kile asichokipata kwa waita ndomana ananogewa namna hii japo nimechukizwa sina budi kukubali " alizungumza malkia huyo.
Basi nikanyanyuka kumsitiri mfalme, hakuwa mtupu kama mnavyofikiria ni vile maumbile yake yalijichora kutikana na vazi jeupe na jepesi alilolivaa mithili ya sanda .
" Nifuate " alizungumza malkia Dorcas nami nikamfuata.
Kwanza mnajua ilikuwaje? mpaka malkia waita hakufika kwenye chumba changu ilihali alionekana akija huku kwa jazba .
Najua mna hamu ya kujua basi ngoja niwahadithie sasa.
Ilikuwa hivi, kama tulivyoona malkia mkuu ama Dorcas mzuri wa sura mkavu wa roho punde aliposikia utabiri ulivosema aligundua moja kwa moja huyo binti mjamzito ni Amara si mwingine na alipoambiwa mimba ya mfalme itaharibika siku hii alifahamu fika haitaharibiwa na mwingine zaidi ya malkia waita.
Hivyo akaamua kufunga safari kuja chumbani kwangu.
Kama alivyotegemea njiani akakutana na malkia waita akiwa kafura kweli kweli.
Imezoeleka kwa malkia waita kunywea mbele ya mkwe wake, hivyo alijikuta akielezea lile linalo msibu.
" Mama Jampio simuoni chumbani kwake na kama tulivyokubaliana ni lazima nishike minba siku ya leo, kuna kijakazi kanipa uelekeo wake hivyo nimeamua kumfata japo nina mashaka " Alizungumza malkia waita.
" Mashaka gani hayo ? " Aliuliza malkia Dorcas akiwa mkavu kama ndimu.
" Nina mashaka kuwa anatembea na mpishi mkuu " akajibu waita akiwa na uwoga machoni mwake .
" Naona ni muda umeanza kumvunjia heshima mumeo sasa, naona umesahau kuwa ni mfalme wa nchii hii, hebu rudi mara moja chumbani kwako nitahakikisha anakuja kulala nawe siku ya leo " alizungumza malkia Dorcas.
" Lakini mama !!! "
" Nafahamu una uhitaji wa mimba na kulinda cheo chako, niamini nitakusaidia katika hilo" alizungumza malkia Dorcas kisha akampa mgongo waita.
Alijikuta akiachia tabasamu la ushindi pale mpango wake ulipotiki kirahisi sana, uwoga na utii wa malkia waita ulikuwa ni nguvu kubwa ya ushindi machoni mwa malkia huyo.
Basi baada ya mazungumzo hayo, malkia waita akarudi kwenye kasri lake kisha malkia Dorcas akaja chumbani kwangu ambapo alifahamu fika ni nini kinaendelea au atakikuta.
Najua unahitaji kujua nini aliniutia muda ule.
Tukutane kipande kijacho, endelea kuwa na mimi.
Umesoma kwa utulivu ยท dakika chache tu Asante Endelea kusoma chagua hapo chini
Umependezwa ?? Asante Soma Zaidi mpishi-ana-utamu-wake

