VYOTE NDANI GONGA94
Story.....................MFALME KIPOFU 9
Usimulizi huu ni wa watu wazima. Chukua muda wako, tulia, kisha usome kwa utulivu kama machapisho yetu yanayoendelea moja kwa moja.
Ilipoishia sehemu iliyopita........
Mzee yule aliongea na kuondoka zake pamoja na mjukuu wake aliyekwisha kutibiwa na kuwacha Amma pamoja na baba yake katika maswali mengi yasiyo na majibu........
ENDELEA NAYO......
"Baba ivi umemuelewa yule mzee kanishika mkono na kuniangalia lakini cha ajabu kapiga magoti mbele yangu??"
"Binti yangu Amma huwezi jua hawa wazee wa zamani wanaona mambo mengi isivyo kawaida".
"Ni sawa baba lakini mimi naona kuna kitu ambacho itakuwa ameona kwangu na natamani nijue nikitu gani icho alichoona"
"Kila kitu kinakuja kwa sababu mda maalumu ukifika mambo yote yakuwa wazi binti yangu".
Amma aliona kuna kila sababu ya kufatilia kuona ni kitu gani kilichomfanya mzee yule aweze kupiga magoti baada ya kuutazama mkono wake.
Upande wa pili babu pamoja na mjukuu wake,
"Babu unajua umenishangaza sana wewe kupiga magoti mbele ya yule binti??"
"Huwezi kujua mjukuu wangu wewe bado mdogo"
"Mmmh sijaona cha ajabu alichonacho yule binti".
"Nyamaza kabisa yule ndio atakaye kuja kuwa malikia wa ADELI sikutaka kuongea mbele yao ila kwakuwa nipo na wewe ngoja nikuambie sasa"
"Mmmh babu bwana tangu lini ukawa mtabili wewe??".
"Ukikua utaelewa sasa ivi wewe baba mdogo".
"Sawa babu".
Ni mazungumzo ya mzee yule na mjukuu wake na hii ni baada ya kumpigia magoti Amma kitu kilichomshangaza mpaka mjukuu wake kwa kitendo alichokifanya mzee yule.
****************
Katika ufalme wa YUNDI leo ni sherehe ya kusherekea siku ya kuzaliwa kwa binti Mfalme aliyetambulika kwa jina la Princess Nailet,
Maonyesho na michezo mbalimbali ilikuwepo siku hiyo iliyowapendeza raia wengi katika ufalme ule na kuwafanya waone kama ni siku maalumu kwao,
Na raia wengi kusogea eneo la tukio kwa ajili ya kushuhudia maonyesho hayo.
Moja ya raia waliokuja kushuhudia maonyesho hayo ni Lindiwe pamoja na Prince Yao aliyekuwa haoni kinachoendelea ila mama yake mlezi Lindiwe alifanya kazi ya kumsimulia kila kilichokuwa kikiendelea pale.
Mfalme Tengu akiwa kama Mfalme wa YUNDI alisimama nakuanza kuongea mbele ya umati ule,
Watu wote walika kmya kumsikiliza mfalme wao aliyedumu kwenye uongonzi karibu miaka thelathini(30).
Lakini Princess Nailet katika kutazama umati wa watu uliofulika kushuhudia siku yake ile ndipo alipomuona Prince Yao akiwa amefungwa kitambaa machoni,
Nakumfanya kushangaa kidogo.
"Yule ni nani???,mbona kafungwa kitambaa machoni???,
alimuuliza mtumishi wake aliyekuwa nae karibu mtumishi alifata kidole cha Princess na kuelewa ni mtu gani aliyeulizwa.
"Yule ni kipofu".
Princess Nailet alimtazama kwa mara nyingine Prince Yao na hapo ndipo aliposhuhudia uzuri wa mwanaume yule licha upofu aliona nao.
"Sherehe ikiisha naomba unipeleke anapokaa"
"Sawa princess".
Sherehe ikiwa bado inaendelea katika ufalme huo wa YUNDI,
"Mama naomba tuelekee nyumbani sijisikii tena kuendelea kukaa hapa,Prince Yao aliongea na kumfanya Lindiwe afanye kile anachokitaka na safari ikaanza kuelekea katika makazi yao".
********************
Safari ilikuwa bado inaendelea ya asikari waliotumwa na Mfalme kwenda kumtafuta kijana na wanafanyikiwa kufika katika mipaka ya YUNDI,
"Nyie ni watu mnaotoka katika ufalme upi??,walinzi walinda mipaka waliwauliza asikari wale wa ADELI".
Hawakutaka maneno mengi walitoa barua maalumu waliyopewa na mfalme wao yenye mhuli na walipoisoma, waliwaruhusu kuingia katika ufalme wao.
"Sawa tumepita mipakani tunaanzia wapi sasa falme za watu hizi??, askari mmoja aliongea baada ya wao kufanyikiwa kufika katika ufalme wa YUNDI"
"Tupite huku tunaweza kupata tunachokitaka".
Walikubaliana na safari ikaanza kutafuta kilichowaleta katika falme hiyo.
Lindiwe anafanyikiwa kufika nyumbani akiwa na Prince Yao lakini alipogeuza shingo yake alishangaa kuona asikari wakipita wakiwa wamevaa nguo zilizowatambulisha kama asikari wa ADELI,
"Yao naomba ukae hapa nakuja sasa ivi tu"
"Aya mama".
Lindiwe alitoka nakuanza kuwafatilia kisirisiri asikari wale wa ADELI bira ya wao kujua ili ajue ni kitu gani kilichowaleta pale YUNDI.
Asikari wale wanakutana na Cheki kijana anayempenda binti Yunde na wana msimamisha,
"Habari yako "
"Salama sijui ni wasaidie nini???"
"Wew n mzaliwa wa falme hii tungependa kufahamu???"
"Ndio hamjakosea".
Walitazamana asikari wale nakupeana ishara ya kutoboa siri yao iliyo waleta pale.
"Kuna mpango ambao unaweza kubadilisha maisha yako".
Cheki baada ya kusikia mpango tena alitega masikio kwa umakini asikilize ni mpango gani huo.
Wale asikari walimweleza lengo kuu la wao kuja mpaka kwenye falme yao na kumwonyesha vipande vya dhahabu kama malipo ya awali endapo akikubali kufanya ile kazi.
Cheki hakutaka kuipoteza ile nafasi alikubali pasipo ata kufikili mara mbilimbili.
Maongezi yote yaliyokuwa yanaendelea pale Lindiwe alikuwa akisikia kila kitu..
"Hii haiwezekani yani mfalme ameamua aje amtafute Prince mwingine, hapana hii haiwezekani.........ITAENDELEA
Maamuzi gani atakayochukua Lindiwe baada ya kusikia kijana mwingine anatafutwa kwa ajili ya kuchukua nafasi ya Prince Yao???? na vip kuhusu Princess Nailet atafanyikiwa kwenda kumuona Prince Yao????, karibu katika hatua inayofata
Umesoma kwa utulivu · dakika chache tu Asante Endelea kusoma chagua hapo chini
Umependezwa ?? Asante Soma Zaidi story-mfalme-kipofu
Story.....................MFALME KIPOFU Sehemi..ya............08 Ilipoishia sehemu iliyopita........ "Tarifa gani???" "Inasemekana baada ya siku tatu Prince
Story.....................MFALME KIPOFU Sehemi..ya............04 Ilipoishia sehemu iliyopita........ Farasi ilifika Lindiwe pamoja na prince Yao walipanda na safari ikaanza kutoka katika jengo
Story.....................MFALME KIPOFU Ilipoishia sehemu iliyopita.. General Tengeli anataman kuwa mfalme na ndio sababu ilimfanya atengeneza jeshi
Story MFALME KIPOFU Sehemi..ya............02 Ilipoishia sehemu iliyopita... "Mbona unazunguka mtabili emu niambie mwanangu niliyemzaa leo anatatizo gani???