,, WATOTO MAPACHA
Sehemu ya """""1
Barozi wa Tanzania nchin Colombia Mr Benson alikuwa anawaza namna ya kumwambia mkewe atakapoamka ,kuwa mtoto wao amefariki. Kwa mala ya tatu mfululizo mkewe akipata ujauzito hiaribika ,au akifikisha muda wa kujifungua basi mtoto huyo hufariki hata kabla hajakaa hata lisaa limoja ,
Na ndivyo ilivyotokea siku hiyo
.
Mr Benson akapata wazo akawafuata manesi wa hospitali hiyo na kuwaambia atawapa milioni 20 cash ,wakimuibia mtoto hospitalin hapo na apewe mkewe kabla hajaamka yaani akistuka tu amkute mtoto pembeni yake,
Manes wawili wakakubali kufanya dili hilo ,
Siku hiyo hospitalin hapo palikuwa na mama mmoja mjamzito anaitwa Rebecca,
Nae alikuja kujifungua na kwa bahati nzuri yule Mama akajifungua MAPACHA.
Rebecca baada tu ya kujifungua alizimia akakimbizwa ICU ,
Wale manesi wakamchukua mtoto mmoja na kumuweka kwenye kitanda cha mke wa Mr Benson ,na katoto kengine wakaenda kukatupa dampo wakijua mpaka asubuhi katakuwa kamekufa,
""Tumeshamaliza kazi yako tumalizane bas,,"""!
Wale manes walimwambia Mr Benson
Mr Benson alifurahi sana baada ya kukaona katoto ka kike kapo pembeni ya mkewe.
Akatoa check ya milioni 30 akawapa wale manes ,
Mr Benson hakujua kuwa mtoto alieuziwa wamezaliwa Mapacha na mmoja alitupwa dampo kupoteza ushahidi.
Mke wa Mr Benson alipoamka akamuona mtoto pembeni yake ,alifurahi sana mpaka machozi yalimtoka kwa furaha ,bila kujua kuwa mtoto aliezaa alifariki na mtoto alienae mumewe alimnunua pesa ndefu na akamuwekea pale kitandan ili atakapoamka ajue ni mtoto aliemzaa,
Wakat mke wa Mr Benson anafurahi huku Rebecca analia ,baada ya kuzinduka na kuambiwa alizaa Mapacha lakini wote wamefariki ,
Rebecca alilia sana hata mumewe alipokuja kumfariji hakunyamaza,
Miaka ikakatika hatimae miaka 7 ikatimia ,
Familia ya Mr Benson ilimpenda sana yule mtoto huku mtoto akiita "mama "na mke wa Benson akijibu "mwanangu,,"huku Siri ikibaki kwa baba yaan Mr Benson mwenyewe.
Yule mtoto walimpa jina la celena na alijaaliwa uzuri haswa ,
Siku moja mama yake alimchukua waende super market ,wakapanda kwenye gari yao ya kifahari na safar ikaanza,
Wakiwa njian gar ilikuwa inatembea taratibu huku mke wa Benson akiongea na sim ,
Selena akatupa jicho nnje
Akamuona kaschana makamo kama yake kachafu na kanaokota makopo ,alipokaza macho vzr akashangaa na asiamin macho yake ,kale kasichana kalifanana nayeye kila kitu,
Celena akamwambia mama yake asimamishe gari , mama yake bila kujua akasimamisha , celena akashuka na kumkimbilia kale kaschana na alipomfikia akaanza kumshangaa,
""Wewe ni mimi ,,""!!!
Celena aliongea na kumshtua kale kasichana wakakutanisha macho,
Walijikuta wanasisimka na mapigo yao yanakwenda spidi ,
Kale kasichana hakuamini macho yake kama kuna mtu anaweza kufanana nae kiasi kile ,yaan kasoro yao ni celena alikuwa kavaa nguo za garama na kale kasichana kamevaa nguo chafu ,
""Unaitwa nani ..""
Celena alijitahid kumuuliza huku anamshangaa ,
"Naitwa Celina ,,""
Kale kasichana kalijibu .
Celena akaduwaa ,akashangaa huyu mtoto alifanana nae eti anaitwa Celina wakati yeye anaitwa Celena , naukumbuke ndugu msomaji kuwa Hawa watoto wamefanana kila kitu mpaka mambo yao,
"We celenaaaa,,""""
Mama yake celena aliita huku anakimbia upande uleule waliposimama wakina celena ,
Itaendelea.